Ijumaa, 8 Novemba 2024

URITHI wa Bibi 8

 Story............ URITHI WA BIBI EP. 8

Author............Steven Morgan.

 

Contact........... 0764655342,+255659115223.


Naaam,ndugu zangu wasomaji kwa mara nyingine tena kwa uweza wake mungu baba tumekutana Tena tukiwa na afya njema kabisa katika hii chemba yetu ya story zenye maarifa na mafunzo yenye maonyo. Poleni sana  ninyi ambao afya zenu zimetetereka kwa namna moja au nyingine kutokana na maradhi mbalimbali  ya mwanadamu. Zaidi tuendelee kumwomba Mungu zaidi maana yeye ndie anaye ponya.


Bila kuwachosha, wacha tuendelee na story yetu ya URITHI WA BIBI EP. 8

Kama kawaida , TULIPOISHIA ndipo tunapo ANZIA Ili twende sawa bila kupinda pinda.

 

TULIPOISHIA.πŸ‘‡


"Eheee ni kweli alafu nilitaka kukuuliza tangia mwanzao kua Chuma Yuko wapi? Na aliye kufa huko ni nani?"

" Mme wangu Chuma aliniaga kua anakwenda kumsalimia Bibi yake huko Kijiji Cha pili lakini inasemekana ,alipofika huko, alimkuta Bibi yake amefariki na haijulikani kilicho sababisha kifo Cha Bibi Chuma."

"Duuuh! Mke wangu,tunavita kubwa na tusipo kua makini tunaweza tukaangamia mmoja mmoja maana Bibi yake chuma ndio alikua hadui yetu namba moja ,na mganga aliniambia kua hadui namba mbili tunaishi nae nyumba moja,bila Shaka atakua ni Chuma!! Chuma ama zako ama zangu na kuanzia Sasa simtaki Tena Chuma katika familia yangu"


Mzee Foya aliongea kwa uchungu huku akimsisitizia mke wake kua Chuma hamtaki tena maana  ni hadui yao mkubwa sana hawatakiwi kuishi nae nyumba moja....


Kesho yake ikafika mazishi yakafanyika pande zote mbili watu walilala matanga kisha tarehe za kupanda msalaba zilitajwa pande zote mbili ,kule kwa Chuma msalaba utakua 15/08/20..

Na kule kwa bibi zubeda ni 14/08/20.. 

 Shughuli za mazishi kwa ujumla zilikwisha.

 

Basi baada ya mazishi kuisha ,mzee foya na familia yake walirudi kwao dar es salaam. Huku Chuma akiwa amebakia nyumbani kwa bibi yake. Siku kadhaa zilipita ,siku moja Chuma akiwa nje ya nyumba yao, nyakati za asubuhi,alitembelewa na ugeni wa ghafla!    Yaani ugeni wa kufumba na kufumbua.

"Ahaaha haaa! Usiogope Chuma ,ni Mimi ,unanikumbuka?"  " Hapana Mama kwani wewe ni nani?" Alijibu Chuma. 

" Chuma mara hii umenisahau? Basi ngoja nikukumbushe! Mimi ni yule Mama nilie kusaidiaga kule Kenya ,kipindi kileeee! Ulipokua unafundishwa uchawi na marehemu Bibi yako,na mara ya mwisho mlipata matatizo nilikusaidiaga na nilikurudisha hadi huku kwenu Tanzania nyumbani kwa Bibi yako.vipi,Bado hujanikumbuka tu Chuma?"

Ahaaa! Nimesha kukumbuka mama ,karibu sana. " Asante sana "

 Nilimkaribisha yule Mama mkenya kwani nilimkumbuka vizuri sana,aliwahi kunisaidia sana. Alikuja asubuhi sana kwa njia za kichawi.

"Chuma pole sana kwa msiba ,na nimekuja huku baada ya kupata ripoti siku chache zilizo pita kwenye kikao kikuu Cha wakurugenzi wa umoja wa Africa,moja kati ya ajenda zilizo zungumzwa ni pamoja na rambirambi ya msiba wa Bibi yako.wakuu wote wanakupa pole na wamenichagua Mimi ili nikusaidie kulipa kisasi kwa wahusika wote akiwemo mzee Foya na familia yake  na yule mganga wa mgeta Alumbile Kalumba.leo nimekuletea pesa hizi taslimu milioni mbili na laki nane Kama pole ,kwa niaba ya wanachama wote wa ndani na nje ya nchi za Africa. Bibi yako hakua mchawi mdogo alikua ni mchawi mkubwa sana na mchango wake unajulikana katika nchi zote za umoja wa Africa."

Asante sana mama yangu ,kwa upendo wenu kwangu,nafurahi Kama utakua pamoja nami katika kulipa hiki kisasi.


"Usijari Chuma tupo pamoja,ila Kuna Jambo nilisahau kukwambia kua ,wakuu wamesema kua ,hakuna kufanya msalaba au arobaini. Unachotakiwa Sasa  kuendelea na maisha yako Kama kawaida kuongeza juhudi katika kuhudhuria vikao vya kichawi na kuchawia ,hii itakusaidia kujiongezea nguvu zaidi. Pia uki hitaji msaada wowote kwangu, niite kichawi muda wowote nitakuja kukupa msahada."


Sawa mama ,nimekuelewa nashukuru sana kwa maelezo yako .Nami Nita yafanyia kazi zaidi yote uliyo nieleza. 


Basi baada ya kumalizana na yule mgeni wangu akatoweka ghafla katika uono wa macho yangu ,Yani aliondoka kichawi.


Siku hiyo nilikaa nyumbani siku nzima nikiwa peke yangu ,nilifikilia mengi sana,ilamwishoni nikapata wazo la kuhama pale kijijini !  Ukizingatia pale kijijini Sina ndugu wa karibu ninae elewana nae. Kwakua nilikua na pesa za kutosha,sikutaka kupoteza muda ,niliandaa mizigo yangu ,nilikuwa na mabegi mawili yenye kila kitu kilicho nifaa.

 Ilipofika jioni niliondoka na kuelekea Msamvu stendi ya mabasi ili niende zangu dar es salaam. Huko dar Sina ndugu Wala sijui nitafikia kwa nani! Maana bosi wangu najua amesha kua hadui yangu . Kwakua nilikua na pesa,sikua na wasi wasi . 

Nilipata Basi la Abood na Safari ilianza  na hatimae saa mbili Usiku nilifika ubungo. Sikua na sehemu ya kwenda bali nilitafuta nyumba ya wageni ili nipate kulala kwa Usiku huo. Nilipata chumba katika gesti moja ya maeneo Fulani pale tabata. Nililipia Kisha wakanipa funguo nikaenda ndani ili kuweka mizigo yangu. Nikaweka mizigo Kisha nikaingia kuoga na kubadiri nguo Kisha,nikatoka gesti nikaingia pale baa ambapo niliona watu wakila chakula na kunywa. Namimi nilichagua kukaa kwenye meza isio kua na mteja yeyote ,nika agiza chips mayai na nusu ya kuku  wa kukaanga na maji Safi ya lita moja na nusu ya Kilimanjaro.


Nikawa naendelea kula taratibu huku nikisikiliza mziki wa kizamani uliokua ukipigwa pale kaunta. Mara nikaona Kuna kijana mmoja alikua akinikonyeza na kunipa ishara za kuniita. Siku mjibu chochote lakini yeye mwishoni aka amua kuja hadi kwenye meza niliyo kaa,akachukua kiti akasogeza karibu yangu,Kisha akawa ananihojihoji.

" Binti mrembo unaitwa nani?"

"Chuma" 

"Chuma jina zuri sana,Mimi naitwa Sadi au wengine wanapenda kurefusha jina langu na kuniita Sadiki. Ok, Chuma naona hapa upo mwenyewe nami nilikaa kule mwenyewe,nikaona sio mbaya nije hapa nikuombe kampani yako ili tufurahi wote pamoja tukiwa meza moja." 


"Sawa karibu" nilimjibu yule kijana kwa urahisi kabisa bila usumbufu.

"Asante sana mrembo Chuma naomba nipe dakika 3 tu nikachukua vinywaji vyangu kule kwenye meza yangu nihamishie hapa."

"Sawa nenda." Nilimjibu. Sasa wakati anaenda kuchukua vinywaji vyake yule kijana ,Mimi Kuna kitu kikanishtua au naweza sema nilipata message ya kichawi,nikanyanyuka haraka na kwenda chumbani kuangalia vizuri huo ujumbe.............. ...............Itaendelea 

Samahani kwa kuwaletea story fupi,hii ni kutokana na sababu zisizo zuhirika.πŸ™


Je ,huo ujumbe ni upi? Je,yule kijana nae kitamkuta nini?

Mambo ni mengi muda mchache, Fuatilia sehemu ya 9 kesho .kizaa zaa kimeanza.

URITHI wa Bibi 7

 STORY............ URITHI WA BIBI EP. 7


    MTUNZI........ STEVEN MORGAN


    SIMU........ +255659115223


Naaam,Kwa mara nyingine tena, tumshukuru Mungu kwa kukutana tena ,katika episode ya 7, karibu tena katika muendelezo wetu wa URITHI WA BIBI. Bila kupoteza muda ,

 

TULIPOISHIA ndipo tunapo anziaπŸ‘‡πŸ‘‡

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


   

                                                                             Mzee foya baada ya kuria kwa muda mrefu kutokana na taarifa ya kifo cha bibi zubeda wa morogoro,alinyamaza Kisha akamwambia mkewe aketi chini wazungumze kua itakuaje?

" Mke wangu kesho inabidi niwatangulize  huko morogoro kwenye msiba  mapema,lakini Mimi nitakuja jioni sababu kuna sehemu nitapitia  kutafuta ukweli wa kifo cha ndugu yangu bibi zubeda. Na nikimjua hadui alie husika ,hama zake ,hama zangu."  Mzee foya aliongea kwa hasira sana,huku Mimi na mama Maria tukiwa tumetulia kama tumezubaa vile. Basi kwa kua muda ulikua umeshaenda,Kila mtu aliingia chumbani kulala.............         ............    .................. ....


ENDELEA...

Basi ,kwakua muda ulikua umeshaenda,kila mtu aliingia ndani kulala.  Usiku huo chuma Mimi sikuweza kupata usingizi,kwani niliwaza mengi sana ,ikiwemo suala la bosi wangu mzee foya kutaka kuchunguza kifo Cha ndugu yake bibi zubeda wa morogoro. Nilijiuliza je,akinibahini kua ni Mimi mfanyakazi wake Chuma ndie niliye husika je ,itakuaje? 

Ndugu msomaji katika vitu ambavyo ukivifanya basi ,ni lazima utaandamwa na wachawi sana, ikiwa ni pamoja na kufuatilia ishu za kishirikina zilizofanywa na wachawi, maana wachawi wanapofanya Jambo huwa hawataki mtu mwingine ajue chanzo Cha tukio,na endapo wakigundua kua Kuna mtu anataka kufuatilia ukweli wa Jambo Fulani ambalo lilifanywa na wao ,basi hapo vita itakua imeanza .


Niliwaza na kuwazua bila kupata jibu ,usingizi sikupata kabisa ,lakini mwishowe nikatoa kioo changu Cha kichawi,Kisha nikamuita mkuu wetu wa uchawi . Mkuu alitokea palepale ndani ya kioo , " Chuma unashida gani ,naona umeniita" mkuu aliongea, " nikweli mkuu nimekuita Kuna Jambo linanitatiza sana,tulifanya mauaji, lakini bosi wangu anataka kuchunguza ukweli wa kifo Cha ndugu yake,nina hofu endapo akinibahini itakuaje? Nisaidie mkuu".   Nilimueleza mkuu kinacho nisibu.  " Chuma hilo mbona ni Jambo dogo sana,lakini pia usipokua makini huwa ni Jambo kubwa sana. Sasa,chakufanya unakijua chukua kioo chako hiko baada ya Mimi kuondoka ,muite bosi wako humo,Kisha umuhoji kua atakwenda kwa mganga gani,Kisha umfuate huyo mganga na umpe rushwa yoyote ile iwe ya pesa au ya mwili ilimradi tu aupindishe ukweli kwa mteja wake,hapo utakua umeokoka. Hahaha hahahaha hahahahaaaaaaa!!! Kwa heri!" 

 Mkuu baada ya kunipa maelekezo ,alicheka sana ,Tena cheko nzito mpaka nilitaka kuogopa!

Ndugu zangu hapa ngoja kidogo tujifunze kitu,wakati mwingine waganga sio wa kuwaamini sana. Haswa pale unapoona kua tatizo lako kila unapotibiwa hauponi ,anakubadirishia kila dawa lakini hauponi. Ukiona hivyo maranyingi huwa ,huyo mganga wako unaye mtegemea kutatua matatizo yako kila wakati,tayari amesha anza kupotoshwa na wachawi ,anakula rushwa na badala ya kukutibu anakuongezea maumivu kwa dawa anazopewa na wachawi .


Tuachane na hayo, turejee pale chumbani nilipokua ,baada ya kupokea muongozo kwa mkuu, nikachukua kioo changu tena,hua nakiamini sana,ni kioo ambacho alinipaga bibi. 

Nikakikazia macho kile kioo Kisha nikamuita bosi wangu mzee foya kwa sauti ya mamraka isiyo pingika. Palepale mzee foya bosi wangu,akatokea ndani ya kioo changu. Nikaanza kumuhoji maswari kwa maneno ya mamlaka yasio pingika naye alinijibu vile  vyote anavyo vikusudia kuvifanya kutoka moyoni.

Hapo nilijua kua mzee foya kesho anatarajia kwenda kwa mganga gani,hivyo kabla yeye hajafika nilazima nifike Mimi Kwanza ili nimrubuni yule mganga wake ili bosi asije akaujua ukweli.

