Ijumaa, 8 Novemba 2024

URITHI wa Bibi 12

 Story....... URITHI WA BIBI EP.12 

Mtunzi..........Steven Morgan


WhatsApp..............+255659115223


Karibu tena kwenye mwendelezo wetu wa story yetu ya URITHI WA BIBI sehemu ya12. Najua nipo slow Sana ,Mambo ni mengi muda mchache . Watu wanataka kuburudika na kuelimika kwa kupata ufahamu wa Mambo mbalimbali kupitia story. Mambo mazuri hayahitaji haraka,Usinichoke , endelea kunifuatilia ili upate kuyajua Yale ambayo hukutarajia kuyajua kamwe.

 

Kama kawaida pale tulipoishia ndipo tunapo anzia:


ILIPOISHIA.....🖋️


"Mh! Jina gani hilo mzee wangu! Na kwanini likushtue hivyo?"

" Kijana wangu hilo jina ni lilikua ni la mfanya kazi wangu wa ndani,lakini kwa Sasa huyo mtu NI hadui yangu mkubwa,najua huko aliko Chuma wa morogoro Ndolelo, anataka alipe kisasi kwangu na familia yangu .Chuma ni mchawi Yani ni binti hatari Sana.!!!!"


" Mzee Foya, samahani kidogo ,unajua Chuma Mimi ni mke wangu,Na nilishaona  Mambo ya hajabu pale nyumbani,nahisi huenda akawa ndio huyohuyo binti unaye mzungumzia."


" Ndio huyo huyo bila Shaka,kijana,unatakiwa ujiongeze,japo Mungu yupo lakini unatakiwa ujiongeze raha sivyo utapotea."

" Sasa mzee wangu Mimi sielewi chochote Cha kufanya,nilishawahi kumshilikisha mchungaji ,lakini mchungaji alinishauli kumwomba mungu tu zaidi."

" Kijana mchungaji yupo sahihi kabisa , Mungu kwanza lazima umtangulize Kisha mengine ndio yanafuatia. Kama hutojari tafuta siku moja  baada au kabla ya kumaliza kazi yangu,nikupeleke kwa mtaaaramu mmoja yupo huko huko morogoro vijijini mgeta ,huyo anaitwa "Mganga Alumbile Kalumba" kiboko ya vibwengo wote,atakucheki na atakukinga dhidi ya hadui yako. Mimi mwenyewe mpaka Leo niko salama ,ni kwa  ajili yake japo Mungu ndio mkuu katika hayo.Nadhani umenielewa?"


"Nimekuelewa bosi wangu ,wacha nikafanye kazi tutaendelea kuwasiliana"


Endelea 👇.

Basi , tukaendelea kufanya kazi na jamaa yangu Mwambe. Lakini nilikua na mawazo Sana juu ya Mke wangu Chuma.

Tulifanya kazi mpaka jioni,tulibakiza sehemu ndogo Sana ya kazi, bosi mzee foya alitugea nusu ya pesa ,tuligawana na jamaa yangu Mwambe Kisha tukaondoka.


Mimi nilishika njia yangu baada ya kuagana na Mwambe ,nilitembea kwa miguu kwa muda mrefu kwani , nilijisahau  hata kupanda gari,kutokana na wimbi zito la mawazo juu ya Mke wangu Chuma.Nilipokuja kushtuka nilijihisi maumivu ya miguu,ndipo nilipopanda gari ili niwahi nyumbani maana giza lilishaanza kutanda.


" Hodi hodi mke wangu!"

Kimya.

"Hodi hodi mke wangu Chuma!"

Kimya.

"Uuuwiiii! Jamani! Kuna mtu ndani huku?"

 

Nilipiga Sana hodi lakini sikuona dalili yoyote ya mke wangu Chuma kuitika au kufunga mlango maana nilishika kitasa na kugundua kua mlango ulikua umefungwa .

Nilishangaa lakini dakika ileile nikiwa nipo pale nje mlangoni mwa chumba changu,nilianza kuhisi kizunguzungu kikali Sana,mpaka kichwa kikaanza kuuma,nilianguka pale pale mlangoni kwangu chini puuuuu! Nilipoteza fahamu sikujua Tena kilicho endelea muda huo.


"Hahaha hahaha hahaha aaaa!, Ongera Sana Chuma, unatakiwa kua makini Sana na vita iliyopo mbele yako."

"Asante Sana mamangu kwa msaada wako wa kua bega kwa bega na Mimi."

"Usijari Chuma tupo pa moja ,kwa Sasa ngoja nikuache najua unajua nini Cha kufanya ."

