Ijumaa, 8 Novemba 2024

URITHI wa Bibi 14

 Story.......... URITHI WA BIBI EP.14


Author........ $teven Morgan.


📲.............. 0659115223


ILIPOISHIA episode 13.

Tuliendelea kusubiri Kisha tukaroga ili mzee foya ajisikie kwenda chooni,mida ileile tulisikia sauti ya binti akilia kilio Cha ukweli na sio Cha mahaba ,yule binti akatoka mbio akatupita pale sebuleni bila kutuona akatoka nje huku akiwa amejifunga kanga moja ,akaondoka zake ,nasi tulienda hadi chooni kwa mzee foya na kumkuta ametoa macho huku damu zikimtoka puani. Tukajua kua tumesha maliza mchezo ,tulicheka Sana Kisha tukatoweka kurudi nyumbani.


.............. ENDELEA...................


Baada ya kurudi nyumbani nikiwa Mimi na mama mkenya,tulijipongenza kwa kazi nzuri tuliyo ifanya.

Baada ya hapo , nikachukua kioo changu Cha urithi alicho niachiaga bibi. Nikapiga Rada zangu ili nihakikishe kwa Mara nyingine Kama mzee Foya atakua amekufa kweli au lah?


Nikatazama kwa makini Sana ,lakini huwezi amini,mzee Foya nilimwona akiwa mzima wa afya kabisa !!! 


"Mzee Foya mzima! Inawezekanaje?"

Nilizungumza kwa sauti ya unyonge Sana.


"Mzima!!!"

Alishtuka mama mkenya.


Ndugu msomaji kiukweli wachawi wanapokutumia jini la mauaji chooni ,huwa kupona kwako kutategemeana na ukaribu wako na mwenye enzi Mungu.


Pia ndugu msomaji kiukweli amini usiamini ,kua Kuna watu hapahapa Duniani hawarogeki hata ufanyaje au hata uwe mchawi mkubwa kiasi gani utachemka tu!!

Kutorogeka kwao haina maana kwamba wamejikinga Sana kwa Waganga! Raha Sha! Bali watu hawa wasio rogeka huwa wanakua na urinzi maarumu walio wekewa na Mungu mwenyewe kabla hawajazaliwa au kutoka kwenye matumbo ya Mama zao . Huwa hawarogeki kabisa ,na ndo maana mchawi anaposhindwa kumuua mtu wa dizaini hii, hutumia majambazi ili kumuondoa mtu huyo Duniani.


Basi , ndugu msomaji,Mimi na mama yangu ,tulishangaa Sana kwa tukio like la mzee Foya kuendelea kubaki hai. Lakini pia kiukweli mzee Foya pia alikua ni miongoni mwa watu walio barikiwa na Mungu mwenyewe kuwekewa ulinzi maarumu,japo mwenyewe alikua hajijui,alikua akihisi kwamba dawa za mganga wake ndipo zinazo fanya kazi zaidi.


"Chuma naomba unipe muda wa lisaa limoja baada ya kutoweka hapa ,Kisha nitakupa mrejesho. Naenda kuandaa bomu la kushiba kutokea Kenya lililoundwa kwa uchawi wa kizamani,naamini mzee Foya hatoweza kuishi tena."


Mama mkenya aliongea kwa kumaanisha kwelikweli!! Kisha akaondoka kwa kutoweka ghafla . Nami nilikua nasikilizia huo muda wa mrejesho alio niambia mama mkenya niusubili.


Sikuamini Sana akilini mwwngu Kama mbinu na siraha ya Mama mkenya itatosha kumuangamiza mzee Foya,maana kiukweli nilisha gundua kua mzee Foya hawezi kurogeka hata kidogo.


Muda ulizidi kwenda masaa ya kutosha yalipita! Nilishangaa kutopata ripoti yoyote kutoka kwa Mama mkenya!! 


Nilihisi kua huenda kukawa na tatizo,nikampigia simu ya kichawi,lakini hakupatikana,nikampigia simu ya kawaida pia , hakupatikana!!


Na muda ulikua umeenda kweli,ilikua imeshafika saa kumi na mbili jioni. Bado sikuelewa kilichotokea au kumkuta Mama yangu mkenya!


Lakini kipindi nafikiria hayo,Mara ghafla nikapata ujumbe wa kichawi,kwamba muda huohuo nahitajika maari flani Kuna tatizo la kujadiri kwa dharula!


Ndugu msomaji,wachawi huwa wapo monitored Yani kwa lugha nyepesi unaweza kusema kua wachawi huwa wanaonganishwa kulingana na kamati zao ama kikundi Chao,na hupeana taarifa za haraka kupitia ishara maarumu . Ishara hiyo inaweza ikawa mlio maarumu wa ngoma au filimbi, nadhani wale walio pitia mgambo au skauti au jeshi ,watakua wananielewa vizuri hapa. Yaani huwa jeshini Kuna milio tofauti ya filimbi, na ukilia mlio fulani Basi ujue kuna watu flani wanna hitajika eneo flani ,huenda ikawa viongozi pekee ndio wanao hitajika,au wanajeshi wote wa kambini wanajitajika eneo flani kulingana na tafsiri ya filimbi. 