Basi ,Kama waswahili wasemavyo ,kua awike asiwike ni lazima kuche na Usiku wa deni haukawii kuisha. Ndivyo ilivyo kua ,nilishtuka asubuhi ya saa kumi na mbili na nusu baada ya mke wa bosi kunigongea mlango na kunitaka nijiandae kwa safari ya kurudi morogoro kwenye msiba.

Kiukweli sikujua usingizi ulinikamata muda gani lakini ndo ikawa hivyo nimeshtuliwa kumesha kucha. Bila kupoteza muda Kwanza nikachukua kioo Tena nikamuita Bibi chapu Kisha nikampa maelekezo ,kua bosi wangu mzee foya leo anataka aende kwa mganga mmoja anayeitwa " Aumbile kalumba" anayepatikana mgeta. Kwa hiyo nilimpa maelekezo Bibi kua amfuate yule mganga asubuhi ileile amrubuni na ampe rushwa ya pesa ili aupindishe ukweli wa kifo Cha Bibi zubeda. Bibi alinielewa Kisha akatoweka . Nami nikaenda kuoga Kisha nikawaogesha na watoto nikawavalisha ,nami nikajiandaa vyema ,tayari kwa Safari.

 

"Chuma toka twende maana muda umeenda sana" alikua ni mke wa bosi akiniita ili tuondoke,muda huo nami nilishabeba begi langu nikatoka chumbani kwangu na kuelekea sebuleni,ambako nilimkuta mke wa bosi na bosi mwenyewe mzee foya .


"Safari njema mke wangu,muende salama nami jioni au Usiku nitakua nishafika huko msibani" aliongea mzee foya Kisha akatusindikiza hadi ubungo stendi ya mabasi .Tukapanda Basi la abood la saa mbili ,tukaagana na mzee foya Kisha yeye akageuza akarudi nyumbani baada ya gari kuanza kuondoka.  Mipango ya mzee foya nilishaijua na tayari nimeshaitafutia korokwini ,sikua na wasiwasi tena kwani nilijua tu kwamba Bibi ameshaenda kuvuruga mitambo. Safari iliendelea huku njaa zikiwa zinauma kutokana na kutokula asubuhi. Wakati mwingine nilitapika ndani ya gari,sijui kwanini ila nafikiri ni kutokana na kutokula au kutokua na mazoea na Safari ndefu za mara kwa mara.  Baadhi ya sehemu gari lilidimama ,tulichimba dawa na kupata chakula kidogo Kisha Safari iliendelea.

  

Hatimaye tulifika Msamvu stendi ya mabasi ya morogoro saa Saba mchana.Tukachukua usafiri wa taxi ukatupeleka milimani kwetu huko Ndolelo kwenye safu za milima ya ulugulu. Baada dakika Kama kumi na tano tulifika sehemu tulishuka kwenye gari,Mama alimlipa dereva Kisha sisi tuliendelea na Safari yetu kwa miguu kwani gari lilishindwa kusonga mbele kutokana na ufinyu wa barabara. Tukapandisha vilima huku Mimi nikiwa nimembeba mtoto mmoja na Mama nae amembeba mtoto mmoja.  Jasho zilituvuja wakati mwingine tulipumzika Kwanza kwani mama Maria mke wa bosi hakuzoea Safari za vilima na miteremko mikali. 

Tuliendelea na Safari ,hatimaye yapata saa Tisa na nusu ,tunafika msibani kwa marehemu Bibi zubeda. Tulikuta watu wengi sana wakiwemo majirani na ndugu wengi sana na watoto wa bibi zubeda,walikuja watu kutupokea mizigo yetu lakini Mimi niligoma kupokelewa begi langu nililibeba mwenyewe.Tukapelekwa ndani sebuleni kupumzika jamvini kwani tulikua tumechoka sana.


Tuachane Sasa na habari za Chuma huko msibani ngoja tumuone sasa Bibi yake Chuma na Safari yake ya uvurugaji wa mitambo.


Bibi Chuma au Bibi Mbokeleni bila kuchelewa baada ya kupewa taarifa na mjukuu wake Chuma ,alifunga Safari ya kichawi kwenda kwa huyo mganga  Alumbile Kalumba huko mgeta. Ninaposema alifunga Safari ya kichawi namaanisha sio Safari ya kawaida bari ni Safari ya MWENDO KASI Yani ni Safari ya kufumba na kufumbua Yani ni chapu kwa haraka.

Ghafla! Tayari Bibi Mbokeleni amejikuta ametua kwa kishindo kikari sana ,nje ya nyumba ya mganga Alumbile,mpaka mganga akashtuka na akatoka nje ya kibanda chake cha msonge kilicho ezekwa kwa nyasi. Uso kwa uso na Bibi Mbokeleni, " Mbona umekuja kwa kitisho ,umekuja kwa Shari au kwa heri?" Aliuliza mganga Alumbile. " Ha ha haaa haaaa haaa! Nimekuja kwa heri kabisa,wala sina Shari na wewe, ila Kuna mtu atakuja mchana wa leo ,anaitwa Foya,huyo ndio nina shari nae. Kuna ndugu yake tumemuua Mimi na mjukuu wangu anaitwa Chuma,Sasa huyu mzee foya atakuja kwako kupata ukweli kuhusu kifo cha ndugu yake."

" Sawa hiyo ni kazi yangu na huyo atakua ni mteja wangu wa siku nyingi, Sasa wewe mchawi unataka nikusaidie nini? "


" Naomba sana mganga,uufiche ukweli wa Jambo hili ,nitakulipa kiasi Cha pesa kikubwa mara mbili na kile atakacho kupa  mteja wako.  Na ukilikataa ombi langu ,utakua umeitangaza vita Kali isiyoweza kumalizika ." 


" Kwa hiyo umekuja hapa kwa mganga Alumbile Kalumba,kuja kunitisha na kunitangazia vita?, Mimi sijawahi kutishwa na kigagura wala mchawi yoyote yule,Kama wewe ni mchawi kwa nini usi zuie kuumbuka kwenu? Nafikiri wewe Bibi hunijui vizuri, labda ngoja nijitambulishe kwako vizuri maaana naona umekuja kwa Shari. Mimi ndio mganga Alumbile Kalumba,kiboko ya majini na wachawi wakubwa na wadogo Kama wewe na timu yako. Sitoi wala sipokei rushwa kutoka kwa kiumbe hai yeyote yule. Sipindishagi ukweli kua uongo hata siku moja,pia simuogopagi kiumbe hai yeyote yule na ukitangaza vita na Mimi,hakikisha unajiandalia kabuli lako Kwanza.Nadhani mpaka hapo utakua umenielewa Bibi unaweza ukaondoka kwa amani huwa sitaki mzaha."


Bibi Chuma jitihada zinaonekana kugonga mwamba baada ya mganga Alumbile kumkatalia ombi lake la kupotosha ukweli.


" Hahaha! Hayo ni maneno tu mganga,huna lolote wewe,Mimi ndio Bibi Mbokeleni au Bibi Chuma ,mchawi niliye kubuu nisie wezekana,kwa kua hutaki kunifanyia kazi yangu ,umesha tangaza vita na kamati ya ufundi jiandae kuiyaga Dunia mganga raha sivyo kubaliana na Mimi kunifanyia kazi yangu."


"Bibi Chuma Kama nilivyo kueleza Mimi huwa sitishiki kwa lolote na huwa nangoja hadui anianze na Mimi namaliza kabisa,kwa hiyo nakupa muda Kwanza kajiandalie kaburi lako kabisa na Kama Kuna URITHI wowote nenda kauache kabisa maana ukipambana na Mimi Sasa hivi hutopata  bahati ya kua hai ndani ya lisaa limoja lijalo Mimi ndio Alumbile kiboko ya wachawi Sina muda Tena wa kuzungumza na wewe ondoka haraka hapa kabla sijakudhuru!" Aliongea mganga kwa hasira sana.


Bibi Chuma akajifanya mwamba hakutaka kuondoka akataka kuujaribu uwezo wa mganga Alumbile,bila kujua kua Alumbile huwa hajaribiwi! Bibi Chuma akarusha uchawi mzito wa maangamizi lakini hakufua dafu kwa mganga Alumbile,alitulizwa kiwepesi Kama pasi ya mpira wa miguu. Alumbile bila huruma akapiga pigo moja takatifu linalo itwa mwana ukome,Bibi Chuma alirushwa juu Kisha akajipigiza chini kwa kishindo na habari yake ikawa imeisha, alikufa palepale!!

" Nilikwambia wewe Bibi lakini ulikua mbishi Sasa habari yako imeisha nenda kwako sitaki mzoga hapa"  aliongea mganga Kisha akaupoteza mwili wa Bibi Chuma kimiujiza na kuurejesha nyumbani kwake ili waje wamshtukie ndani kwake akiwa maiti.

Baada ya masaaa machache mbeleni Mzee Foya aliwasiri kwa mganga Alumbile Kalumba ,alikuta Kuna watu wanne wakingoja kuhudumiwa, alisubiri mpaka ilipofika zamu yake na yeye akaingia kibandani.


" Karibu sana mzee Foya ,pole sana na Safari pia pole sana kwa msiba na pole sana kwa matatizo." 

" Asante sana mganga Alumbile sijui umejuaje Kama Nina msiba na hayo matatizo?"

 " Mimi ni mganga wa kweli ,kabla ya wewe kufika hapa,hadui yako tayari alishafika hapa maana alijua kua wewe utakuja hapa." 

" Hadui yangu ni nani ,na alikuja hapa kufanya nini?" 

" Kua mpole bwana Foya wanasemaga waswahili kua kikuracho ki nguoni mwako.Hadui yako unaishi nae wewe mwenyewe tena nyumba moja! Ila hadui namba moja nimesha ndio alie kuja hapa leo. Kunirubuni kua nisikwambie ukweli wa kifo cha ndugu yako ,na akataka kunidhuru baada ya kumkatalia lakini hakuweza nikamdhuru yeye na kumuua kabisa.!"

" Duh! Unaweza kuniambia huyo ni nani alikuja na ukamuua?"     " Usiwe na haraka foya kila kitu Kiko wazi utajua tu mwenyewe taratibu. Sina Cha kufanya kwako kwa Sasa sababu kinga nilisha kupatia na familia yako yote zaidi muombe sana mungu akusaidie zaidi. Lakini kumbuka kua hadui yako unaishi nae nyumba moja ila sikwambii ni nani,sababu unaonekana kua una hasira sana ,kua mpole Leo au kesho utamjua hadui yako .Nenda tu msibani na ukifika huko Kuna msiba mwingine utausikia ,huyo aliekufa ndio hadui namba moja na hadui  mwingine aliye bakia ndio unashi nae nyumba moja,ila usije ukachukua sheria mkononi utafungwa haya mambo yataisha kimya kimya."

"Sawa mganga Alumbile Mimi nimekuelewa sana na nitakua mpole Kama ulivyo sema wacha niende niwahi msibani." 

Mzee foya alia aga Kisha akaanza Safari ya kurudi Ndolelo msibani .


Tuachane na mzee Foya,turudi kule msibani kwa marehemu Bibi zubeda.

 Chuma akiwa na Mama Maria na watu wengine kibao wakiwa wametulia pale ndani sebuleni kwenye jamvi au mkeka, Chuma Kuna kitu kilimshtua sana,machale yakamcheza Kisha akamwambia mama Maria  mke wa mzee Foya, " Mama samahani naomba niende nyumbani mara moja kwa Bibi yangu sio mbali sana ni hapo tu Kijiji Cha pili." 

"Sawa Chuma nenda ila usichelewe kurudi maana si unaona hawa watoto wanavyo sumbua?" " Sawa mama nitawahi sana kurudi Wala sita chelewa."


Binti Chuma alitoka ndani na kuondoka kuelekea kwao kwa Bibi yake Mbokeleni,Chuma akiwa na begi lake mgongoni Safari inaendelea kupanda na kushuka vilima Chuma alishazoea. Chuma alikua Kama amechanganyikiwa flani hivi! Japo kinacho mchanganya hakukijua kabisa ila ,alikua na hamu kubwa ya kufika nyumbani kwa Bibi yake Mbokeleni. Masikini Chuma bila kujua kilichomkuta Bibi yake ni kipi aliendelea na Safari yake.

Hatimaye Chuma anafika nyumbani kwa Bibi yake Mbokeleni akiwa na presha bila kujua sababu ni nini?

Nyumbani palikua kimya sana ,nikaangalia mlango wa nyumba ya Bibi ,ulikua umefungwa kwa komeo,nikafungua komeo nikausukuma mlango lakini,haukufunguka. Unaonekana ulifungwa kwa ndani .nikatazama huku na kule hakuna aliye niona nikaingia ndani kichawi .

Ghafla !  Namwona Bibi yupo kitandani amejinyoosha huku macho yamemtoka kweli kweli Yani ukimtazama kwa mbali,unaweza ukamwona Kama amevaa miwani kumbe ni macho yamemtoka bibi yangu! Nilishtuka sana kwani nilianza kuziona dalili za hatari kubwa .Nikamsogelea Bibi nikawa namwamsha lakini hakuamka,ndipo nilipo gundua kua Bibi yangu Mbokeleni ameshafariki.!! Nilichanganyikiwa sana nikaanza kulia huku machozi yakinivuja Kama maji lakini nikajikaza,nikaanza kukusanya vitu vyote muhimu haswa dhana za uchawi na nikaenda kuzificha nje mbali kidogo na nyumbani,niliondoka kichawi na nikarudi kichawi. Nikatuma meseji ya kichawi yenye  taarifa ya msiba wa Bibi , wachawi wote wa hapa kijijini wao ndio watu wa Kwanza kupata taarifa .