Mama yangu yule mkenya aliniaga Kisha akapotea Kama mwale wa radi. Muda huo tulikua tupo palepale chumbani,hata mume wangu Sadi alipokua akigonga hodi tulimsikia,ila sikutaka kumfungulia sababu tulikua kwenye Mambo yetu ya Siri. Hivyo niliamua kumroga na kumzima ufahamu.

Nilimchukua mume wangu kichawi kutoka pale nje alipoanguka na kuja ndani mpaka kwenye Kochi bila ya yeye kujijua.

Muda huo nipo kwenye gwanda la kichawi,nilijua mipango yote aliyo panga mume wangu Sadi kupitia kiganja chake,nilitambua kua alionana na hadui yangu mzee foya na kupanga kwenda kwa mganga Alumbile Kalumba ambaye ndie Alie muua Bibi yangu Mbokeleni,au Bibi Chuma. 

Ndugu msomaji kumsoma mtu na kujua dhamira yake na mipango yake ya baadae ni elimu ndogo Sana ambayo si uchawi bali ni utaaramu ambao hutumiwa hata na wanajimu au watabiri wa nyota. 

Ningependa kuelekeza hapa lakini hii ni ishu nyingine ila nitamwomba ndugu mwandishi siku moja baada ya kumaliza story hii,nitakuja na somo la fomula maaarumu kwaajili ya kusovu Mambo madogo madogo bila kwenda hata kwa mganga. Na nitamwomba afungue group la WhatsApp kwa ajiri ya somo hilo.


Basi turejee ,kwenye story yetu, mume wangu alionekana kulala usingizi kabisa,ilikua imeshafika saa mbili kasoro Usiku. Nikatenga chakula mezani maana nilijua kua mume wangu ana njaa Sana.

Nilipomaliza kutenga chakula ,nilimuamsha . 

"Mume wangu amka kutoka kwenye usingizi batiri!"

Nilimuamsha mume wangu kwa sauti ya mamraka ya Lusifa. Nae aka amka kwa kushtuka ghafla huku akivuta pumzi Kama mtu Alie kua amekabwa.

" Nipo wapi hapa?"

"Jamani mume wangu si upo nyumbani hapa kwa mke wako Chuma?"

"Mbona sikumbuki niliingia muda gani humu ndani mke wangu! Nini kimenitokea?"

Mume wangu aliendelea kuniuliza maswari! Lengo langu la kumrudishia ufahamu ,ili aweze kula chakula kwa raha.Lakini naona mwenzangu anazidi kuniuliza maswari ya kushangaza.

Ndugu msomaji ngoja nikupe ufahamu kidogo ,siku zote mtu alie tolewa ufahamu kichawi, hata akila chakula hawezi kukiona kitamu Kama wewe unavyo kiona. Mtu alie tolewa ufahamu hawezi kuhisi kichefuchefu Wala hawezi kuhisi uzuri au ubaya wa chakula . Aliye tolewa ufahamu ana uwezo wa kula hata mavi bila kinyaa,lakini wewe mwenye ufahamu wako huwezi kula hivyo. Mfano mtu Alie wekwa Msukule au ndondocha ,huyu nae ametolewa ufahamu ,ana uwezo wa kula chochote kibichi au kimewiva,kichafu au kisafi,pia wanakula mpaka unga wa ugal au pumba za maindi Kama nguruwe bila kujisikia kichefuchefu.  Hi yote ni kutokana na kuzimwa kwa ufahamu ambao umebeba sensa muhimu za mwili.


Ok,tuendelee Sasa na story yetu, kiukweli sikutaka mume wangu Sadi ale chakula akiwa kwenye hari ya kutokua na ufahamu sababu najua madhara yake Kama hayo niliyo yaeleza hapo juu.


" Mke wangu nini kimenitokea Mimi au ndio unaniletea ...... unaniletea.....!!!" Mume wangu Sadi kwakua fahamu zake zimerudia ameanza kuhisi Mambo flani kwangi.

"Nakuletea nini tena mume wangu hebu kula kwanza."

"Si unaniletea uchawi wako siwezi kula hiko chakula chako mchawi mkubwa wewe!!"

Duh! Mume wangu akaanza kunisanukia kua Mimi ni mchawi. Lakini kabla sijamjibu chochote mara ghafla akaja mkuu wetu wa uchawi akiwa katika umbo la kutisha Sana,na akajionesha kwa kila mtu pale ndani ,Yani jinsi alivyokuja hakujiweka paswadi za kuto onekana na mtu wa kawaida,hivyo hata mume wangu Sadi alimuona pia mkuu wangu kwa urahisi.

" Chuma kwa nini unamlembea mtu mwenye kiburi? Maliza kazi Sasa hivi!"