Basi ,hata sisi wachawi tupo hivyo pia. Kina mlio flani wa ngoma nilimsikia, ninaposema niliusikia ndungu msomaji, namaanisha kwamba hata Kama ningekua kwenye kundi la watu Mia,mlio huo ningeusikia Mimi tu,labda Kama kutakua na mchawi mwingine Kati yetu nae pia anaweza akasikia.


Baada ya hapo ,sikutaka kupoteza muda, nilijiandaa Kisha nikatoweka Kama nuru iliyo zidiwa na kiza kinene.


Ndugu msomaji wachawi huwa hukutana popote pale palipo pendekezwa kwa muda huo,huenda ikawa barabarani,au chini ya mti,au pembezoni mwa mto au makaburini au njia panda. Kokote pale wachawi huweka mkutano wao na muda wowote ule huenda ikawa asubuhi,mchana,jioni au usiku.


Ndugu msomaji ngoja nikupe faida ndogo, unapotembea barabarani Kisha ukapita sehemu flani na ukasimama  barabarani au chini ya mti ukapumzika,lakini baada ya muda ukaanza kuhisi Kama Kuna kundi la watu limekuzunguuka na nywele zako za mwili haswa kichwani zinasisimka,au jicho likaanza kukucheza bila lidhaa yako,ujue wazi kua ,eneo hilo ulilo kuwepo,kina kundi la watu wabaya wanafanya Yao, na unachotakiwa hapo ni kuondoka Mara moja eneo hilo Kisha muombe Mungu kwa ulinzi zaidi.


Basi,baaada ya Mimi kutoweka ,Kama kawaida nikaenda kuibukia kwenye kilinge chetu tunacho kutanaga siku zote.Nilikuta wachawi kibao wameshafika Yani Kama walikua wakiningoja Mimi tu!


"Karibu Chuma,tulikua tunakusubilia wewe tu! Najua kila mtu hapa anataka kujua nini nilicho wahitia ."


Aliongea mkuu. Lakini Mimi nolizidi kushangaza Jambo moja ambalo nilikua sielewi kbisa! Nilikua nikiangaza macho huku na kule lakini yule Mama mkenya,sikumuona kabisa.Nilikua na hofu Sana. Mara ghafla mkuu akaonge.


"  Chuma pole Sana kwa kumpoteza rafiki pia Kama Mama yako mkenya,hatupo nae Tena hapa Duniani!!! Na hivi Ninavyo zungumza,tayari ndugu zake huko Kenya wamesha mshtukia kua amefariki na wanaendelea na taratibu zao za msiba.!!


Kila mtu alishangaa Sana pia nami nililia Sana kwani iliniuma Sana na amekufa kwa ajiri yangu.Mkuu alizidi kuongea.


"Baada ya hapo,Chuma naomba nikushahuri Jambo moja kwamba,kwanza achana na mzee Foya kwanza,Kisha muanze kumuua mganga wake Alumbile Kalumba Kisha mzee Foya atakua mwepesi tu!"


Mkuu alionge bila kujua kua mzee Foya harogeki hata kidogo.


" Chuma msalaba huu wa kulipiza kisasi Cha Bibi yako utakua peke yako mwenyewe,sitaki uwaponze wengine kwaajiri ya nafsi yako.Jipange vya kutosha Kisha Anza kumdondosha mganga Alumbile Kalumba Kisha mmalizie mzee Foya ,sawa?"


Mkuu alinisisitizia.

"Sawa mkuu" 

Nilimjibu.


"Basi Kama tume elewana kila mtu atoweke mahara hapa Mara moja na muende mkaendelee na shughuri zenu nyumbani."


Mkuu alituruhusu Kisha kila mtu alitoweka kwa stahili yake,kurudi nyumbani. Wengine walitoweka Kama radi,wengine walitoweka Kama upepo ,Yani zilikua ni mbwembwe tu za kichawi katika kuonesha uwezo.


xxxxxxxxxxx Itaendele xxxxxxxxxxxx


Je,Chuma atawezaje kumuua mganga Alumbile Kalumba? Ikiwa Bibi yake alikua bingwa lakini aliuawa na Mganga Alumbile Kalumba!!!

Je , Chuma atawezaje kumuua mzee Foya? Ikiwa mbinu zao zimeshindikana mpaka mama mkenya amefariki!  Na Chuma amesha gundua kua mzee Foya harogeki,je atatumia njia gani?


USIKOSE KUFUATILIA SEHEMU YA MWISHO KABISA YA STORY YETU YA URITHI WA BIBI EP.15. [ MWISHO ]🔌

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

URITHI wa Bibi 15

 Story... URITHI WA BIBI EP.15. Mwisho. Mtunzi....Steven Morgan 📲......... 0659115223 Naam kwa Mara nyingine tena ndugu msomaji tumekutana ...