Kisha nikaaanza kulia kwa sauti mpaka majirani wakanisikia wakaanza kuja nikawaeleza nilicho kikuta ndio hicho ila sijui chanzo. Baada ya muda watu walijaa kwa wingi ,walitoa vitu vyote nje, vijana walifunga maturubai na baadhi ya watu walipeleka taarifa mpaka Kijiji Cha pili. 

Nilishangaa sana kwani baada ya muda mchache ,baadhi ya watu nilio waona kule kwenye msiba wa Bibi zubeda wamekuja pale nyumbani na kunipa pole wengine waliuliza kilichotokea lakini niliwaeleza hari harisi niliyo ikuta. Ndipo nilipo amini kua taarifa za msiba zimesha fika mpaka Kijiji Cha pili. Mipango ya msiba ikapangika kua kesho yake ndio maziko yatafanyika sawa na msiba wa kule Kijiji Cha pili.


Tumuache Chuma kidogo na majanga yake , ngoja tukaone kinachoendelea kule msibani Kijiji cha pili kwa marehemu Bibi zubeda. Maana Mzee Foya amesha anza kupanda na kushuka vilima karibia atafika msibani.

Msibani kwa Bibi zubeda kulitawaliwa na vilio vya kila aina ,Yani ni kelele tu ndizo zilizo tawala. 

Mara ghafla! Mzee Foya aliwasiri msibani alianza kuwasalimia watua alio wakuta pale nje huku wakipeana pole ya msiba. Aliingia ndani alikutana na mkewe huku watoto wake wakiwa wanacheza na watoto wenzao. Alimchukua mke wake na kwenda kukaa chemba ili waongee kidogo.

" Mama Maria mke wangu,kifo Cha ndugu yangu ,sio Cha heri za  mwenye enzi Mungu,kimesababishwa na mwana wa adamu,na nikimgundua ,hakika sita muacha mzima na Leo mganga wangu ameniambia kua nitajua hilo,Kuna ishara nitaziona "

"Sawa baba Maria lakini pia Kuna msiba mwingine umetokea kule Kijiji Cha pili..!"


"Eheee! Sasa hiyo ndio ishara yenyewe ya Kwanza niliyo ambiwa na mganga Alumbile Kalumba,na huyo aliekufa ndio hadui yetu namba moja na mwingine..... Mwi..ngine!"   "Sawa baba maria lakini unajua aliye kufa huko ni nani? Na hujiulizi kua Chuma Yuko wapi hapa?"


" Eheee ni kweli alafu nilitaka kukuuliza tangia mwanzao kua Chuma Yuko wapi? Na aliye kufa huko ni nani?"

" Mme wangu Chuma aliniaga kua anakwenda kumsalimia Bibi yake huko Kijiji Cha pili lakini inasemekana ,alipofika huko, alimkuta Bibi yake amefariki na haijulikani kilicho sababisha kifo Cha Bibi Chuma."

"Duuuh! Mke wangu,tunavita kubwa na tusipo kua makini tunaweza tukaangamia mmoja mmoja maana Bibi yake chuma ndio alikua hadui yetu namba moja ,na mganga aliniambia kua hadui namba mbili tunaishi nae nyumba moja,bila Shaka atakua ni Chuma!! Chuma ama zako ama zangu na kuanzia Sasa simtaki Tena Chuma katika familia yangu"


Mzee Foya aliongea kwa uchungu huku akimsisitizia mke wake kua Chuma hamtaki tena maana  ni hadui yao mkubwa sana hawatakiwi kuishi nae nyumba moja....


Kesho yake ikafika mazishi yakafanyika pande zote mbili watu walilala matanga kisha tarehe za kupanda msalaba zilitajwa pande zote mbili ,kule kwa Chuma msalaba utakua 15/08/20..

Na kule kwa bibi zubeda ni 14/08/20.. 

 Shughuli za mazishi kwa ujumla zilikwisha.


Je, unafikiri nini Kita endelea? Je, Chuma ataenda kuungana na mzee Foya na kurudi Tena dar es salaam? Je, Chuma atabaini nini kuhusu kifo Cha Bibi yake? Je,vita vikali vitakua kati ya Chuma na mganga Alumbile Kalumba! Au kati ya Chuma na mzee Foya? Usikose kufuatilia sehemu ya 8 ya URITHI WA BIBI, utapata majibu ya maswari yote. Vita ndio inaanza vita vikali vya kiroho na kimwili.

URITHI wa Bib 6

 Story .......... URITHI WA BIBI EP. 6

Author..............Steven Morgan

Contact : ...WhatsApp.. +255 659 115 223


Naam ,kwa mara nyingine tena kwa neema za mungu tumekutana tena katika sehemu ya sita ya story yetu. Tumshukuru Kwanza mungu kwa neema zake pia atusamehe pale tulipokosea na awasamehe pia wale wanao endelea kutukosea maana hawajui wanayo yatenda. Hatupaswi kuhukumu anaye hukumu ni Mungu pekee,sisi yatupasa kujirinda tu dhidi ya wale wabaya.

Nb: Tumtangulize Mungu kwa Kila Jambo maana, Yeye ndie muweza wa yote.


Story yetu tulipoishia ndipo tunapo anzia ili twende sambamba.


TULIPOISHIA....πŸ‘‡


Mama mwenye nyumba alinielekeza mambo mengi haswa majukumu ya kazi. Nikaingia chumbani kwangu nikabadirisha nguo,Kisha nikatoka nikiwa na kanga moja ambayo imenichora umbo langu la mwili haswa makalioni ambapo sio siri ,sijisifii  kweli Mungu amenibariki minyama ya makario. 

Nikakatiza pale sebureni ambapo alikaa baba mwenye. Nyumba na mkewe .  Nilijisahau nilijua kua bafu na choo vipo nje hivyo, nilitaka kutoka nje. " Wewe binti vipi! Mbona hivyo?" " Naenda kuoga mama!"   " Wewe si nilikwambia kua bafu na choo vipo chumba Cha tatu pembeni? Sasa huko nje unaenda wapi!  Au umeshazoea huko kwenu vijijini milimani huko?

" Nilijisahau tu mama samahani!"  " Sawa Chuma tumekuelewa  nenda tu kaoge mama!!"  

Aliongea mzee Foya huku akinitazama kwelikweli. Basi nikageuka na kuelekea huko bafuni . " We baba Maria vipi? Mbona unamtazama Sana yule binti kwa nini?" 

Nilimsikia mama mwenye nyumba akimsema mmewe kua alikua akinishangaa Sana. Nafikiri ni kwa sababu ya ile kanga niliyovaa na umbo langu ,lilimpa shida Sana.

 Basi nikaelekea bafuni ,ile nafungua mlango tu!

Namwona bibi yuko kule bafuni,kiukweli nilishtuka Sana ,ilibaki kidogo tu ,nipige kelele.

" Tulia Chuma, nimekuja tu kuona unapokaa ,ni pazuri Sana, nafikiri tutaonana baadae ,mida ya kazi,kuna kazi ya kufanya leo". "sawa bibi" 

 Bibi alitoweka Kisha nami nilioga na kuondoka chumbani kwangu.

Ile naingia chumbani tu! Nakuta kioo kipo kitandani kwangu. Kioo hiko hakikua kigeni kwangu kwani nilikitambua vizuri tu ,kua ndio kile alichonipa Bibi na nilikiweka kwenye begi langu ,Sasa sijui kilitoka vipi kukaa pale kitandani.!! Nikakisogelea Kisha nikakitazama ,nilichokiona ni tofauti na nilicho kitarajia! Nilijua nitajiona Mimi mwenyewe,lakini, huwezi amini,nilimwona Bibi zubeda wa kule kwetu morogoro, ambae ana undugu na mzee Foya, na mzee Foya ndipo alipofikia  kwa Bibi zubeda ambapo siku moja kabla ya kuja huku dar tulienda na Bibi kumwangia mzee Foya na ndipo nilipo kwama kwenye tumbo la mzee Foya.

Sasa tuachane na hayo,turudi pale ndani chumbani kwangu ,nilizidi kukitazama  kile kioo,nikamwona Bibi zubeda akiniteta na jirani yetu mmoja wa kulekule nyumbani . Huyo jirani alikua anaitwa mama majuto ,alimpelekea umbea Bibi zubeda kua eti Mimi na Bibi yangu ni wachawi Sana na pia ikiwezekana, wamwambie mzee Foya kua Mimi ni mchawi anifukuze. Kama nilivyo eleza hapo  mwanzo kua ,kioo ni msaada mkubwa Sana kwa wachawi,nimeweza kumwona Bibi zubeda kwenye kioo changu Cha kichawi kwa sababu yule Bibi zubeda na mwenzake walikua wakizungumza sehemu ambayo kulikua na kioo kilichokua wazi yani hakikufunikwa. Kwa hiyo kwetu sisi inakua ni Kama CCTV camera.

  

Basi baada ya hapo Sura ya Bibi zubeda na mwenzake zikapotea Kisha ikaja sura ya mkuu wetu wa uchawi, mkuu alinikazia macho Kisha akasema ," Chuma nadhani unajua Cha kufanya" Kisha mkuu akapotea. 

Nikamwita Bibi zubeda kwenye kioo akatokea tena. Nikachukua begi langu Kisha nikatoa mdori wa kike, nikaanza kuukaba kwenye shingo ule mdori huku nikinuiza maneno ya ufundi. Mara nikaanza kumwona Bibi zubeda kwenye Koo akijishika shingo huku akitoa macho ,kuhashiria maumivu makari. Alihangaika mpaka alianguka chini ,huku Mimi nikiwa bado naendelea kumkaba yule mdori ,mwishoni nikamnyonga shingo ya Yule mdori ,na Bibi Zubeda nae alijinyoosha palepale. Yani nimuua kabisa asije akaniharibia kwa bosi wangu Foya.

  Nikachukua kile kioo na kukirudisha kwenye begi, nikikabadili nguo Kisha nikatulia kitandani. Mara nikasikia mama Maria yani mama mwenye nyumba ananiita, " Chuma , Chuma toka uje tule " kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona ..................................

      

        ENDELEA πŸ‘‡

"Chuma,chuma  toka nje uje tile"

Kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona Bibi amekaa pale kwenye Kochi katikati ya mzee foya na mkewe bibi nae aliketi. Nilishtuka sana mpaka mama Maria na mumewe mzee foya au baba Maria walishtuka sana. " Vipi Chuma mbona umeshtuka ghafla kwa hofu ? Vipi! ". Alihoji bosi wangu mama Maria mke was mzee foya.  " Hapana mama niko sawa tu!" Nilijibu kwa mkato Kisha nami nikaketi kwenye Kochi la mtu mmoja lililokua pembeni.


Nikajisevia chakula pale mezani Kisha bibi nae akajisevia chakula chake bila ya kuonekana na mtu. Mimi pekee ndio nilie kua namwona bibi. Wakati wote tunaendelea kula ,bibi aliniongelesha ,na Mimi pia nilimjibu yani tulikua tunaongea kwa sauti bila ya mtu mwingine kujua. Hapa utashangaa kua kwanini wengine hawakujua kua Mimi naongea na mtu mwingine? Kiukweli mchawi huwa aongei taratibu yani hanong'oni ,kwani kama mchawi akijaribu kunong'ona basi Kila mtu anaweza akamsikia. Ndomana Mimi na Bibi tulikua tunaongea kwa sauti ili tusishtukiwe . 

" Vipi Chuma mbona unakula huku unaimba ,utajing'ata shahuri yako!!"

 Aliongea mama Maria. Lakini kiukweli nilikua siimbi wimbo wowote ila ,nilipokua nanyanyua mdomo na kuongea kwa sauti na bibi, kumbe wao walinisikia ila walinielewa tofauti yani wao walinisikia kama vile nilikua naimba kumbe nilikua naongea na bibi ambae wao hawaku muona.

Mimi na bibi tuliendelea kuongea mambo mengi haswa yale mauaji ya Bibi zubeda tuliyo yafanya jioni ile .


Baada ya hapo bibi akachota ubwabwa tonge moja kwenye sahani ya mke wa mzee foya yani mama Maria Kisha akalimeza lile tonge Kisha bibi aka anza kujibinya binya tumbo kama vile linamuuma. Mara ghafla! Mama Maria bosi wangu nae akaanza kujishika tumbo na kugugumia maumivu ya tumbo. Kumbe bibi alipochota lile tonge na kufanya alivyofanya, alimroga yule mama mwenye nyumba, ila huu urogi mdogo tu wa kumshikisha mtu adabu hauna madhara sana zaidi ya kuumwa na tumbo na mwishowe kuharisha.

 Ndugu msomaji bila Shaka kama utakua umewahi kula chakula alafu baada ya muda mfupi tumbo likakuuma sana tena sana mpaka unaacha chakula na kwenda kulala kidogo ili ujinyooshe upate nafuu.

Sasa hari kama hiyo huwa mara nyingi husababishwa na wachawi yani ukiona hivyo ujue, ulipokua unakula ,mchawi alikuja na kukitemea mate chakula chako Kisha akakuroga tumbo.!!!

Hapa naomba niwasaidie kidogo kuepukana na hatari hii. Dawa pekee ya kuepukana na mchezo huu ni, kama wewe ni mcha Mungu,Kabla ya kula kiombee chakula kwanza kwa imani yako Kisha endelea kula ,utakua salama. Lakini pia kwa wale wasiojua hata maana ya kusali na kumwomba Mungu basi, hakikisha unapokula chakula chochote unatumia kijiko cha Chuma na usipende kula chakula ukiwa nje ( hadharani) pendelea Kula  chakula ukiwa ndani na usisahau kutumia kijiko ,utakuwa salama katika janga hili.


"Chuma hebu mwangalie mama amepatwa na nini?" Ilikua ni sauti ya mzee foya. "Sawa baba" nilimjibu kwa mkato Kisha nikaanza kumwangalia mama Maria,muda huo bibi alikua akicheka na kung'ong'a kwa kukenua kenua meno huku akiwa kwenye muonekano wa kutisha kwelikweli.

"Chuma naomba uninyanyue taratibu unipeleke chooni "  mama aliongea Kisha baba nae alinyanyuka tukasaidiana kumnyanyua na kumpeleka chooni. Tukamwacha huko chooni huku sisi tukiwa sebuleni tunamsubiri. Muda huo watoto walisha lala muda Maria na kaka yake Matias. 

"Chuma hebu wachukue hawa watoto kawalaze chumbani kwao."  "Sawa baba" nilimjibu bosi Kisha nikaanza kumnyanyua Maria nikampeleka chumbani kumlaza Kisha nikamrudia Matias lakini wakati namrudia matiasi ,bibi pale alipokaa kwenye kochi bado alikua akiendelea kucheka sana Kisha akanioneshea ishara ya kuniaga Kisha akatoweka. Wakati namnyanyua mtoto Matias,simu ya bosi ikaita ,wakati bosi anaongea na simu Mimi nilisha ondoka kumlaza Matias chumbani. Ile natoka kuja tena sebuleni,namkuta bosi mzee foya analia machozi mwamwamwa.. " bosi vipi tena kulikoni?"  Nilimuuliza ili nijue kinacho mliza ni nini? Japo moyoni nilijua nini kinacho endelea.

Alizidi kulia mpaka alianguaka chini na kugalagala!!!!

Mara ghafla akaja mkeo mama Maria kutoka kule chooni alipokua baada ya kusikia sauti ya mmewe akiria. Lakini baada ya kufika yeye, mmewe alinyamaza na akawa anamshangaa mkewe. Mimi na mama Maria pia tukawa tunamshangaa baba Maria kwa kua alikua akiria sana alafu akanyamaza ghafla kulikoni!!!

" Baba Maria mbona sikuelewi? Unachoriria ni nini? Na kilicho kufanya unyamaze ni nini?"


"Mama Maria ! Kwanza Kabla ya kukuambia ninacho lilia ! Naomba kwanza nikuambie kilichonifanya ninyamaze ghafla!!"

 "Sawa baba Maria nakusikiriza" alijibu mama Maria.

" Mke wangu, Mimi na chuma tulikupeleka chooni ukiwa hata kutembea huwezi! Sasa imekuaje umekua na nguvu za kutembea kwa haraka ukaja hapa sebuleni mwenyewe?"

" Baba Maria,baada ya kula kile chakula,tumbo lilianza kuniuma sana Kisha nikahisi kama vile nataka kwenda haja kubwa. Lakini ,mliponinyanyua na kunipeleka na kuniacha kule chooni,hakuna nilicho kinya zaidi ya kutoa upepo muda wote Kisha tumbo limetulia!! Haya Sasa nambie wewe unachoriria ni nini?

Mzee foya kabla hajaanza kuzungumza ,akaanza kulia tena huku akimtaja bibi zubeda wa morogoro.

"Jamani bibi zubeda wa morogoro,amefanya nini?" Aliuliza mama.  "Sijui" nilijibu Mimi kwa ufupi.  "Amefariki masikini wa Mungu!!!" Baba alionge kwa uchungu mkubwa. " Amefariki?" Alijibu mama kwa kushangaaa sana. " Ndio amefariki jioni hii hii ya leo,amekutwa ndani kwake ameanguka chini na kufariki " alizidi kuongea mzee foya.  "Alikua anaumwa?" Aliuliza mama. " Hapana kifo chake Wala hakijahusika na kuumwa itakua ni mambo ya ushirikina,na nikomgundua mtu alie husika na kifo hochi,basi na yeye nitamfanya mfu."" Aliongea mzee foya kwa uchungu


Mzee foya baada ya kuria kwa muda mrefu kutokana na taarifa ya kifo cha bibi zubeda wa morogoro,alinyamaza Kisha akamwambi mkewe aketi chini wazungumze kua itakuaje?

" Mke wangu kesho inabidi niwatangulize  huko morogoro kwenye msiba  mapema,lakini Mimi nitakuja jioni sababu kuna sehemu nitapitia  kutafuta ukweli wa kifo cha ndugu yangu bibi zubeda. Na nikimjua hadui alie husika ,hama zake ,hama zangu."  Mzee foya aliongea kwa hasira sana,huku Mimi na mama Maria tukiwa tumetulia kama tumezubaa vile. Basi kwa kua muda ulikua umeshaenda,Kila mtu aliingia chumbani kulala.............         ............    .................. .....

                         ITAENDELEA.


Je,mzee foya atagundua chanzo cha kifo cha ndugu yake Bibi zubeda? Je, na kama atamgundua hadui alie husika  ,nini atakacho kifanya? Hayo na mengine mengi usikose kufuatilia sehemu ya saba ya URITHI WA BIBI. 

Naamini kwa uweza wa Mungu tutakutana tena kipindi kijacho kunako majaariwa. Maarifana uhondo ndio kwanza unaanza ,Wala hujachelewa,mambo ni mengi sana ,muda  ni mchache.

Nb:Mtangulize Mungu kwanza kwa Kila Jambo.πŸ™

URITHI wa Bibi 5

 Story ...... URITHI WA BIBI EP. 5

Author..............Steven Morgan

πŸ“ž..................... +255 659 115 223


🌷 TULIPOISHIA 🌷


Basi nikiwa bado nipo chumbani na Bibi huku nikikiweka kioo alicho nipa kwenye begi langu la kusafiria. Baada ya hapo  kwakua ilikua tayari ni usiku Sana ,tukatoka nje kichawi,yani tulitoka bila ya kufungua milango,moja kwa moja tulienda kwa Bibi zubeda ambae yule mgeni Foya ndipo alipo fikia,ilikua ni usiku Sana ,wote ndani walishalala fofofo, Mimi na Bibi tuliruka na kutua kwenye paa la nyumba la Bibi zubeda.Tulipotua juu ya bati,hapakua na kelele wala kishindo zaidi Kama aliekua ndani Kama hajalala basi anaweza akasikia Kama mchanga au vimawe mawe vinamiminika kwenye bati!! 

Ndugu msomaji ukisikia Hari hiyo,ujue wanga wamesha tua na Kama hujalala basi utalala kwa lazima .unachotakiwa kufanya baada ya kuona Hari hiyo ni kumwomba Mungu Sana akunusuru na ibirisi huyo.

Basi tukatua kwenye lile bati la bibi zubeda ,japo bati zake zili oza lakini hatuwezi kuanguka kwani tunakuaga wepesi sana . Tulimwaga madawa yetu ili asie lala kwa muda huo ,alale kwa lazima ili sisi tuendelee na kazi yetu.

Tulitazama kwa kupitia jicho la tatu la kichawi tulimwona yule bosi Foya anaye taka kesho juma tatu twende wote dares salaam amelala fofofo huku simu yake ya tachi ikiwa chini. Tulirukaruka huko juu ya bati huku tukiimba nyimbo za kichawi kwa sauti. Hata Kama hujalala huwezi kutusikia. zaidi, utahisi wimbo flani unao ufahamu ume play katika kichwa chako ,ukiona hivyo ujue wazee wa kiza wapo nje au ndani wanacheza na kuimba.   Basi tukacheza Sana Mimi na Bibi baadae  tukaingia ndani chumbani kwa yule mgeni Foya . Taa ilikua inawaka tukaizima  Kisha tukaanza kumsotea kwa makalio ,muda mwingine tulimjambia mdomoni akawa anashtuka na kukohoa  sana. Bibi aliniambia kua nimkalie tumboni kwa makalio yangu Kisha nimsotee sotee !! Nami nikafanya hivyo tena kwa haraka . Lakini ghafla yule mzee Foya alishtuka usingizini kwa haraka na akanikamata nikiwa palepale juu ya tumbo lake!!! Huwezi amini Bibi aliondoka na kuniacha nimekwama juu ya tumbo la mzee Foya ambae ni bosi wangu mtarajiwa  huku nikiwa uchi wa mnyama na makalio yangu makubwa yaliyojaziana minyama yakiwa juu ya tumbo la mzee Foya.

******* ***** ENDELEA πŸ‘‡ ************

Nikiwa  bado nipo juu ya tumbo la mzee Foya ,sikua na ujanja kwani mzee Foya alinikamata kisawa sawa!! Nikajua sasa leo ndio mwisho wangu wa maisha ,nikahisi huwenda mzee Foya akanidhuru .  " Ahaaa! Kumbe ulijua Mimi ni mtu wa mchezo mchezo! Sasa Leo nakuua yani nakuchinja kabisa!!". Aliongea mzee Foya kwa kujiamini zaidi  huku Mimi nikitetemeka kwa hofu nisijue Cha kufanya. Nilihofia zaidi kwamba je,nitafanyaje endapo mzee Foya atanibahini? Maana mpaka muda huo bado  alikua hajanitambua kua ndio Mimi binti Chuma anaye taka kunichukua nikamfanyie kazi. Kulikua na giza nene pale chumbani sababu chemli iliyokua inawaka ,tuliizima mwanzoni kipindi tunaingia na Bibi . " Alafu unaonekana wewe ni binti mdogo kabisa kwanini Sasa  unakua shetani namna hii? Ngoja kwanza nifanye mpango wa kuwasha taa ili nikuone vizuri!"   Duh! Nilishtuka Sana kwani nilijua muda wa kumbuka umekaribia. Lakini kabla mzee Foya hajafanya chochote ,ghafla tu akatokea mkuu wetu, yule aliyetuhapisha uchawi. Akampiga kofi mzee foya la paji la uso,Foya akazimia Kisha akanichukua na kupotea ghafla,mara tu nikajikuta nipo juu ya kibeku yani ndege ya kichawi aina ya Air fagio plane( Broom air plane ) huku mkuu akiwa ndio dereva na Mimi nilikaa nyuma nikiwa kwenye umbo la nyau. Usafiri huu huwa ni wa haraka Sana Kama nilivyo elekeza hapo mwanzo. Hivyo mkuu alinifikisha mpaka mlangoni nyumbani kwa Bibi.Bibi alitoka nje haraka Wakati sisi tukiwa tunakaribia kutua.

" Bibi Chuma mnatakiwa kuwa makini Sana ,hata hivyo umefanya la maana Sana kunipa taarifa mapema. Raha sivyo leo Chuma angeumbuka." 

Hayo yalikua ni maneno ya mkuu akimwambia Bibi, kumbe Bibi baada ya kukimbia na kuniacha alitoa taarifa kwa mkuu ndio akaja kunipa msaada. 

" Na wewe chuma inabidi utulize akili ,ujitambue ! Wewe una nguvu Sana ila hujui kuzitumia,uwezo ulio nao wewe, chocho te waweza fanya , Chuma bila Shaka kesho ndio unakwenda kufanya kazi kwa huyo mzee Foya huko dar es salaam. Hakikisha unakua makini Sana usije ukakosea chochote. Yule mzee mpaka asubuhi akiamka hakuna chochote atakacho kikumbuka zaidi tu atakufuata ili muondoke,Mimi nakutakia safari njema pia ukatanye kazi yetu kwa weredi na umakini zaidi. Kwaherini!"

Mkuu baada ya kuongea maneno hayo,alituaga na akaondoka kwa usafiri wake wa haraka. Tukabakia Mimi na Bibi

Kwakua ilikua ni USIKU Sana, hatukuzungumza mengi ,tukaenda kulala ili kesho niwahi kuamka kwaajiri ya safari.

Kama wasemavyo waswahiri kua ,awike asiwike ni lazima kuche, Ndivyo ilivyokua , asubuhi ilifika ,nikajiandaa vya kutosha ,ninaposema nimejiandaa vya kutosha namaanisha nilifungasha Kila kitu kinacho nihusu haswa dhana za kichawi. Kumbuka hiyo ilikua ni siku ya juma tatu na ilipofika saa kumi na mbili asubuhi ,mzee Foya alikuja alinikuta nje na Bibi tukimngoja yeye tu! 

" Karibu Sana mzee foya ,mfanyakazi wako ndo huyu yuko tayari kwa Safari." Bibi alimwambia mzee Foya kwa msisitizo. " Asante Sana Bibi mbokeleni, Chuma..tusipoteze Sana muda wacha tuwahi gari la kwanza" 

Foya akatoa shilingi elfu 30 akampa Bibi Kisha sisi tukaondoka. Bibi alinipungia mkono Kila nilipogeuka kumtazama.

Tulifika msamvu mapema tukapata basi ,safari ilisonga mida ya saa kumi tukafika kwa mzee Foya maeneo ya Tabata shuleni. Tulimkuta mkeo na watoto wawili wa umri wa miaka 6 na miaka minne. " Karibuni wageni , karibuni sana,lete huo mzigo wako binti nikupokee!" Nilimpa begi langu mama mwenye nyumba ambalo lilikua zito Sana . " Heee! Mbona begi lako zito Sana,umeweka mawe nini?" Aliongea mama mwenye nyumba. " Kaweke huo mzigo bana mbona unataka kuchunguza mzigo usio kuhusu?" Alidakia baba mwenye nyumba Foya. Basi yule mama Akaniambia nimfuate,akaenda kunionesha ,chumba changu Cha kulala nikaingia nikaweka mzigo wangu. Kisha tukatoka akanitembeza nyumba nzima ,nikaona mazingira yote.akanielekeza na majukumu yangu ya kazi . " Hivi dada unaitwa nani?" " Naitwa Chuma."   (  "Aahaa,sasa dada Chuma,Mimi na baba yako wote ni wafanya kazi ,na asubuhi wote tunaondoka ,Mimi huwa narudi mida ya saa kumi,baba yako huwa anarudi saa kumi na moja na kuelekea. Watoto hawa wanasoma chekechea,huwa kuna gari mida ya saa moja linawapitiaga kwahiyo uhakikishe unawapikia asubuhi na mapema wale,waoge kisha uwaandae kwaajiri ya shule. Ukisiki honi ya gari unawatoa nje wapande gari la shule ,sawa Dada Chuma?"  "Sawa mama nimekuelewa."   "Nashukuru Kama umenielewa lakini pia ,unatakiwa inapofika saa Saba mchana una andaa chakula . Mambo mengine ni kujitahidi usafi wa mwili na mazingira ,sawa Chuma?" " Sawa mama nimekuelewa". Basi Kama umenielewa unaweza kwenda kuoga bafu ni  lile pale chumba Cha tatu pembeni na kinacho fuata ni choo."


Mama mwenye nyumba alinielekeza mambo mengi haswa majukumu ya kazi. Nikaingia chumbani kwangu nikabadirisha nguo,Kisha nikatoka nikiwa na kanga moja ambayo imenichora umbo langu la mwili haswa makalioni ambapo sio siri ,sijisifii  kweli Mungu amenibariki minyama ya makario. 

Nikakatiza pale sebureni ambapo alikaa baba mwenye. Nyumba na mkewe .  Nilijisahau nilijua kua bafu na choo vipo nje hivyo, nilitaka kutoka nje. " Wewe binti vipi! Mbona hivyo?" " Naenda kuoga mama!"   " Wewe si nilikwambia kua bafu na choo vipo chumba Cha tatu pembeni? Sasa huko nje unaenda wapi!  Au umeshazoea huko kwenu vijijini milimani huko?

" Nilijisahau tu mama samahani!"  " Sawa Chuma tumekuelewa  nenda tu kaoge mama!!"  

Aliongea mzee Foya huku akinitazama kwelikweli. Basi nikageuka na kuelekea huko bafuni . " We baba Maria vipi? Mbona unamtazama Sana yule binti kwa nini?" 

Nilimsikia mama mwenye nyumba akimsema mmewe kua alikua akinishangaa Sana. Nafikiri ni kwa sababu ya ile kanga niliyovaa na umbo langu ,lilimpa shida Sana.

 Basi nikaelekea bafuni ,ile nafungua mlango tu!

Namwona bibi yuko kule bafuni,kiukweli nilishtuka Sana ,ilibaki kidogo tu ,nipige kelele.

" Tulia Chuma, nimekuja tu kuona unapokaa ,ni pazuri Sana, nafikiri tutaonana baadae ,mida ya kazi,kuna kazi ya kufanya leo". "sawa bibi" 

 Bibi alitoweka Kisha nami nilioga na kuondoka chumbani kwangu.

Ile naingia chumbani tu! Nakuta kioo kipo kitandani kwangu. Kioo hiko hakikua kigeni kwangu kwani nilikitambua vizuri tu ,kua ndio kile alichonipa Bibi na nilikiweka kwenye begi langu ,Sasa sijui kilitoka vipi kukaa pale kitandani.!! Nikakisogelea Kisha nikakitazama ,nilichokiona ni tofauti na nilicho kitarajia! Nilijua nitajiona Mimi mwenyewe,lakini, huwezi amini,nilimwona Bibi zubeda wa kule kwetu morogoro, ambae ana undugu na mzee Foya, na mzee Foya ndipo alipofikia  kwa Bibi zubeda ambapo siku moja kabla ya kuja huku dar tulienda na Bibi kumwangia mzee Foya na ndipo nilipo kwama kwenye tumbo la mzee Foya.

Sasa tuachane na hayo,turudi pale ndani chumbani kwangu ,nilizidi kukitazama  kile kioo,nikamwona Bibi zubeda akiniteta na jirani yetu mmoja wa kulekule nyumbani . Huyo jirani alikua anaitwa mama majuto ,alimpelekea umbea Bibi zubeda kua eti Mimi na Bibi yangu ni wachawi Sana na pia ikiwezekana, wamwambie mzee Foya kua Mimi ni mchawi anifukuze. Kama nilivyo eleza hapo  mwanzo kua ,kioo ni msaada mkubwa Sana kwa wachawi,nimeweza kumwona Bibi zubeda kwenye kioo changu Cha kichawi kwa sababu yule Bibi zubeda na mwenzake walikua wakizungumza sehemu ambayo kulikua na kioo kilichokua wazi yani hakikufunikwa. Kwa hiyo kwetu sisi inakua ni Kama CCTV camera.

  

Basi baada ya hapo Sura ya Bibi zubeda na mwenzake zikapotea Kisha ikaja sura ya mkuu wetu wa uchawi, mkuu alinikazia macho Kisha akasema ," Chuma nadhani unajua Cha kufanya" Kisha mkuu akapotea. 

Nikamwita Bibi zubeda kwenye kioo akatokea tena. Nikachukua begi langu Kisha nikatoa mdori wa kike, nikaanza kuukaba kwenye shingo ule mdori huku nikinuiza maneno ya ufundi. Mara nikaanza kumwona Bibi zubeda kwenye Koo akijishika shingo huku akitoa macho ,kuhashiria maumivu makari. Alihangaika mpaka alianguka chini ,huku Mimi nikiwa bado naendelea kumkaba yule mdori ,mwishoni nikamnyonga shingo ya Yule mdori ,na Bibi Zubeda nae alijinyoosha palepale. Yani nimuua kabisa asije akaniharibia kwa bosi wangu Foya.

  Nikachukua kile kioo na kukirudisha kwenye begi, nikikabadili nguo Kisha nikatulia kitandani. Mara nikasikia mama Maria yani mama mwenye nyumba ananiita, " Chuma , Chuma toka uje tule " kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona ..................................

      

        ITAENDELEA.................

Je, Chuma ameona nini pale sebuleni? Usikose sehemu ya 6 . Uhondo ndio kwanza unaanza ukiwa na maarifa kibao. Mambo mengi muda mchache.Mungu akijaaria tutakutana tena sehemu ijayo.Asante.

URITHI wa Bibi 4

 Story : URITHI WA BIBI . EP.4


Author........... Steven Morgan


πŸ“ž : .............+255 659 115 223


Email : ................. stevennemes2k@gmail.com


Karibu tena ndugu msomaji katika mwendelezo wa story yetu. Tulipoishia ndipo tunapo anzia .


ILIPOISHIA.

Binti chuma na wenzake  wakiwa msituni waki hapishwa na mkuu wa wachawi.


Basi,mvua ikaendelea kunyesha na jua likaendelea kuwaka ,mara ghafla mvua ikakata na likabakia jua Kama mwanzo. Mkuu wa wachawi akatupongeza na kusema kua Sasa tunatakiwa  kuusumbua ulimwengu. Natumaini mtakua mawakala wazuri Sana wa shetani katika kuleta ubovu ulio kidhiri katika Dunia . Mbarikiwe Sana na lusifa ,na mkafanikiwe katika kutenda dhambi zenu zilizobarikiwa na shetani". 

 Mkuu alipomaliza kusema hayo Mimi nikajihisi mwenye nguvu Sana na nikajikuta naweza kufikiria na kufanya mambo makubwa bila ya kufundishwa. Macho yaliniwiva kama nyanya ya utunguja. Mkuu alinitazama Kisha akasema " Chuma ,wewe unaonekana kua na nguvu nyingi sana ,kafanye kazi ,jamii ikutambue na kukuogopa ,hakuna kiumbe atakae weza kukudondosha , ulimwengu ni wako chuma , chochote unaweza kufanya kuanzia Sasa,umesha pewa nguvu ya mamlaka!"  Hayo yalikua maneno ya mkuu akinisifu,baada ya hapo tukanyanyuka na kurudi nyumbani baada ya kuruhusiwa na mkuu.


                      ENDELEA.

Kwakua ilishafika jioni Sana ya saa kumi na mbili ,Mimi na bibi tulishilikiana kupika  chakula Cha jioni kwa haraka Kisha ilipofika saa mbili kamili usiku ,tukaandaa chakula na kuanza kula huku maongezi ya hapa na pale yakiendelea.

Siku ikaisha hatimaye asubuhi ikafikia ,Kama kawaida nikaamka na kufagia uwanja  ,nikaanda chai na maji ya Moto ya kuoga.  Bibi alipoamka alienda kuoga baada ya Mimi kumaliza. Baada ya hapo tukatandika mkeka wetu nje na kuketi kwa ajili ya kunywa chai. 

"Chuma mjukuu wangu,kwa Sasa umeshakua kamili tena una nguvu nyingi zaidi yangu. Sasa ni Wakati wako wa kutamba unavyo taka"

Natamba kivipi bibi?"  "Kwa nguvu ulizonazo unaweza ukafanya chochote na kupata chochote unachokitaka,kwa mfano Kama kuna mtu unamchukia unataka kumfanya vibaya awe kichaa au awe na mikosi au maradhi, unaweza fanya."  "Sawa Bibi hayo uyasemayo Kama yanawezekana nitayatenda maana kuna watu nawachukia Sana."  Hayo yalikua ni maongezi ya hapa na pale Kati ya Chuma na Bibi yake,  Chuma anaendelea kueleza ...tukiwa bado tupo pale nje tukinywa chai mara akaja mtu mmoja wa kiume ni mbaba kwakua alikua  ni mtu mzima . " Hodi hodi wenyewe hapa!!"  " Karibu " tukamjibu yule mbaba kwa pamoja. " Bila Shaka hapa ndio kwa bibi Mbokeleni au kwa bibi chuma?" Aliuliza yule mgeni tusie mfahamu. " Ndio bila Shaka umefika Mimi ndio Bibi Mbokeleni na huyu ndio mjukuu wangu Chuma" Bibi alimjibu yule mgeni. " Nashukuru kuwafahamu! Bila Shaka hamnifahamu ,Mimi naitwa Foya ni mwenyeji wa moshi lakini kwa Sasa makazi yangu naishi Dares salaam.Kuja hapa nimeelekezwa na ndugu yangu mmoja ambaye ni mwenyeji wa hapa Ndolelo anaitwa Bibi zubeda anaishi hapo ng'ambo ya pili" " aaah! Bibi zubeda namfahamu  vizuri,Sasa nambie shida yako ni nini?" Bibi alimjibu yule mgeni. " Shida yangu nilikua nahitaji binti wa kunifanyia kazi za ndani,nipo Mimi,mke wangu na wanangu wawili wadogo wa kike na wa kiume . Sasa nimeambiwa kua kuna binti anaitwa chuma unae hapa ,ndo maana nimekuja kukuomba Kama itawezekana niende nae dar es salaam akanifanyie kazi." Yule baba mgeni alijieleza Wakati huo wote Mimi nilikua nipo kimya nikisikilizia kinachoendelea Kati ya Bibi na yule mgeni. " Sasa wewe umetoka huko kote umepaona hapa ndio kwenye mfanyakazi?" " Nimekuja hapa kwakua nime elekezwa raha sivyo, nisinge fika,nisamehe lakini Kama nimefanya kosa kuja hapa"  " ha ha ha haaa! wewe huna kosa ila kosa analo aliekuelekeza kuja hapa!, Sasa je, utaweza kwenda kuishi na mjukuu wangu kweli huko dar es salaam?, " Bila Shaka Bibi ,Kama Chuma mwenyewe atakubari, basi hakuna kitakacho shindikana ,ataishi vizuri Sana atakua Kama yupo nyumbani"  " sawa ,Mimi Kama bibi na Kama ndio mzazi wa Chuma,sina neno tena labda tumsikia mwenyewe Chuma anasemaje kuhusu hilo? Maana nae pia ana maamuzi yakepia"  Bibi alimalizana na yule mgeni kisha bibi alinigeukia na kuniuliza ," Chuma nadhani umesikia mazungumzo yote hapa ,Sasa je,upo tayari kwenda dar es salaam kufanya kazi?  " Bibi Mimi bana  sitaki niende mbali nikuache wewe peke yako,siwezi kuishi mbali nawe"  " Chuma kumbuka wewe umeshajitambua na unaendelea kua mtu mzima ,kumbuka sasa unatakiwa kujitafutia maisha yako mwenyewe ,naamini ukifanikiwa unanikumbuka na Mimi Bibi yako kwa kuninunulia upande wa kitenge na kaniki na sukari utaniletea au we unasemaje?" Bibi alinig'ang'ania Sana Mimi kukubari kwenda kufanya kazi dar es salaam,sijui kwa nini! Lakini nahisi alikua na maana yake. " Sawa bibi kwakua wewe umekubari Mimi niende ,siwezi tena kupinga,niko tayari ila nataka nijui kwanza nitalipwa shilingi ngapi?

"Nashukuru Sana Bibi, pia nakushukuru Sana Chuma. Kwa kukubali kwendakufanya kazi kwangu, mshahara nitakulipa shilingi elfu kumi, na ukifanya kazi vizuri nitakuongeza!!"  Aliongea yule mgeni alie jitambulisha kwa jina la Foya ndugu na Bibi Zubeda. Basi kwa kua ilikua  asubuhi ya alhamisi ,bibi alimwambia  yule mzee Foya kua aje juma tatu kunichukua . Mzee Foya alifurahi Sana bila kujua kua anamkaribisha shetani alietoka depo. Alituaga Kisha akasema kua atakuja juma tatu asubuhi kunichukua na tutaianza safari asubuhi hiyo hiyo.

Bibi alifurahi Sana na akaniambia kua " Sasa Chuma huko unakokwenda ndio pa kujikomaza mjukuu wangu sawa?"  " Sawa bibi kwa Sasa huna haja ya kunielekeza najua nini cha kufanya. Watamjua chuma kua ni mtu wa aina gani!!


Story ................ URITHI WA BIBI EP. 4.B

Author..............Steven Morgan

πŸ“ž..................... +255 659 115 223


Kwa mara nyingine tena bado tupo sehemu ya 4 ya story yetu ambapo tunaingia katika kipengele B ya sehemu ya 4. Kabla hatuja endelea katika kipengele B,ngoja tukumbushane kidogo yaliyopita katika kipengele Cha 4.A.


ILIPOISHIA,

Tumeona kua Bibi Mbokeleni au Bibi chuma amepata ugeni wa baba mmoja asubuhi na mapema ambaye alijitambulisha kwa jina la Foya . Mzee Foya alikua anahitaji mfanyakazi wa ndani ili aondoke nae Dares salaam ,ambako ndiko anako ishi yeye na  familia yake ,akiwemo mkewe na watoto wawili wadogo.Binti chuma ndio mlengwa anae hitajika kwenda huko dares salaam kufanya kazi. Kumbuka binti chuma siku si nyingi ametoka kufuzu depo la kichawi na kuhapishwa. Bibi yake amemruhusu chuma aende akafanye kazi. Mzee Foya ameambiwa aje juma tatu kumchukua binti chuma ili aondoke nae dar es salaam. 

 

ENDELEA.

Bibi alifurahi Sana Mimi kupata kazi ,japo Mimi sikupenda kua mbali na bibi yangu maana yeye ni Kama mzazi wangu alie bakia katika Dunia hii.

Lakini kwakua bibi ameridhia ,basi Mimi pia siwezi kumpinga kwani bibi alitaka na Mimi pia nijitafutie maisha yangu ili baadae nikifanikiwa ,nimsaidie na yeye.

 Kama wasemavyo waswahili kua usiku wa deni haukawii kucha,basi siku zilikwenda Sana na juma pili ikafika ,ambapo nilijiandaa vya kutosha,nilifungasha kila kilicho changu kwaajili ya safari ya dar es salaam. Usiku ukaingia,Bibi aliniita katika chumba chake Kisha akanipa kioo Cha pembe nne ,akaniambia nikitunze maisha yangu yote,na yeyote ninaye mtaka kumwona nimwite kwa jina lake nitamwona pale kwent kioo.

Ndugu msomaji,kioo kina maajabu mengi usiyo yajua ambayo unaweza ukafanya hata wewe ambae sio mchawi!! Nitakwambia hajabu moja wapo la kioo unacho jitazamiaga nyumbani kwako. Baadhi ya watu ukiingia vyumbani mwao,utakuta vioo vya kujitazamia ,vimefunikwa kwa nguo au boksi au karatasi kubwa na vitafunuliwa Wakati mtu anapotaka kujitazamia tu!!

Huwa wanavifunika kwa sababu,vioo hutumika Kama CCTV Camera ya wachawi,na huona na kusikia chochote mnacho ongea au kuteta mkiwa ndani huku vioo vya kujitazamia vikiwa wazi. Ndugu msomaji unashauriwa kufunika kioo chako Cha kujitazama na ukifunue pale unapotaka kukitumia tu!!, Kwani unapo viacha wazi muda wote ,wachawi watajua kila kitu kinacho endelea ndani mwako.

Hajabu lingine lakioo,nikwamba kwa kupitia kioo unaweza kumwita jini yeyote akaja na unaweza kuzungumza nae kwa kupitia kioo chako Cha kujitazama. Unacho takiwa kufanya hapa ,ni kuchukua kioo chako Cha ukubwa wa kutosha wa pembe nne Kisha jifungie ndani mwako,hakikisha hakuna kelele Kisha chukua kioo chako kiweke mbele ,mezani ,ukutani au Kama kipo kwenye dressing table yako ni vizuri zidi.simama mbele ya kioo chako Kisha kitazame kioo chako bila kubwenza kwa dakika kadhaa huku katika akili yako fikiria kua kuna jini au kiumbe Cha hajabu utamwona!! Kisha  taratibu utaanza kuona sura yako inabadirika na kua sura mbaya ya kutisha ,ukiona hari hiyo inajitokeza ,ujue jini ameshafika ,unachotakiwa kufanya Sasa ni kumwomba unachokitaka akutendee. Angalizo : usije ukafanya zoezi hili Kama wew ni mwoga ndugu msomaji,kwani inatisha mno. Na usije ukafanya zoezi hili usiku,ni hatari Sana.


Basi nikiwa bado nipo chumbani na Bibi huku nikikiweka kioo alicho nipa kwenye begi langu la kusafiria. Baada ya happy kwakua ilikua tayari ni usiku Sana ,tukatoka nje kichawi,yani tulitoka bila ya kufungua milango,moja kwa moja tulienda kwa Bibi zubeda ambae yule mgeni Foya ndipo alipo fikia,ilikua ni usiku Sana ,wote ndani walishalala fofofo, Mimi na Bibi tuliruka na kutua kwenye paa la nyumba la Bibi zubeda.Tulipotua juu ya bati,hapakua na kelele wala kishindo zaidi Kama aliekua ndani Kama hajalala basi anaweza akasikia Kama mchanga au vimawe mawe vinamiminika kwenye bati!! 

Ndugu msomaji ukisikia Hari hiyo,ujue wanga wamesha tua na Kama hujalala basi utalala kwa lazima .unachotakiwa kufanya baada ya kuona Hari hiyo ni kumwomba Mungu Sana akunusuru na ibirisi huyo.

Basi tukatua kwenye lile bati la bibi zubeda ,japo bati zake zili oza lakini hatuwezi kuanguka kwani tunakuaga wepesi sana . Tulimwaga madawa yetu ili asie lala kwa muda huo ,alale kwa lazima ili sisi tuendelee na kazi yetu.

Tulitazama kwa kupitia jicho la tatu la kichawi tulimwona yule bosi Foya anaye taka kesho juma tatu twende wote dares salaam amelala fofofo huku simu yake ya tachi ikiwa chini. Tulirukaruka huko juu ya bati huku tukiimba nyimbo za kichawi kwa sauti. Hata Kama hujalala huwezi kutusikia. zaidi, utahisi wimbo flani unao ufahamu ume play katika kichwa chako ,ukiona hivyo ujue wazee wa kiza wapo nje au ndani wanacheza na kuimba.   Basi tukacheza Sana Mimi na Bibi baadae  tukaingia ndani chumbani kwa yule mgeni Foya . Taa ilikua inawaka tukaizima  Kisha tukaanza kumsotea kwa makalio ,muda mwingine tulimjambia mdomoni akawa anashtuka na kukohoa  sana. Bibi aliniambia kua nimkalie tumboni kwa makalio yangu Kisha nimsotee sotee !! Nami nikafanya hivyo tena kwa haraka . Lakini ghafla yule mzee Foya alishtuka usingizini kwa haraka na akanikamata nikiwa palepale juu ya tumbo lake!!! Huwezi amini Bibi aliondoka na kuniacha nimekwama juu ya tumbo la mzee Foya ambae ni bosi wangu mtarajiwa  huku nikiwa uchi wa mnyama na makalio yangu makubwa yaliyojaziana minyama yakiwa juu ya tumbo la mzee Foya.

******* ***** ITAENDELEA ************

 JE,nini kitafuatia?

Mzee Foya atamtambua binti Chuma?

Je,safari ya dar es salaam ipo?

 Hayo na mengine mengi utayajua katika sehemu ya EP. 5 ya URITHI WA BIBI


USISAHAU KU LIKE , COMMEnt


URITHI wa Bibi 3

 Story :.................... URITHI WA BIBI . EP.3


Author................... Steven Morgan


πŸ“ž : .......................+255 659 115 223


Email : ................. stevennemes2k@gmail.com


Karibu tena ndugu msomaji katika mwendelezo wa story yetu.Kabla ya kusonga mbele, ngoja tukumbushane kidogo..

TULIPOISHIA:

Ndugu msomaji, sehemu iliyopita tumeona kua chuma mashaka na bibi yake mbokeleni,wakiwa kwenye harakati za kishirikina za kuruka kwa usafiri wa  air kibeku aina ya " ungo natural air plane" ambayo safari yao iliwapeleka mpaka Nairobi Kenya. Ambako huko ,mambo yaliwaendea hovyo,walipokatiza kwenye anga la kanisa moja la Kenya Assemblies of God . Ambapo wali anguka na ndege yao kwenye uwanja wa kanisa nyakati hizo za usiku,ila bibi alifanikiwa kukimbia na kumwacha mjukuu wake Chuma akiwa amekwama.Ambapo baadae alikuja kuokolewa na mmama mmoja mchawi wa hukohuko Kenya na kutoweka nae.Chuma akiwa kwenye mikono ya yule mama mwenyeji wa kenya mambo ya kichawi yaliendelea Kama kawaida.Kwani tumeona kua chuma kwakua alikua na njaa aliweza kula supu ya kichawi yani supu ya nyama ya mtu ikiwa na mchuzi mwingi wa damu.Majanga kwa chuma yaliendelea ambapo walipata misukosuko pia walipokwenda kuwachawia watu mtaani. Mwishoni tuliona Chuma akinusurika kubakwa akiwa amekwama kwenye nyumba ya kijana mmoja huku yule mama akiwa amekimbia na kumwacha na alipojipanga tena ,alirudi kumwokoa tena Chuma .Ambapo baaadae kwa kutumia usafiri wa ndege ya kichawi aina ya "fagio natural Air Plane" , Chuma akiwa na yule mama bila kupoteza muda walisafiri kwa haraka na kuwasiri nchini Tanzania nyumbani kwa kina chuma.Ambapo walimkuta bibi yake na chuma akiwasubiri ,kisha baada ya chuma kupokelewa na bibi yake,yule mmama mchawi wa Kenya akaondoka zake bila kusubiri. 


ENDELEA..

 Bibi alinipokea usiku ule ,kwakua nilichoka Sana sikuweza kuongea mengi bali nili muomba bibi niende nikalale afu mambo mengine tutazungumza asubuhi. Bibi aliniruhusu Kisha nikaenda chumbani kwangu kulala . Nilipokuja kushtuka ilikua tayari kumesha kucha,kwani nilisikia ndege wakilia huku nje bibi aliendelea kufagia uwanja. Niliamka na kuchukua ndoo yenye maji ya kuoga ya baridi ,nikaenda kuyaoga ili niondoe uchovu. Kiukweli nilichoka Sana tena Sana!!  Nilipomaliza kuoga , tayari bibi alisha ivisha chai na futari yenye mchanganyiko wa magimbi,miogo ,ndizi na vigonzo. Futari iliungwa kwa nazi . Bibi alitandika jamvi dogo na aliandaa chai Kisha wote tukaketi jamvini na kunywa chai kwa pamoja. "Pole Sana mjukuu wangu ndio ukubwa huo".  " Asante bibi ila namshukuru Sana mungu ameniepusha na mengi".    " Mh! Mungu tena katokea wapi? Wewe umshukuru tu yule mama mchawi wa Kenya ,ndie alie kusaidia sana."   "Nikweli bibi napaswa pia kumshukuru yule mama mungu ambariki Sana."  

"Mungu ambariki kwa kazi gani nzuri aliyoifanya? Hebu wacha kumtaja taja huyo mungu wako kwenye haya mambo!"


"Sawa bibi ila hii kazi Mimi siitaki tena !"


"Wee! Tena funga huo mdomo wako,hivyo unavyosema wiki hii tu! Natakiwa nikukabidhi mikoba rasmi ,na wala huwezi kupinga wamesha kuchagua wakubwa, hahaha haahaa haahaa!" 


Kiukweli mtoto wa nyoka ni nyoka , sikuweza kulipinga hilo . Sijui bibi aliniroga!! Maana siku zilikwenda hatimaye wiki ikafikia ,alilolisema bibi ndilo lililokua . Na kiukweli sikuweza kupinga . Nakumbuka ilikua siku ya juma nne nyakati za usiku sana,waswahili wanaita mida ya wanga! Tukiwa nyumbani ,bibi alinipaka dawa na kunichanja chale nyingi za kichawi mwilini na kunielekeza baadhi ya mambo makubwa. Kisha baada ya hapo ,tukaenda kwenye sherehe ya kukaribishwa mwanachama mpya wa kichawi. Tukaenda kwa kuruka kwa kupiga guu la kushoto chini na kupotea kwa ghafla Kisha tukaenda kutokea kwenye uwanja wa mpira wa miguu,ukiwa umefurika watu kibao ,wakubwa kwa watoto ,vijana kwa wazee!! Uwanja huo pembeni kuna makaburi mengi sana . Kiukweli niliogopa Sana ! Japo Mimi mwenyewe nilikua natisha ukinitazama lakini,na Mimi pia niliwaogopa wenzangu nilipo watazama ! Walikua wanatisha Sana.!

Uwanja huo siku ufahamu kwa haraka kwani sikua mtu wa kutembea tembea sana maeneo.

Basi kwakua watu walijaa Sana uwanjani,na sisi pia tukatafuta siti na kuketi. Tukawa tuna sikiliza kinacho zungumzwa na mkuu pale katikati ya uwanja.    " Karibuni Sana wanachama wenzangu,katika utangulizi wa  sherehe yetu ya kuwakaribisha wanachama wapya katika utawala wetu" 

Watu walishangilia Sana kwa sauti zenye milio tofauti za wanyama ,yani wengine walilia Kama paka , wengine Kama farasi ,Simba ,bundi yani kila mtu alikua na mlio wake ! Niliogopa Sana kwani hata bibi nilie kaa karibu nae ,pia nae alishangilia kwa kulia Kama paka shume " nng'aaaaaaaaaauuuuuuuuuuu!" 

Haisee! Muda mwingine nilitamani hata kumkimbia bibi lakini sikua na jeuri hiyo.


" Bila kupoteza muda,tunawaomba watu wafuatao waje hapa kati, aje binti nuru,aje kijana Lazaki,aje binti Chuma,pia aje na mwana dada Maria ."

  Nilishtuka sana nilipo lisikia jina langu lakini Cha kushangaza nilijikuta nakwenda pale kati bila mwenyewe kujielewa . Wote tulio tajwa tulienda pale katikati ya uwanja kwa mkuu ambae alionekana kutisha zaidi ya wengine. Mkuu akanyosha msinga wenye manyoya ya mnyama was hajabu Kisha akatupiga piga nao usoni Kisha akanyosha mkono wa kushoto likaja kapo kubwa lililojaa vibuyu tofauti tofauti. Akatoa dawa ya mgando katika kila kibuyu akazichanganya Kisha akatuchanja chale za kutosha na kutupaka ile dawa .Alipo maliza akasema karibuni Sana ,nasi nasi kwa pamoja tukajibu  Asante sana mkuu.


" Ndugu zangu Sasa mmekua mafundi,hakuna mtu wa kuwasumbua duniani hapa ,labda mbinguni! Zoezi la kuwapa mikoba limekwisha,kilichobakia ni kuwaapisha ambapo zoezi hilo litafanyika kesho juma tano kuanzia saa kumi jioni.Leo tutashangilia kwa pamoja kwa kuimba na kucheza pia tutakula na kunywa.hivyo kila kamati ijiandae kwa majukumu yake . Kamati ya mapishi naomba mchangamshe mikono Wakati tunaendelea kuburudika kwa ngoma na kucheza baada ya hapo tunataka kula "

 

Mkuu aliongea hivyo Kisha ngoma zikaanza kupigwa lakini nilishangaa Sana baada ya kuona ngoma zinazopigwa haziku ngoma Kama unavyo fikiria,bali walikua watu wakipigwa vichwa na wengine walipigwa makalio na kutoa mlio Kama ngoma iliyo wambwa kwa ngozi!!

Tulicheza Sana kwa kuimba kwa sauti kubwa yani endapo watu wangetusikia majumbani basi ni lazima wangetoka kututazama.

Mkuu alinyoosha msinga wake juu ,ngoma ikazima na wale watu waliofanywa kua ngoma walionekana kuchoka Sana. Mkuu aliwanyoshea msinga wake ,wale watu wakatoweka!!

Sijui walipokwenda ila nafikiri walirudishwa makwao.

    

"Ndugu washirika wenzangu,baada ya kucheza vya kutosha ,na kuimba vya kutosha ,Sasa ni muda muhimu wa kula chakula chetu pendwa . Chakula kipo tayari ,bakia hapo hapo ulipo utaletewa chakula chako" 

Mkuu baada ya kumaliza maneno hayo,mara watu wa hajabu wakaanza kugawa chakula kwenye mabakuli makubwa Sana yakiwa yamejaa mapande makubwa ya nyama huku yakiwa na mchuzi mwekundu wa kutosha. Chakula kiligawiwa kwa haraka ,muda huo sisi pia tukiwa katikati ya uwanja Kama wanawali,pia tuliletewa msosi wetu kwenye mabakuli makubwa . Tukala na kunywa bila kuhofia msosi ulikua mtamu Sana kwani ulikua unafanana kabisa na utamu wa supu niliyo kunywa kule Kenya. Nilikunywa na kula bila hofu kwani niliufurahia msosi ule, kiukweli ilikua ni damu mbichi ya mtu pamoja na minyama nyama ya mwili wa mwana damu.


Tulipomaliza kula na kunywa mkuu akasimama na kutupongeza wote tuliojiunga na uchawi siku hiyo na kusema kua kesho juma tano tusisahau ,saa kumi kamili jioni tukutane kwenye pori la kusimikwa .


"Ndugu zangu sherehe yetu imeisha ,ila kesho juma tano chonde Sana,walengwa wote tukutane kwenye pori la kusimikwa kwa haraka kwa muda uliotajwa, kwa Sasa hakuna Cha zaidi ,kusanya kilichochako kila mtu arudi nyumbani ila msikose kuwanga japo nyumba moja kabla hamjaenda kulala makwenu"


"Sawa mkuu" watu wote tuliitikia kwa pamoja Kisha tukapiga miguu chini na kutoweka kwa ghafla .Mimi na bibi tukakutana kwenye njia panda moja karibu na makazi ya watu ,ikiwa kunakaribia kupambazuka kabisa,bila hofu tuliingia kwenye nyumba moja ya mchungaji Boniface ,tuliwanga kwa kusota sota kwa makalio kuanzia sebuleni mpaka vyumbani walimo lala. Kiukweli mchungaji Boniface alikua mwepesi Sana ,alikua anamwongopea mungu hakua mchungaji kweli alikua tapeli yani ni nabii wa uwongo. Tulimchezea Sana mwisho tulimbeba na kumlaza nje ya nyumba yake Kisha sisi tukaondoka zetu nyumbani. Tukalala kidogo asubuhi na mapema ikawadia . Bibi aliniambia kua nijiandae mapema kwani saa kumi kamili inatakiwa niondoke ili nikasimikwe.


Siku hiyo nilichoka kiasi nikaenda kuoga Kisha nika andaa chai Kama kawaida Mimi na Bibi yangu tukanywa huku story nyingine zikiendelea. Muda ulisonga mbele hatimaye saa kumi kasoro dakika tano,nilishtuka bibi akiniamsha kumbe nilipitiwa na usingizi,Bibi alishapika Cha mchana Lakini sijala tukaingia ndani na kuvaa mavazi yetu ya kazi. Tukapiga miguu chini na kuibukia kwenye msitu mkubwa ambapo tuliwakuta wenzetu walishafika nilikua nasubiriwa Mimi tu!

 

"Afadhari bibi mbokeleni na chuma kwa kufika maaana mlikua mnatuchelewesha"

Aliongea mkuu mwenye sura ya kutisha.

"Bila ya kupoteza muda walengwa wote njoeni mkae chini ya mti huu" ulikua ni mti mkubwa sana ,tulikaa pale chini tukiwa uchi ,mkuu alitambika kwa lugha yake tusio ielewa ,mara ghafla ikanyesha mvu kubwa japo kulikua na jua kari la saa kumi.Yani kulikua na mvua na jua kwa pamoja. Waswahili wanasemaga eti,simba anazaa!!!!  Dhana hii imeenea Sana mtaani kwamba jua likiwaka na mvua ikinyesha kwa pamoja eti,Simba ana zaa, ukweli ni kwamba ukiona jua linawaka na mvua inanyesha kwa pamoja, ujue kuna wachawi wapya wana hapishwa na wamekubariwa kupokea nguvu kutoka kwa shetani wa kichawi.


Basi,mvua ikaendelea kunyesha na jua likaendelea kuwaka ,mara ghafla mvua ikakata na likabakia jua Kama kawaida. Mkuu wetu alicheka Sana , akasema kwamba " vijana wangu mmepokea nguvu kubwa Sana za kuusumbua ulimwengu, natumaini mtakua mawakala wazuri Sana wa shetani katika kuleta ubovu ulio kidhiri katika Dunia . Mbarikiwe Sana na lusifa ,na mkafanikiwe katika kutenda dhambi zenu zilizobarikiwa na shetani". 

 Mkuu alipomaliza kusema hayo Mimi nikajihisi mwenye nguvu Sana na nikajikuta naweza kufikiria na kufanya mambo makubwa bila ya kufundishwa. Macho yaliniwiva kama nyanya ya utunguja. Mkuu alinitazama Kisha akasema " Chuma ,wewe unaonekana kua na nguvu nyingi sana ,kafanye kazi ,jamii ikutambue na kukuogopa ,hakuna kiumbe atakae weza kukudondosha , ulimwengu ni wako chuma , chochote unaweza kufanya kuanzia Sasa,umesha pewa nguvu ya mamlaka!"  Hayo yalikua maneno ya mkuu akinisifu,baada ya hapo tukanyanyuka na kurudi nyumbani baada ya kuruhusiwa na mkuu.

********************************************

                      ITAENDELEA.


JE,nini kitafuatia? Sasa chuma amesha kua kamili ,unafikiri nini kitaendelea? Usikose kufuatilia sehemu ya 4,ya URITHI WA BIBI. UHONDO NDIO KWANZA UNAANZA. Fanya ku LIKE PAGE, NA KU SHARE,Ili wengine waone na kuburudika.

URITHI wa Bibi 2

 story : URITHI WA BIBI. EP.2

 ( Grandmother's inheritance.Ep.2)

Author :  Steven Morgan

Email : stevennemes2k@gmail.com


Kabla hatujaendelea ngoja tukumbushane kidogo pale tulipoishia.

Ndugu msomaji tumeona jinsi binti chuma mashaka anavyo fundishwa jinsi ya kuendesha aina za ndege za kichawi .Tumeona kati ya mifagio miwili, mkubwa wa nje wa chelewa na mdogo wa ndani wa ukindu pamoja na ungo, vyote vikiwa ni aina za usafiri wa kichawi.Tumeona bibi yake na chuma amechukua ungo na kuweka manjonjo yake kisha kwa pamoja na mjukuu wake chuma walianza kuyakata mawingu kwa raha zao! Lakini baadae bibi aliamua kumpeleka mjukuu wake kenya ,kwa  usafiri wa ungo ,lakini mambo yalikua mabaya kwani baada ya kufika kwenye anga la kanisa moja la kiroho mjini Nairobi, ndege yao iliyumba na wote walishuka chini kwa kasi pamoja na ungo wao.!! Lakini bibi ghafla alipaa juu na kutoweka kabisa maeneo yale ,alibakia mjukuu wake Chuma ambae ndio siku  yake ya kwanza katika shughuri za uchawi.Masikini chuma amebakia yeye mwenyewe akiwa uchi wa mnyama pamoja na ungo wake asijue cha kufanya ndani ya uwanja wa kanisa la kiroho.Ikiwa ni bado usiku sana chuma akatulia akisubiri asubuhi ifike ili azijue mbivu na mbichi.

Nini kiliendelea? Chuma anaendelea kusimulia  Endelea nayo.


Nikiwa bado nipo nje ya kanisa la kiroho nikihangaika,lakini hakuna nilicho kifanya zaidi ya kubakia palepale ,nililitazama lile kanisa, kwa juu lilikua limeandikwa (Kenya assemblies of God - Buruburu). Usiku ule wote ukaniishia mimi yani kama waswahili wanavyosemaga kua ,usiku wa deni haukawii kucha (the night of debt does not last long), ndivyo ilivyokua ,asubuhi ikafika ,maana nilianza kusikia sauti za ndege wakilia na majogoo yakiwika.Lakini kuna sauti nilikua nikiisikia ikipenya masikioni mwangu kama sauti ya bibi! Ikiniambia "chuma ili upate msaada ,inakupasa ulale kifudifudi muda wote yani ulalie tumbo,kinyume na hapo utaumbuka,zingatia hilo sasa" sauti hii ilikua ikijirudia rudia mpaka masikio yalikua yanauma . Kulizidi kupambazuka na kua kweupe,!! Ghafla nikasikia mayowe mtu akiita "jamani mje mjionee maajabu,mchawi amenasa hapa kanisani!!" Nilishtuka sana,kumbe alikua ni mlinzi wa kanisa tayari ameshaniona!! Haraka nikalala kifudifudi huku furushi langu la makalio yakiwa juu na ungo ukiwa pembeni.Watu walijaa sana,kila mtu alisema lake huku mwingine nilimsikia akisema "jamani afu mchawi mwenyewe ni binti mdogo sana,bado mwali alafu ana umbo zuri!!"

Sikuyajari maneno yao ,mimi niliendelea kulala kifudifudi huku watu wakiendelea kuyashangaa makalio yangu yalio chafuka kwa vumbi na maungaunga ya kichawi. Nilijisikia vibaya sana ila sikua na namna. Mara nikamsikia mtu akiongea na simu.."haloo mchungaji,wahi kanisani,kuna mchawi mtoto ameanguka"  Nilishtuka tena kwa presha baada ya kusikia kua mchungaji anakuja!! Niliona sasa huo ndio mwisho wangu! Watu walizidi kujaa na mimi nilizidi kuduwaa huku nikiwa nimelala chali.

Huwezi amini ghafla nikamwona mmama mmoja akipenya kwenye ule umati wa watu na kunijia mimi huku akiwa uchi !! Bila shaka alikua haonekani na watu wengine zaidi yangu.sura yake ilikua ni ngeni kwangu ! Lakini akaja akaniezeka kibao kimoja cha makalio kisha akaniambia kua ninyanyuke tuondoke kwani hakuna mtu anaeniona kwa sasa!! Nikweli sikuonekana maana ghafla! Niliwasikia watu wakisema huku wakikimbia kua "ameyeyuka" "jamani ameyeyuka yeye na ungo wake!!"  Kiukweli sikuyeyuka bali,nilipotea kwenye macho yao kimiujiza baada ya yule mama kuja kunigusa na kuninyanyua.kiukweli yule mama alie nisaidia ,alikua ni mchawi wa kulekule kenya ! Ila amenisaidia kwa kunipa nguvu tena za kichawi .Ngoja nitoboe siri moja hapa,kwamba mchawi yeyote anapokwama sehemu,asipolala kifudifudi ,hawezi kupata msaada kutoka kwa washirika wenzake labda ajiokoe mwenyewe.

Basi watu wakawa wanatimka huku na kule huku na sisi taratibu tukaondoka kwa miguu mbali kidogo na kanisa nikiwa na yule mama,wote tukiwa uchi na kuto kuonekana (invisible). Yule mama aliniambia kua nisiogope ,kwani atanisaidia kurudi nyumbani Tanzania.Nikiwa nimeshika ungo wangu yule mama ,akanikumbatia ,ghafla tukapotea  nikaja kushtuka ,nikajikuta nipo ndani ya nyumba ya yule mama . "Itakubidi leo ushinde hapa kwangu mpaka usiku Ili niandae usafiri wa haraka kwaajiri yako."yalikua ni maneno ya yule mama nami,sikua na lakusema zaidi ya kumshukuru.yule mama hakutaka kunijua sana zaidi ya kutambua kua Mimi ni mshirika mwenzake. Ikawa hivyo ,nilishinda kutwa nzima kwa yule mama!! Mpaka giza likaingia ,ilikua ni usiku wa saa mbili, Kama kawaida yule mama aliingia ndani na kutoka na fagio kubwa la njelewa likiwa na mpini mrefu ."Binti unajua kuendesha usafiri huu?" Aliniuliza. "Hapana mama ,Mimi bado mgeni Sana kweye hayo mambo " nilimjibu.  " Sawa ,Sasa ngoja kwanza nikuandalie chakula Cha kichawi ,maana huwezi kunitembelea ,alafu uondoke bila kula hata supu." Nilishtuka sana .. "chakula Cha kichawi?" Nilimuuliza. " Ndio ,kwani hujawahi kula? Mbona unaonekana kua ni mgeni sana?" Aliniuliza.. "ni kweli mama yangu ,ndio kwanza siku yangu ya kwanza leo,bibi yangu alinibeba,hivyo Sijui mengi sana!!" Nilimjibu yule mama. Yule mama akacheka sana ,Kisha akaingia tena chumbani kwake na kutoka na bakuri kubwa la aluminium,likiwa limejaa nyama nisio ijua na mchuzi mwingi ila ulikua mwekundu sana.


"Kunywa na kula hizi nyama ,kutakufanya wewe uwe na nguvu nyingi,hebu kula kwanza alafu ntajua Cha kufanya!" Alinifosi kunywa ile supu,niligoma lakini akanifosi mpaka akaninywesha! Sio Siri ule mchuzi ulikua mtamu sana,japo ukiutazama ilionekana kua ni damu kabisa.sikua na jinsi ,kwakua nilikua na njaa Kali,nikala na zile nyama zote,nazo pia zilikua tamu sana ,yani utamu wake sijui nifananishe na mnyama gani!!! 

"Vizuri Sana binti, unaonekana ni muelewa Sana ,Sasa usafiri uko tayari lakini kabla hatujaondoka inatakiwa twende tukawachawie watu kwanza (kuwanga) ili kupata nguvu zaidi!"  Aliongea yule mama huku Mimi nikitikisa kichwa ,kama ishara ya kumkubalia.

Yule mama akiwa uchi kama mimi lakini ukimtazama alionekana Kama amevaa kaniki ,alinichukua nakutoka nje ya nyumba yake,akanishika mkono Kisha akapiga mguu chini kwa nguvu!! Ghafla tukajikuta tupo kwenye mitaa flani huko ulaiyani kwenye makazi ya watu. Tukaenda kwenye nyumba moja ambapo tulitua juu ya paa,kwakua ilikua mapema Kama usiku wa saa tatu hivi, wenye nyumba walikua bado hawajalala ila watoto zao baadhi walionekana wamelala vyumbani. Kwakutumia maneneo makali ya kiimani tuliweza kuingia ndani bila ya kufungua milango,tulifikia sebuleni ambako tulimkuta mtu na mke wake wakitazama sinema runingani.Tukaanza kuwazunguuka kwa kuwasoteasotea na makalio.Kuna muda Kama walikua wakihisi Kama kuna Jambo linatendeka! Lakini hawakua na uhakika .Nilimsikia yule mzee akimwambia mkewe .. "mbona nyumba imekua nzito ghafla? itakua kuna wachawi wameingia mke wangu,hebu niletee ile biblia yangu." Tuliposikia habari ya biblia tukashtuka automatic na kujikuta tupo nje juu ya paa, kule ndani walianza kufanya maombi mazito wakilitaja mara nyingi jina la Yesu na Mungu baba. Sio Siri tulipata tabu Sana , nikajihisi Kuungua mwili mzima ,yule mama akanishika mkono ,tukakimbia huku atua zetu zikisikika kwenye mabati ,tuliruka na kupaa Kama ndege na kwenda kutua barabarani. Asikudanganye mtu,neno la mungu ni kiboko ya wachawi haswa unapomtaja mara nyingi bwana yesu na Mungu baba,mchawi hawezi kukukalia karibu. 

Basi baada ya hapo tukaenda kwenye nyumba nyingine ambapo ile tunatua tu kwenye paa,tulihisi Kama tumekanyaga misumari ya Moto !! Haraka tena tukakimbia kwa kuruka juu na kutua mtaa wa pili!!   Nikaamua nimuulize yule mama kua inakuaje lile paa linaumiza namna ile? Akaniambia kua yule mwenye nyumba aliweka chumvi ya mawe batini ndio maana ilitupa shida.Hapa naomba nikufafanulie kidogo ndugu msomaji kuhusiana na chumvi ya mawe. Chumvi ya mawe ni ulinzi mkubwa sana wa nyumba yako Kama hutaki wachawi wakujie.Unaweza kuchukua chumvi kidogo ukanuiza na maneno kidogo alafu ukairusha batini ,hapo mchawi hawezi kuingia ndani,au ukachukua chumvi kidogo alafu ukaiweka kwenye kila pembe  au cona ya nyumba yako ,hapo pia mchawi hawezi kuingia wala kutoka .Au ukachukua chumvi ya mawe na kuiweka kwenye mvungu was kitanda unacho lalia ,hapo mchawi hata Kama ameingia ndani,lakini hatoweza kukusogelea au kukugusa.Huwezi amini lakini ukweli ndio huo ,Kama unasumbuliwa Sana na wachawi, fanya hivyo ,utalala vizuri sana bila kuchezewa.Kama uhamini ngoja nikuhaminishe kitu, je,umeshawahi kujiuliza kua ,ni kwanini kanisani maji ya baraka wanaweka chumvi na sio sukari? Jiulize vizuri ndio utahisi kua chumvi  ya mawe ina Siri nzito kuliko haya niliyo kueleza.

Basi tukiwa bado tupo pale njiani Mimi na yule mama mkenya,tukawaza Cha kufanya nini, mwisho yule mama akasema kua twende kwenye nyumba ya mwisho kwa kijana mmoja hua anaringaga Sana wacha tukamkomeshe.Tulishikana mikono na kuruka juu sana na tulipotua , tulitua kwenye paa la nyumba la huyo kijana.Mama akanyoosha mkono juu ikaja dawa flani ya ungaunga akaiweka batini nyingine akaipeperusha kwa kuipuliza .Kisha akasema kua Mustafa hajalala  bado ,huyu kijana ni mbishi Sana,ila muda si mrefu atalala tu. Tukasubiri kidogo baadae tukaingia ndani tena chumbani kwa yule kijana! Tulimkuta akiwa amevalia bukta huku akiwa tumbo wazi na mikono yake ikiwa nyuma Kama ameficha kitu . Niliogopa Sana kwani yule kijana alikua akitutazama sana mpaka nikahisi kua huenda ikawa anatuona. "Mama mbona huyu kijana anatushangaa Sana! Au anatuona?" Nilimuuliza mama .. " mh! Sidhani Kama atakua na uwezo huo!"  Alijibu mama kwa hofu. Lakini tulipo angalia pembeni mwa kile chumba tukayaona marimao kadhaa na sindano zikiwa zinaning'inia juu yake! Mama alishtuka Sana Kisha akasema " tukimbie tunaonekana!!" Wakati huo yeye tayari ameshapiga guu lake chini na kutoweka peke yake.Na Mimi nilitaka kufanya hivyo, lakini kabla sijanyanyua mguu yule kijana alinikamata na sikuwa na ujanja tena!! .


Nilijiona mtu mwenye mikosi Sana kwani ,kila mara Mimi ndio wa kukamatwa tu! Kumbe yule kijana aliweka mtego wa kuona wachawi .Hata wewe ndugu msomaji endapo utachukua malimao au ndimu Saba,na sindano za kushonea nguo kwa mkono saba, Kisha ukachukua kila sindano moja ukaichomeka kwenye ndimu au rimao lake ,usiikandamize Sana,choma juu juu ili sindano ining'inie Kisha chukua hizo ndimu weka eneo ambalo upo Kisha tulia,hapo unaweza ukaona vitu vilivyo jificha visionekane kwa macho.(invisible) Lakini nikuonye usije ukafanya zoezi hili Kama una roho nyepesi ,maana wachawi huwa wanatisha Sana wanapokuja kwako.Kabla hujafanya hivyo jiulize kua baada ya kumwona mchawi utamfanya nini? Je, unaweza kumkamata akiwa na sura ya kutisha? Kama huwezi usijaribu ni hatari Sana.

Basi,nikiwa mikononi mwa yule kijana Mustafa ,sikua na ujanja kwani mchawi ukisha kamatwa huwezi fanya lolote zaidi ya kuokolewa baadae na mchawi mwenzio. " unaitwa nani wewe binti?"  Ilikua ni sauti ya ukari ya yule kijana aliniuliza. " Naitwa chuma" nilimjibu. " Chuma! Hahahaha haa! Chuma leo hunaga bahati " alishangaa yule kijana Kisha akasema .." chuma wewe unaonekana ni binti mzuri Sana ,una umbo zuri ,makalio makubwa Sasa kwanini,unakua mchawi ? Ona Sasa ulivyojiweka Kama kinyago Wakati wewe ni mrembo!!!" Yalikua ni maneno ya yule kijana Mustafa. Mimi sikujibu chochote zaidi ya kuinamisha kichwa chini kwa haibu!!  " Sasa nikufanye nini binti chuma?" Aliniuliza lakini nilinyamaza kimya . Sauti ya hajabu ikapita masikioni mwangu kua nilale kifudifudi ili nipate msaada ,nami nikafanya hivyo muda uleule ,yule kijana Mustafa alishangaa Sana kua nina maana gani ya Mimi kulala pale sakafuni kifudifudi huku makalio yangu yaliyojaa minofu yakiwa juu yakitikisika. " We binti ndio nini Sasa?, Au una nitega? Nitakubaka kweli Mimi mwenyewe nimedata vilevile!" Nilishtuka nilivyosikia yule kijana Mustafa anataka kunibaka ,nilimtazama nikaona taratibu bukta aliyovaa inanyanyuka juu yani tayari alishakua na hisia Kali na Mimi japokua nilikua Kama kinyago lakini Mustafa alivutiwa na Mimi,ama kweli huyu kijana ni jasiri Sana kwa mtu mwingine huwezi kunitazama mara mbili,nilitisha sana.

Taratibu Mustafa akaanza kunisogelea pale nilipolala na akaanza kuyachezea makalio yangu ,nikajua Sasa muda si mrefu huyu kijana atanibaka !!

Nikatulia Kama maji ya kisimani,ghafla mbele yangu namwona yule mama mkenya ananipa mkono ,nami nikamshika  mkono tukapotea na kuibukia nyumbani kwa yule mama mkenya. " Pole Sana binti,hizi ni ajari ndogondogo huwa zinatokeaga maana siku hizi watu wengi wanajua jinsi ya kujikinga na wachawi." "Asante mama "  nilijibu.." ehee! Nambie ,vipi yule kijana Mustafa mbona alikua anakuchezea makalio alikua anataka kukufanya nini? ".   "Alikua anataka kunibaka !!" Nilimjibu . " Kukubaka? Huyu kijana ana hatari kweli na angesubutu kufanya hivyo, basi jua la asubuhi ,asingeliona tena,angekufa.!  Alishtuka yule mama alivyosikia kua nilitaka kubakwa ningari kwenye hari ya vazi la kichawi. Baada ya hapo yule mama akauchukua ungo wangu na kuupigia maombi maarumu Kisha ule ungo ukapotea  kimiujiza. Kisha akachukua lile fagio lenye mti au mpini mrefu akanishika mkono ,akapiga guu lake chini tukatokea njia ya panda .Akaniambia Sasa muda wa kurudi nyumbani Tanzania umefika.Ilikua bado ni usiku Sana Kama Sasa nane hivi! Baada ya hapo akaulaza ule mfagio chini Kisha akanipaka dawa flani nayeye pia akajipaka Kisha tukaukalia ule mfagio.sijui nini kilitokea lakini tukajikuta tupo juu ya anga kwenye spidi Kali zaidi ya ndege za kivita!! Haikuchukua dakika nyingi tukajikuta tupo nje nyumbani kwa bibi. Bibi alitoka nje akiwa kwenye hari yake ya kichawi,akatupokea na akamshukuru Sana mshirika mwenzake raia wa Nairobi Kenya. Yule mama hakutaka kukaa Sana alituaga na akaondoka na usafiri wake kwa haraka. 


*********** ITAENDELEA ***************


Je,nini kitafuatia? Usikose kufuatilia sehemu ya tatu ya URITHI WA BIBI.Uhondo ndio kwanza unaanza. Hujachelewa, fanya ku LIKE PAGE, COMMENT , au SHARE ili wengine wapate kuburudika na kuelimika pia.Asante.

URITHI wa Bibi 15

 Story... URITHI WA BIBI EP.15. Mwisho. Mtunzi....Steven Morgan πŸ“²......... 0659115223 Naam kwa Mara nyingine tena ndugu msomaji tumekutana ...