Wakati mkuu anaongea hayo,. Sadiki mume wangu alishazimiaga muda,kwani hakuweza kudumu kumtazama mkuu Alie kua anatisha Sana. Hata wewe ndugu msomaji ungekuwepo nadhani,ungekua wa Kwanza kuzimia au kufa kabisa.


Ndugu msomaji unajua kua mwili wa mwanadamu umeumbwa na kuwekewa mipaka maarumu katika utendaji wake wa kazi mfano kutazama na kuona,mwanadamu kawekewa mipaka , unaweza ukawa na uwezo wa kuona na kutazama vitu vidogovidogo vya kutisha lakini siku moja ukikumbana na kitu kinachotisha zaidi ,mafaili na system ya ubongo hushindwa kufanya kazi hatimaye mtu huyo anaweza kupoteza fahamu au kufa kabisa! Ili uweze kuona vitu vya kutisha zaidi bila kudhurika inakubidi uwe na utukufu zaidi au inakubidi uwe na Roho ngumu Sana na uji update vya kutosha.


Mume wangu alikua na Roho nyepesi Sana ,alizimia!!,

Kwakua mkuu ameniamuru kumaliza kazi bila kulemba muda uleule ,sikulaza damu nilimkata Sadi kichawi,kwa ajili ya kafara .Namaanisha nilimchukua Msukule Sadiki kwaajili ya kafara.

Mkuu alifurahi Sana.

" Chuma hongera , nadhani unajua nini kinacho fuatia ,kwaheli tuonane badae kidogo kilingeni."

Mkuu aliniaga Kisha akaondoka . Mimi nilimchukua Sadi nikawafanya wakawa wawili Kama mapacha Yani nafsi iliyo hai niliichukua na mwili wa kufoji niliuweka kitandani ukiwa hai Ila ulikua haujielewi.

Nilingoja ifike hasubui ili nitengeneze kisa kabla ya mkasa. Mida ilizidi kwenda ,Usiku ukakomaaa,nilienda kilingeni kuonana na mkuu,ndugu msomaji kilingeni ni sehemu yoyote ambayo watu wowote wanaweza kukutana kwa pamoja na kufanya wanayo fanyaga Kama kucheza draft,kucheza usoro au karata au kupiga story. Lakini sisi wachawi kilingenikwetu,tunakutana pia kwa ajiri ya Mambo yetu na dharula.


Basi ,mkuu aliniamuru nitengeneze kisa ambacho kila mtu katika jamii ataamini kua Sadi kafariki kihalari ! Au bahati mbaya.

Nikatengeneza ajari ya kichawi ili kesho nimbabatize Sadi akiwa kwenye mwili wenye nafsi mfu. Baada ya kumaliza nikaondoka kurudi nyumbani,nilimkuta Sadi amelala fofofo.

Asubuhi ilipowadia rafiki yake Sadi walio enda kufanya kazi wote Jana alipiga simu. Simu iliita niliitazama nikaona jina la Mwambe, mara ghafla Sadiki mume wangu akashtuka usingizini na akachukua simu na kuipokea .

" Halloo mwambe,haisee nakuja Sasa hivi rafiki yangu,nimechelewa Sana kuamka,nakuja Sasa hivi!"


Mume wangu Sadiki alikurupuka bila kudai chochote kisha akachukua begi lake akalibeba mgongoni bila kunawa uso akaondoka. 

Alipokua barabarani nami nilimfuatilia nyumanyuma nikiwa kwenye hari ya kichawi ya kuto onekana na mtu wa kawaida. Niliona gari ndogo likija kwa Kasi upande ule ambao Sadi alikuwepo ,nilimzubaishasadi kichawi na kumpa kizunguzungu Cha ghafla,akajiingiza mwenyewe barabarani kwenye kumi na nane ,dereva alishindwa kumkwepa Wala hakupiga bleki ,alimgonga Sadi kwa Kasi ileile aliyo kua anakuja nayo!! 

Sadi alipezwa juu Kama karatasi akatua chini kwa kujipigiza kwenye Rami,alipasuka vibaya Sana !!!!   Kisha Mimi nikaenda kwenye mwili wa Sadi nikafanya yangu Kisha nikaondoka bila kuonekana na mtu.

Nilirudia nyumbani na kuendelea na shughuri zangu. Baada ya masaaa kadhaa ,taarifa zilinifikia na kila mtu alikua kua Sadi amepata hajari amefariki.mwili wa Sadi uliifadhiwa mochwari na ulichukuliwa na ndugu yake mmoja kesho yake Kisha ukasafirishwa kwenda kwao,Mimi sikutaka kwenda sababu sikutambulika na ndugu yake yoyote hivyo waliniona Kama  awala tu!


.............. Itaendelea..............

............... .................. ..............

................ ................ ...............

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni