Ijumaa, 8 Novemba 2024

URITHI wa Bib 6

 Story .......... URITHI WA BIBI EP. 6

Author..............Steven Morgan

Contact : ...WhatsApp.. +255 659 115 223


Naam ,kwa mara nyingine tena kwa neema za mungu tumekutana tena katika sehemu ya sita ya story yetu. Tumshukuru Kwanza mungu kwa neema zake pia atusamehe pale tulipokosea na awasamehe pia wale wanao endelea kutukosea maana hawajui wanayo yatenda. Hatupaswi kuhukumu anaye hukumu ni Mungu pekee,sisi yatupasa kujirinda tu dhidi ya wale wabaya.

Nb: Tumtangulize Mungu kwa Kila Jambo maana, Yeye ndie muweza wa yote.


Story yetu tulipoishia ndipo tunapo anzia ili twende sambamba.


TULIPOISHIA....👇


Mama mwenye nyumba alinielekeza mambo mengi haswa majukumu ya kazi. Nikaingia chumbani kwangu nikabadirisha nguo,Kisha nikatoka nikiwa na kanga moja ambayo imenichora umbo langu la mwili haswa makalioni ambapo sio siri ,sijisifii  kweli Mungu amenibariki minyama ya makario. 

Nikakatiza pale sebureni ambapo alikaa baba mwenye. Nyumba na mkewe .  Nilijisahau nilijua kua bafu na choo vipo nje hivyo, nilitaka kutoka nje. " Wewe binti vipi! Mbona hivyo?" " Naenda kuoga mama!"   " Wewe si nilikwambia kua bafu na choo vipo chumba Cha tatu pembeni? Sasa huko nje unaenda wapi!  Au umeshazoea huko kwenu vijijini milimani huko?

" Nilijisahau tu mama samahani!"  " Sawa Chuma tumekuelewa  nenda tu kaoge mama!!"  

Aliongea mzee Foya huku akinitazama kwelikweli. Basi nikageuka na kuelekea huko bafuni . " We baba Maria vipi? Mbona unamtazama Sana yule binti kwa nini?" 

Nilimsikia mama mwenye nyumba akimsema mmewe kua alikua akinishangaa Sana. Nafikiri ni kwa sababu ya ile kanga niliyovaa na umbo langu ,lilimpa shida Sana.

 Basi nikaelekea bafuni ,ile nafungua mlango tu!

Namwona bibi yuko kule bafuni,kiukweli nilishtuka Sana ,ilibaki kidogo tu ,nipige kelele.

" Tulia Chuma, nimekuja tu kuona unapokaa ,ni pazuri Sana, nafikiri tutaonana baadae ,mida ya kazi,kuna kazi ya kufanya leo". "sawa bibi" 

 Bibi alitoweka Kisha nami nilioga na kuondoka chumbani kwangu.

Ile naingia chumbani tu! Nakuta kioo kipo kitandani kwangu. Kioo hiko hakikua kigeni kwangu kwani nilikitambua vizuri tu ,kua ndio kile alichonipa Bibi na nilikiweka kwenye begi langu ,Sasa sijui kilitoka vipi kukaa pale kitandani.!! Nikakisogelea Kisha nikakitazama ,nilichokiona ni tofauti na nilicho kitarajia! Nilijua nitajiona Mimi mwenyewe,lakini, huwezi amini,nilimwona Bibi zubeda wa kule kwetu morogoro, ambae ana undugu na mzee Foya, na mzee Foya ndipo alipofikia  kwa Bibi zubeda ambapo siku moja kabla ya kuja huku dar tulienda na Bibi kumwangia mzee Foya na ndipo nilipo kwama kwenye tumbo la mzee Foya.

Sasa tuachane na hayo,turudi pale ndani chumbani kwangu ,nilizidi kukitazama  kile kioo,nikamwona Bibi zubeda akiniteta na jirani yetu mmoja wa kulekule nyumbani . Huyo jirani alikua anaitwa mama majuto ,alimpelekea umbea Bibi zubeda kua eti Mimi na Bibi yangu ni wachawi Sana na pia ikiwezekana, wamwambie mzee Foya kua Mimi ni mchawi anifukuze. Kama nilivyo eleza hapo  mwanzo kua ,kioo ni msaada mkubwa Sana kwa wachawi,nimeweza kumwona Bibi zubeda kwenye kioo changu Cha kichawi kwa sababu yule Bibi zubeda na mwenzake walikua wakizungumza sehemu ambayo kulikua na kioo kilichokua wazi yani hakikufunikwa. Kwa hiyo kwetu sisi inakua ni Kama CCTV camera.

  

Basi baada ya hapo Sura ya Bibi zubeda na mwenzake zikapotea Kisha ikaja sura ya mkuu wetu wa uchawi, mkuu alinikazia macho Kisha akasema ," Chuma nadhani unajua Cha kufanya" Kisha mkuu akapotea. 

Nikamwita Bibi zubeda kwenye kioo akatokea tena. Nikachukua begi langu Kisha nikatoa mdori wa kike, nikaanza kuukaba kwenye shingo ule mdori huku nikinuiza maneno ya ufundi. Mara nikaanza kumwona Bibi zubeda kwenye Koo akijishika shingo huku akitoa macho ,kuhashiria maumivu makari. Alihangaika mpaka alianguka chini ,huku Mimi nikiwa bado naendelea kumkaba yule mdori ,mwishoni nikamnyonga shingo ya Yule mdori ,na Bibi Zubeda nae alijinyoosha palepale. Yani nimuua kabisa asije akaniharibia kwa bosi wangu Foya.

  Nikachukua kile kioo na kukirudisha kwenye begi, nikikabadili nguo Kisha nikatulia kitandani. Mara nikasikia mama Maria yani mama mwenye nyumba ananiita, " Chuma , Chuma toka uje tule " kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona ..................................

      

        ENDELEA 👇

"Chuma,chuma  toka nje uje tile"

Kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona Bibi amekaa pale kwenye Kochi katikati ya mzee foya na mkewe bibi nae aliketi. Nilishtuka sana mpaka mama Maria na mumewe mzee foya au baba Maria walishtuka sana. " Vipi Chuma mbona umeshtuka ghafla kwa hofu ? Vipi! ". Alihoji bosi wangu mama Maria mke was mzee foya.  " Hapana mama niko sawa tu!" Nilijibu kwa mkato Kisha nami nikaketi kwenye Kochi la mtu mmoja lililokua pembeni.


Nikajisevia chakula pale mezani Kisha bibi nae akajisevia chakula chake bila ya kuonekana na mtu. Mimi pekee ndio nilie kua namwona bibi. Wakati wote tunaendelea kula ,bibi aliniongelesha ,na Mimi pia nilimjibu yani tulikua tunaongea kwa sauti bila ya mtu mwingine kujua. Hapa utashangaa kua kwanini wengine hawakujua kua Mimi naongea na mtu mwingine? Kiukweli mchawi huwa aongei taratibu yani hanong'oni ,kwani kama mchawi akijaribu kunong'ona basi Kila mtu anaweza akamsikia. Ndomana Mimi na Bibi tulikua tunaongea kwa sauti ili tusishtukiwe . 

" Vipi Chuma mbona unakula huku unaimba ,utajing'ata shahuri yako!!"

 Aliongea mama Maria. Lakini kiukweli nilikua siimbi wimbo wowote ila ,nilipokua nanyanyua mdomo na kuongea kwa sauti na bibi, kumbe wao walinisikia ila walinielewa tofauti yani wao walinisikia kama vile nilikua naimba kumbe nilikua naongea na bibi ambae wao hawaku muona.

Mimi na bibi tuliendelea kuongea mambo mengi haswa yale mauaji ya Bibi zubeda tuliyo yafanya jioni ile .


Baada ya hapo bibi akachota ubwabwa tonge moja kwenye sahani ya mke wa mzee foya yani mama Maria Kisha akalimeza lile tonge Kisha bibi aka anza kujibinya binya tumbo kama vile linamuuma. Mara ghafla! Mama Maria bosi wangu nae akaanza kujishika tumbo na kugugumia maumivu ya tumbo. Kumbe bibi alipochota lile tonge na kufanya alivyofanya, alimroga yule mama mwenye nyumba, ila huu urogi mdogo tu wa kumshikisha mtu adabu hauna madhara sana zaidi ya kuumwa na tumbo na mwishowe kuharisha.

 Ndugu msomaji bila Shaka kama utakua umewahi kula chakula alafu baada ya muda mfupi tumbo likakuuma sana tena sana mpaka unaacha chakula na kwenda kulala kidogo ili ujinyooshe upate nafuu.

Sasa hari kama hiyo huwa mara nyingi husababishwa na wachawi yani ukiona hivyo ujue, ulipokua unakula ,mchawi alikuja na kukitemea mate chakula chako Kisha akakuroga tumbo.!!!

Hapa naomba niwasaidie kidogo kuepukana na hatari hii. Dawa pekee ya kuepukana na mchezo huu ni, kama wewe ni mcha Mungu,Kabla ya kula kiombee chakula kwanza kwa imani yako Kisha endelea kula ,utakua salama. Lakini pia kwa wale wasiojua hata maana ya kusali na kumwomba Mungu basi, hakikisha unapokula chakula chochote unatumia kijiko cha Chuma na usipende kula chakula ukiwa nje ( hadharani) pendelea Kula  chakula ukiwa ndani na usisahau kutumia kijiko ,utakuwa salama katika janga hili.


"Chuma hebu mwangalie mama amepatwa na nini?" Ilikua ni sauti ya mzee foya. "Sawa baba" nilimjibu kwa mkato Kisha nikaanza kumwangalia mama Maria,muda huo bibi alikua akicheka na kung'ong'a kwa kukenua kenua meno huku akiwa kwenye muonekano wa kutisha kwelikweli.

"Chuma naomba uninyanyue taratibu unipeleke chooni "  mama aliongea Kisha baba nae alinyanyuka tukasaidiana kumnyanyua na kumpeleka chooni. Tukamwacha huko chooni huku sisi tukiwa sebuleni tunamsubiri. Muda huo watoto walisha lala muda Maria na kaka yake Matias. 

"Chuma hebu wachukue hawa watoto kawalaze chumbani kwao."  "Sawa baba" nilimjibu bosi Kisha nikaanza kumnyanyua Maria nikampeleka chumbani kumlaza Kisha nikamrudia Matias lakini wakati namrudia matiasi ,bibi pale alipokaa kwenye kochi bado alikua akiendelea kucheka sana Kisha akanioneshea ishara ya kuniaga Kisha akatoweka. Wakati namnyanyua mtoto Matias,simu ya bosi ikaita ,wakati bosi anaongea na simu Mimi nilisha ondoka kumlaza Matias chumbani. Ile natoka kuja tena sebuleni,namkuta bosi mzee foya analia machozi mwamwamwa.. " bosi vipi tena kulikoni?"  Nilimuuliza ili nijue kinacho mliza ni nini? Japo moyoni nilijua nini kinacho endelea.

Alizidi kulia mpaka alianguaka chini na kugalagala!!!!

Mara ghafla akaja mkeo mama Maria kutoka kule chooni alipokua baada ya kusikia sauti ya mmewe akiria. Lakini baada ya kufika yeye, mmewe alinyamaza na akawa anamshangaa mkewe. Mimi na mama Maria pia tukawa tunamshangaa baba Maria kwa kua alikua akiria sana alafu akanyamaza ghafla kulikoni!!!

" Baba Maria mbona sikuelewi? Unachoriria ni nini? Na kilicho kufanya unyamaze ni nini?"


"Mama Maria ! Kwanza Kabla ya kukuambia ninacho lilia ! Naomba kwanza nikuambie kilichonifanya ninyamaze ghafla!!"

 "Sawa baba Maria nakusikiriza" alijibu mama Maria.

" Mke wangu, Mimi na chuma tulikupeleka chooni ukiwa hata kutembea huwezi! Sasa imekuaje umekua na nguvu za kutembea kwa haraka ukaja hapa sebuleni mwenyewe?"

" Baba Maria,baada ya kula kile chakula,tumbo lilianza kuniuma sana Kisha nikahisi kama vile nataka kwenda haja kubwa. Lakini ,mliponinyanyua na kunipeleka na kuniacha kule chooni,hakuna nilicho kinya zaidi ya kutoa upepo muda wote Kisha tumbo limetulia!! Haya Sasa nambie wewe unachoriria ni nini?

Mzee foya kabla hajaanza kuzungumza ,akaanza kulia tena huku akimtaja bibi zubeda wa morogoro.

"Jamani bibi zubeda wa morogoro,amefanya nini?" Aliuliza mama.  "Sijui" nilijibu Mimi kwa ufupi.  "Amefariki masikini wa Mungu!!!" Baba alionge kwa uchungu mkubwa. " Amefariki?" Alijibu mama kwa kushangaaa sana. " Ndio amefariki jioni hii hii ya leo,amekutwa ndani kwake ameanguka chini na kufariki " alizidi kuongea mzee foya.  "Alikua anaumwa?" Aliuliza mama. " Hapana kifo chake Wala hakijahusika na kuumwa itakua ni mambo ya ushirikina,na nikomgundua mtu alie husika na kifo hochi,basi na yeye nitamfanya mfu."" Aliongea mzee foya kwa uchungu


Mzee foya baada ya kuria kwa muda mrefu kutokana na taarifa ya kifo cha bibi zubeda wa morogoro,alinyamaza Kisha akamwambi mkewe aketi chini wazungumze kua itakuaje?

" Mke wangu kesho inabidi niwatangulize  huko morogoro kwenye msiba  mapema,lakini Mimi nitakuja jioni sababu kuna sehemu nitapitia  kutafuta ukweli wa kifo cha ndugu yangu bibi zubeda. Na nikimjua hadui alie husika ,hama zake ,hama zangu."  Mzee foya aliongea kwa hasira sana,huku Mimi na mama Maria tukiwa tumetulia kama tumezubaa vile. Basi kwa kua muda ulikua umeshaenda,Kila mtu aliingia chumbani kulala.............         ............    .................. .....

                         ITAENDELEA.


Je,mzee foya atagundua chanzo cha kifo cha ndugu yake Bibi zubeda? Je, na kama atamgundua hadui alie husika  ,nini atakacho kifanya? Hayo na mengine mengi usikose kufuatilia sehemu ya saba ya URITHI WA BIBI. 

Naamini kwa uweza wa Mungu tutakutana tena kipindi kijacho kunako majaariwa. Maarifana uhondo ndio kwanza unaanza ,Wala hujachelewa,mambo ni mengi sana ,muda  ni mchache.

Nb:Mtangulize Mungu kwanza kwa Kila Jambo.🙏

URITHI wa Bibi 5

 Story ...... URITHI WA BIBI EP. 5

Author..............Steven Morgan

📞..................... +255 659 115 223


🌷 TULIPOISHIA 🌷


Basi nikiwa bado nipo chumbani na Bibi huku nikikiweka kioo alicho nipa kwenye begi langu la kusafiria. Baada ya hapo  kwakua ilikua tayari ni usiku Sana ,tukatoka nje kichawi,yani tulitoka bila ya kufungua milango,moja kwa moja tulienda kwa Bibi zubeda ambae yule mgeni Foya ndipo alipo fikia,ilikua ni usiku Sana ,wote ndani walishalala fofofo, Mimi na Bibi tuliruka na kutua kwenye paa la nyumba la Bibi zubeda.Tulipotua juu ya bati,hapakua na kelele wala kishindo zaidi Kama aliekua ndani Kama hajalala basi anaweza akasikia Kama mchanga au vimawe mawe vinamiminika kwenye bati!! 

Ndugu msomaji ukisikia Hari hiyo,ujue wanga wamesha tua na Kama hujalala basi utalala kwa lazima .unachotakiwa kufanya baada ya kuona Hari hiyo ni kumwomba Mungu Sana akunusuru na ibirisi huyo.

Basi tukatua kwenye lile bati la bibi zubeda ,japo bati zake zili oza lakini hatuwezi kuanguka kwani tunakuaga wepesi sana . Tulimwaga madawa yetu ili asie lala kwa muda huo ,alale kwa lazima ili sisi tuendelee na kazi yetu.

Tulitazama kwa kupitia jicho la tatu la kichawi tulimwona yule bosi Foya anaye taka kesho juma tatu twende wote dares salaam amelala fofofo huku simu yake ya tachi ikiwa chini. Tulirukaruka huko juu ya bati huku tukiimba nyimbo za kichawi kwa sauti. Hata Kama hujalala huwezi kutusikia. zaidi, utahisi wimbo flani unao ufahamu ume play katika kichwa chako ,ukiona hivyo ujue wazee wa kiza wapo nje au ndani wanacheza na kuimba.   Basi tukacheza Sana Mimi na Bibi baadae  tukaingia ndani chumbani kwa yule mgeni Foya . Taa ilikua inawaka tukaizima  Kisha tukaanza kumsotea kwa makalio ,muda mwingine tulimjambia mdomoni akawa anashtuka na kukohoa  sana. Bibi aliniambia kua nimkalie tumboni kwa makalio yangu Kisha nimsotee sotee !! Nami nikafanya hivyo tena kwa haraka . Lakini ghafla yule mzee Foya alishtuka usingizini kwa haraka na akanikamata nikiwa palepale juu ya tumbo lake!!! Huwezi amini Bibi aliondoka na kuniacha nimekwama juu ya tumbo la mzee Foya ambae ni bosi wangu mtarajiwa  huku nikiwa uchi wa mnyama na makalio yangu makubwa yaliyojaziana minyama yakiwa juu ya tumbo la mzee Foya.

******* ***** ENDELEA 👇 ************

Nikiwa  bado nipo juu ya tumbo la mzee Foya ,sikua na ujanja kwani mzee Foya alinikamata kisawa sawa!! Nikajua sasa leo ndio mwisho wangu wa maisha ,nikahisi huwenda mzee Foya akanidhuru .  " Ahaaa! Kumbe ulijua Mimi ni mtu wa mchezo mchezo! Sasa Leo nakuua yani nakuchinja kabisa!!". Aliongea mzee Foya kwa kujiamini zaidi  huku Mimi nikitetemeka kwa hofu nisijue Cha kufanya. Nilihofia zaidi kwamba je,nitafanyaje endapo mzee Foya atanibahini? Maana mpaka muda huo bado  alikua hajanitambua kua ndio Mimi binti Chuma anaye taka kunichukua nikamfanyie kazi. Kulikua na giza nene pale chumbani sababu chemli iliyokua inawaka ,tuliizima mwanzoni kipindi tunaingia na Bibi . " Alafu unaonekana wewe ni binti mdogo kabisa kwanini Sasa  unakua shetani namna hii? Ngoja kwanza nifanye mpango wa kuwasha taa ili nikuone vizuri!"   Duh! Nilishtuka Sana kwani nilijua muda wa kumbuka umekaribia. Lakini kabla mzee Foya hajafanya chochote ,ghafla tu akatokea mkuu wetu, yule aliyetuhapisha uchawi. Akampiga kofi mzee foya la paji la uso,Foya akazimia Kisha akanichukua na kupotea ghafla,mara tu nikajikuta nipo juu ya kibeku yani ndege ya kichawi aina ya Air fagio plane( Broom air plane ) huku mkuu akiwa ndio dereva na Mimi nilikaa nyuma nikiwa kwenye umbo la nyau. Usafiri huu huwa ni wa haraka Sana Kama nilivyo elekeza hapo mwanzo. Hivyo mkuu alinifikisha mpaka mlangoni nyumbani kwa Bibi.Bibi alitoka nje haraka Wakati sisi tukiwa tunakaribia kutua.

" Bibi Chuma mnatakiwa kuwa makini Sana ,hata hivyo umefanya la maana Sana kunipa taarifa mapema. Raha sivyo leo Chuma angeumbuka." 

Hayo yalikua ni maneno ya mkuu akimwambia Bibi, kumbe Bibi baada ya kukimbia na kuniacha alitoa taarifa kwa mkuu ndio akaja kunipa msaada. 

" Na wewe chuma inabidi utulize akili ,ujitambue ! Wewe una nguvu Sana ila hujui kuzitumia,uwezo ulio nao wewe, chocho te waweza fanya , Chuma bila Shaka kesho ndio unakwenda kufanya kazi kwa huyo mzee Foya huko dar es salaam. Hakikisha unakua makini Sana usije ukakosea chochote. Yule mzee mpaka asubuhi akiamka hakuna chochote atakacho kikumbuka zaidi tu atakufuata ili muondoke,Mimi nakutakia safari njema pia ukatanye kazi yetu kwa weredi na umakini zaidi. Kwaherini!"

Mkuu baada ya kuongea maneno hayo,alituaga na akaondoka kwa usafiri wake wa haraka. Tukabakia Mimi na Bibi

Kwakua ilikua ni USIKU Sana, hatukuzungumza mengi ,tukaenda kulala ili kesho niwahi kuamka kwaajiri ya safari.

Kama wasemavyo waswahiri kua ,awike asiwike ni lazima kuche, Ndivyo ilivyokua , asubuhi ilifika ,nikajiandaa vya kutosha ,ninaposema nimejiandaa vya kutosha namaanisha nilifungasha Kila kitu kinacho nihusu haswa dhana za kichawi. Kumbuka hiyo ilikua ni siku ya juma tatu na ilipofika saa kumi na mbili asubuhi ,mzee Foya alikuja alinikuta nje na Bibi tukimngoja yeye tu! 

" Karibu Sana mzee foya ,mfanyakazi wako ndo huyu yuko tayari kwa Safari." Bibi alimwambia mzee Foya kwa msisitizo. " Asante Sana Bibi mbokeleni, Chuma..tusipoteze Sana muda wacha tuwahi gari la kwanza" 

Foya akatoa shilingi elfu 30 akampa Bibi Kisha sisi tukaondoka. Bibi alinipungia mkono Kila nilipogeuka kumtazama.

Tulifika msamvu mapema tukapata basi ,safari ilisonga mida ya saa kumi tukafika kwa mzee Foya maeneo ya Tabata shuleni. Tulimkuta mkeo na watoto wawili wa umri wa miaka 6 na miaka minne. " Karibuni wageni , karibuni sana,lete huo mzigo wako binti nikupokee!" Nilimpa begi langu mama mwenye nyumba ambalo lilikua zito Sana . " Heee! Mbona begi lako zito Sana,umeweka mawe nini?" Aliongea mama mwenye nyumba. " Kaweke huo mzigo bana mbona unataka kuchunguza mzigo usio kuhusu?" Alidakia baba mwenye nyumba Foya. Basi yule mama Akaniambia nimfuate,akaenda kunionesha ,chumba changu Cha kulala nikaingia nikaweka mzigo wangu. Kisha tukatoka akanitembeza nyumba nzima ,nikaona mazingira yote.akanielekeza na majukumu yangu ya kazi . " Hivi dada unaitwa nani?" " Naitwa Chuma."   (  "Aahaa,sasa dada Chuma,Mimi na baba yako wote ni wafanya kazi ,na asubuhi wote tunaondoka ,Mimi huwa narudi mida ya saa kumi,baba yako huwa anarudi saa kumi na moja na kuelekea. Watoto hawa wanasoma chekechea,huwa kuna gari mida ya saa moja linawapitiaga kwahiyo uhakikishe unawapikia asubuhi na mapema wale,waoge kisha uwaandae kwaajiri ya shule. Ukisiki honi ya gari unawatoa nje wapande gari la shule ,sawa Dada Chuma?"  "Sawa mama nimekuelewa."   "Nashukuru Kama umenielewa lakini pia ,unatakiwa inapofika saa Saba mchana una andaa chakula . Mambo mengine ni kujitahidi usafi wa mwili na mazingira ,sawa Chuma?" " Sawa mama nimekuelewa". Basi Kama umenielewa unaweza kwenda kuoga bafu ni  lile pale chumba Cha tatu pembeni na kinacho fuata ni choo."


Mama mwenye nyumba alinielekeza mambo mengi haswa majukumu ya kazi. Nikaingia chumbani kwangu nikabadirisha nguo,Kisha nikatoka nikiwa na kanga moja ambayo imenichora umbo langu la mwili haswa makalioni ambapo sio siri ,sijisifii  kweli Mungu amenibariki minyama ya makario. 

Nikakatiza pale sebureni ambapo alikaa baba mwenye. Nyumba na mkewe .  Nilijisahau nilijua kua bafu na choo vipo nje hivyo, nilitaka kutoka nje. " Wewe binti vipi! Mbona hivyo?" " Naenda kuoga mama!"   " Wewe si nilikwambia kua bafu na choo vipo chumba Cha tatu pembeni? Sasa huko nje unaenda wapi!  Au umeshazoea huko kwenu vijijini milimani huko?

" Nilijisahau tu mama samahani!"  " Sawa Chuma tumekuelewa  nenda tu kaoge mama!!"  

Aliongea mzee Foya huku akinitazama kwelikweli. Basi nikageuka na kuelekea huko bafuni . " We baba Maria vipi? Mbona unamtazama Sana yule binti kwa nini?" 

Nilimsikia mama mwenye nyumba akimsema mmewe kua alikua akinishangaa Sana. Nafikiri ni kwa sababu ya ile kanga niliyovaa na umbo langu ,lilimpa shida Sana.

 Basi nikaelekea bafuni ,ile nafungua mlango tu!

Namwona bibi yuko kule bafuni,kiukweli nilishtuka Sana ,ilibaki kidogo tu ,nipige kelele.

" Tulia Chuma, nimekuja tu kuona unapokaa ,ni pazuri Sana, nafikiri tutaonana baadae ,mida ya kazi,kuna kazi ya kufanya leo". "sawa bibi" 

 Bibi alitoweka Kisha nami nilioga na kuondoka chumbani kwangu.

Ile naingia chumbani tu! Nakuta kioo kipo kitandani kwangu. Kioo hiko hakikua kigeni kwangu kwani nilikitambua vizuri tu ,kua ndio kile alichonipa Bibi na nilikiweka kwenye begi langu ,Sasa sijui kilitoka vipi kukaa pale kitandani.!! Nikakisogelea Kisha nikakitazama ,nilichokiona ni tofauti na nilicho kitarajia! Nilijua nitajiona Mimi mwenyewe,lakini, huwezi amini,nilimwona Bibi zubeda wa kule kwetu morogoro, ambae ana undugu na mzee Foya, na mzee Foya ndipo alipofikia  kwa Bibi zubeda ambapo siku moja kabla ya kuja huku dar tulienda na Bibi kumwangia mzee Foya na ndipo nilipo kwama kwenye tumbo la mzee Foya.

Sasa tuachane na hayo,turudi pale ndani chumbani kwangu ,nilizidi kukitazama  kile kioo,nikamwona Bibi zubeda akiniteta na jirani yetu mmoja wa kulekule nyumbani . Huyo jirani alikua anaitwa mama majuto ,alimpelekea umbea Bibi zubeda kua eti Mimi na Bibi yangu ni wachawi Sana na pia ikiwezekana, wamwambie mzee Foya kua Mimi ni mchawi anifukuze. Kama nilivyo eleza hapo  mwanzo kua ,kioo ni msaada mkubwa Sana kwa wachawi,nimeweza kumwona Bibi zubeda kwenye kioo changu Cha kichawi kwa sababu yule Bibi zubeda na mwenzake walikua wakizungumza sehemu ambayo kulikua na kioo kilichokua wazi yani hakikufunikwa. Kwa hiyo kwetu sisi inakua ni Kama CCTV camera.

  

Basi baada ya hapo Sura ya Bibi zubeda na mwenzake zikapotea Kisha ikaja sura ya mkuu wetu wa uchawi, mkuu alinikazia macho Kisha akasema ," Chuma nadhani unajua Cha kufanya" Kisha mkuu akapotea. 

Nikamwita Bibi zubeda kwenye kioo akatokea tena. Nikachukua begi langu Kisha nikatoa mdori wa kike, nikaanza kuukaba kwenye shingo ule mdori huku nikinuiza maneno ya ufundi. Mara nikaanza kumwona Bibi zubeda kwenye Koo akijishika shingo huku akitoa macho ,kuhashiria maumivu makari. Alihangaika mpaka alianguka chini ,huku Mimi nikiwa bado naendelea kumkaba yule mdori ,mwishoni nikamnyonga shingo ya Yule mdori ,na Bibi Zubeda nae alijinyoosha palepale. Yani nimuua kabisa asije akaniharibia kwa bosi wangu Foya.

  Nikachukua kile kioo na kukirudisha kwenye begi, nikikabadili nguo Kisha nikatulia kitandani. Mara nikasikia mama Maria yani mama mwenye nyumba ananiita, " Chuma , Chuma toka uje tule " kumbe mama alikua amesha pika ,nikatoka kuelekea sebuleni, ile nafika tu sebuleni, mara namwona ..................................

      

        ITAENDELEA.................

Je, Chuma ameona nini pale sebuleni? Usikose sehemu ya 6 . Uhondo ndio kwanza unaanza ukiwa na maarifa kibao. Mambo mengi muda mchache.Mungu akijaaria tutakutana tena sehemu ijayo.Asante.

URITHI wa Bibi 4

 Story : URITHI WA BIBI . EP.4


Author........... Steven Morgan


📞 : .............+255 659 115 223


Email : ................. stevennemes2k@gmail.com


Karibu tena ndugu msomaji katika mwendelezo wa story yetu. Tulipoishia ndipo tunapo anzia .


ILIPOISHIA.

Binti chuma na wenzake  wakiwa msituni waki hapishwa na mkuu wa wachawi.


Basi,mvua ikaendelea kunyesha na jua likaendelea kuwaka ,mara ghafla mvua ikakata na likabakia jua Kama mwanzo. Mkuu wa wachawi akatupongeza na kusema kua Sasa tunatakiwa  kuusumbua ulimwengu. Natumaini mtakua mawakala wazuri Sana wa shetani katika kuleta ubovu ulio kidhiri katika Dunia . Mbarikiwe Sana na lusifa ,na mkafanikiwe katika kutenda dhambi zenu zilizobarikiwa na shetani". 

 Mkuu alipomaliza kusema hayo Mimi nikajihisi mwenye nguvu Sana na nikajikuta naweza kufikiria na kufanya mambo makubwa bila ya kufundishwa. Macho yaliniwiva kama nyanya ya utunguja. Mkuu alinitazama Kisha akasema " Chuma ,wewe unaonekana kua na nguvu nyingi sana ,kafanye kazi ,jamii ikutambue na kukuogopa ,hakuna kiumbe atakae weza kukudondosha , ulimwengu ni wako chuma , chochote unaweza kufanya kuanzia Sasa,umesha pewa nguvu ya mamlaka!"  Hayo yalikua maneno ya mkuu akinisifu,baada ya hapo tukanyanyuka na kurudi nyumbani baada ya kuruhusiwa na mkuu.


                      ENDELEA.

Kwakua ilishafika jioni Sana ya saa kumi na mbili ,Mimi na bibi tulishilikiana kupika  chakula Cha jioni kwa haraka Kisha ilipofika saa mbili kamili usiku ,tukaandaa chakula na kuanza kula huku maongezi ya hapa na pale yakiendelea.

Siku ikaisha hatimaye asubuhi ikafikia ,Kama kawaida nikaamka na kufagia uwanja  ,nikaanda chai na maji ya Moto ya kuoga.  Bibi alipoamka alienda kuoga baada ya Mimi kumaliza. Baada ya hapo tukatandika mkeka wetu nje na kuketi kwa ajili ya kunywa chai. 

"Chuma mjukuu wangu,kwa Sasa umeshakua kamili tena una nguvu nyingi zaidi yangu. Sasa ni Wakati wako wa kutamba unavyo taka"

Natamba kivipi bibi?"  "Kwa nguvu ulizonazo unaweza ukafanya chochote na kupata chochote unachokitaka,kwa mfano Kama kuna mtu unamchukia unataka kumfanya vibaya awe kichaa au awe na mikosi au maradhi, unaweza fanya."  "Sawa Bibi hayo uyasemayo Kama yanawezekana nitayatenda maana kuna watu nawachukia Sana."  Hayo yalikua ni maongezi ya hapa na pale Kati ya Chuma na Bibi yake,  Chuma anaendelea kueleza ...tukiwa bado tupo pale nje tukinywa chai mara akaja mtu mmoja wa kiume ni mbaba kwakua alikua  ni mtu mzima . " Hodi hodi wenyewe hapa!!"  " Karibu " tukamjibu yule mbaba kwa pamoja. " Bila Shaka hapa ndio kwa bibi Mbokeleni au kwa bibi chuma?" Aliuliza yule mgeni tusie mfahamu. " Ndio bila Shaka umefika Mimi ndio Bibi Mbokeleni na huyu ndio mjukuu wangu Chuma" Bibi alimjibu yule mgeni. " Nashukuru kuwafahamu! Bila Shaka hamnifahamu ,Mimi naitwa Foya ni mwenyeji wa moshi lakini kwa Sasa makazi yangu naishi Dares salaam.Kuja hapa nimeelekezwa na ndugu yangu mmoja ambaye ni mwenyeji wa hapa Ndolelo anaitwa Bibi zubeda anaishi hapo ng'ambo ya pili" " aaah! Bibi zubeda namfahamu  vizuri,Sasa nambie shida yako ni nini?" Bibi alimjibu yule mgeni. " Shida yangu nilikua nahitaji binti wa kunifanyia kazi za ndani,nipo Mimi,mke wangu na wanangu wawili wadogo wa kike na wa kiume . Sasa nimeambiwa kua kuna binti anaitwa chuma unae hapa ,ndo maana nimekuja kukuomba Kama itawezekana niende nae dar es salaam akanifanyie kazi." Yule baba mgeni alijieleza Wakati huo wote Mimi nilikua nipo kimya nikisikilizia kinachoendelea Kati ya Bibi na yule mgeni. " Sasa wewe umetoka huko kote umepaona hapa ndio kwenye mfanyakazi?" " Nimekuja hapa kwakua nime elekezwa raha sivyo, nisinge fika,nisamehe lakini Kama nimefanya kosa kuja hapa"  " ha ha ha haaa! wewe huna kosa ila kosa analo aliekuelekeza kuja hapa!, Sasa je, utaweza kwenda kuishi na mjukuu wangu kweli huko dar es salaam?, " Bila Shaka Bibi ,Kama Chuma mwenyewe atakubari, basi hakuna kitakacho shindikana ,ataishi vizuri Sana atakua Kama yupo nyumbani"  " sawa ,Mimi Kama bibi na Kama ndio mzazi wa Chuma,sina neno tena labda tumsikia mwenyewe Chuma anasemaje kuhusu hilo? Maana nae pia ana maamuzi yakepia"  Bibi alimalizana na yule mgeni kisha bibi alinigeukia na kuniuliza ," Chuma nadhani umesikia mazungumzo yote hapa ,Sasa je,upo tayari kwenda dar es salaam kufanya kazi?  " Bibi Mimi bana  sitaki niende mbali nikuache wewe peke yako,siwezi kuishi mbali nawe"  " Chuma kumbuka wewe umeshajitambua na unaendelea kua mtu mzima ,kumbuka sasa unatakiwa kujitafutia maisha yako mwenyewe ,naamini ukifanikiwa unanikumbuka na Mimi Bibi yako kwa kuninunulia upande wa kitenge na kaniki na sukari utaniletea au we unasemaje?" Bibi alinig'ang'ania Sana Mimi kukubari kwenda kufanya kazi dar es salaam,sijui kwa nini! Lakini nahisi alikua na maana yake. " Sawa bibi kwakua wewe umekubari Mimi niende ,siwezi tena kupinga,niko tayari ila nataka nijui kwanza nitalipwa shilingi ngapi?

"Nashukuru Sana Bibi, pia nakushukuru Sana Chuma. Kwa kukubali kwendakufanya kazi kwangu, mshahara nitakulipa shilingi elfu kumi, na ukifanya kazi vizuri nitakuongeza!!"  Aliongea yule mgeni alie jitambulisha kwa jina la Foya ndugu na Bibi Zubeda. Basi kwa kua ilikua  asubuhi ya alhamisi ,bibi alimwambia  yule mzee Foya kua aje juma tatu kunichukua . Mzee Foya alifurahi Sana bila kujua kua anamkaribisha shetani alietoka depo. Alituaga Kisha akasema kua atakuja juma tatu asubuhi kunichukua na tutaianza safari asubuhi hiyo hiyo.

Bibi alifurahi Sana na akaniambia kua " Sasa Chuma huko unakokwenda ndio pa kujikomaza mjukuu wangu sawa?"  " Sawa bibi kwa Sasa huna haja ya kunielekeza najua nini cha kufanya. Watamjua chuma kua ni mtu wa aina gani!!


Story ................ URITHI WA BIBI EP. 4.B

Author..............Steven Morgan

📞..................... +255 659 115 223


Kwa mara nyingine tena bado tupo sehemu ya 4 ya story yetu ambapo tunaingia katika kipengele B ya sehemu ya 4. Kabla hatuja endelea katika kipengele B,ngoja tukumbushane kidogo yaliyopita katika kipengele Cha 4.A.


ILIPOISHIA,

Tumeona kua Bibi Mbokeleni au Bibi chuma amepata ugeni wa baba mmoja asubuhi na mapema ambaye alijitambulisha kwa jina la Foya . Mzee Foya alikua anahitaji mfanyakazi wa ndani ili aondoke nae Dares salaam ,ambako ndiko anako ishi yeye na  familia yake ,akiwemo mkewe na watoto wawili wadogo.Binti chuma ndio mlengwa anae hitajika kwenda huko dares salaam kufanya kazi. Kumbuka binti chuma siku si nyingi ametoka kufuzu depo la kichawi na kuhapishwa. Bibi yake amemruhusu chuma aende akafanye kazi. Mzee Foya ameambiwa aje juma tatu kumchukua binti chuma ili aondoke nae dar es salaam. 

 

ENDELEA.

Bibi alifurahi Sana Mimi kupata kazi ,japo Mimi sikupenda kua mbali na bibi yangu maana yeye ni Kama mzazi wangu alie bakia katika Dunia hii.

Lakini kwakua bibi ameridhia ,basi Mimi pia siwezi kumpinga kwani bibi alitaka na Mimi pia nijitafutie maisha yangu ili baadae nikifanikiwa ,nimsaidie na yeye.

 Kama wasemavyo waswahili kua usiku wa deni haukawii kucha,basi siku zilikwenda Sana na juma pili ikafika ,ambapo nilijiandaa vya kutosha,nilifungasha kila kilicho changu kwaajili ya safari ya dar es salaam. Usiku ukaingia,Bibi aliniita katika chumba chake Kisha akanipa kioo Cha pembe nne ,akaniambia nikitunze maisha yangu yote,na yeyote ninaye mtaka kumwona nimwite kwa jina lake nitamwona pale kwent kioo.

Ndugu msomaji,kioo kina maajabu mengi usiyo yajua ambayo unaweza ukafanya hata wewe ambae sio mchawi!! Nitakwambia hajabu moja wapo la kioo unacho jitazamiaga nyumbani kwako. Baadhi ya watu ukiingia vyumbani mwao,utakuta vioo vya kujitazamia ,vimefunikwa kwa nguo au boksi au karatasi kubwa na vitafunuliwa Wakati mtu anapotaka kujitazamia tu!!

Huwa wanavifunika kwa sababu,vioo hutumika Kama CCTV Camera ya wachawi,na huona na kusikia chochote mnacho ongea au kuteta mkiwa ndani huku vioo vya kujitazamia vikiwa wazi. Ndugu msomaji unashauriwa kufunika kioo chako Cha kujitazama na ukifunue pale unapotaka kukitumia tu!!, Kwani unapo viacha wazi muda wote ,wachawi watajua kila kitu kinacho endelea ndani mwako.

Hajabu lingine lakioo,nikwamba kwa kupitia kioo unaweza kumwita jini yeyote akaja na unaweza kuzungumza nae kwa kupitia kioo chako Cha kujitazama. Unacho takiwa kufanya hapa ,ni kuchukua kioo chako Cha ukubwa wa kutosha wa pembe nne Kisha jifungie ndani mwako,hakikisha hakuna kelele Kisha chukua kioo chako kiweke mbele ,mezani ,ukutani au Kama kipo kwenye dressing table yako ni vizuri zidi.simama mbele ya kioo chako Kisha kitazame kioo chako bila kubwenza kwa dakika kadhaa huku katika akili yako fikiria kua kuna jini au kiumbe Cha hajabu utamwona!! Kisha  taratibu utaanza kuona sura yako inabadirika na kua sura mbaya ya kutisha ,ukiona hari hiyo inajitokeza ,ujue jini ameshafika ,unachotakiwa kufanya Sasa ni kumwomba unachokitaka akutendee. Angalizo : usije ukafanya zoezi hili Kama wew ni mwoga ndugu msomaji,kwani inatisha mno. Na usije ukafanya zoezi hili usiku,ni hatari Sana.


Basi nikiwa bado nipo chumbani na Bibi huku nikikiweka kioo alicho nipa kwenye begi langu la kusafiria. Baada ya happy kwakua ilikua tayari ni usiku Sana ,tukatoka nje kichawi,yani tulitoka bila ya kufungua milango,moja kwa moja tulienda kwa Bibi zubeda ambae yule mgeni Foya ndipo alipo fikia,ilikua ni usiku Sana ,wote ndani walishalala fofofo, Mimi na Bibi tuliruka na kutua kwenye paa la nyumba la Bibi zubeda.Tulipotua juu ya bati,hapakua na kelele wala kishindo zaidi Kama aliekua ndani Kama hajalala basi anaweza akasikia Kama mchanga au vimawe mawe vinamiminika kwenye bati!! 

Ndugu msomaji ukisikia Hari hiyo,ujue wanga wamesha tua na Kama hujalala basi utalala kwa lazima .unachotakiwa kufanya baada ya kuona Hari hiyo ni kumwomba Mungu Sana akunusuru na ibirisi huyo.

Basi tukatua kwenye lile bati la bibi zubeda ,japo bati zake zili oza lakini hatuwezi kuanguka kwani tunakuaga wepesi sana . Tulimwaga madawa yetu ili asie lala kwa muda huo ,alale kwa lazima ili sisi tuendelee na kazi yetu.

Tulitazama kwa kupitia jicho la tatu la kichawi tulimwona yule bosi Foya anaye taka kesho juma tatu twende wote dares salaam amelala fofofo huku simu yake ya tachi ikiwa chini. Tulirukaruka huko juu ya bati huku tukiimba nyimbo za kichawi kwa sauti. Hata Kama hujalala huwezi kutusikia. zaidi, utahisi wimbo flani unao ufahamu ume play katika kichwa chako ,ukiona hivyo ujue wazee wa kiza wapo nje au ndani wanacheza na kuimba.   Basi tukacheza Sana Mimi na Bibi baadae  tukaingia ndani chumbani kwa yule mgeni Foya . Taa ilikua inawaka tukaizima  Kisha tukaanza kumsotea kwa makalio ,muda mwingine tulimjambia mdomoni akawa anashtuka na kukohoa  sana. Bibi aliniambia kua nimkalie tumboni kwa makalio yangu Kisha nimsotee sotee !! Nami nikafanya hivyo tena kwa haraka . Lakini ghafla yule mzee Foya alishtuka usingizini kwa haraka na akanikamata nikiwa palepale juu ya tumbo lake!!! Huwezi amini Bibi aliondoka na kuniacha nimekwama juu ya tumbo la mzee Foya ambae ni bosi wangu mtarajiwa  huku nikiwa uchi wa mnyama na makalio yangu makubwa yaliyojaziana minyama yakiwa juu ya tumbo la mzee Foya.

******* ***** ITAENDELEA ************

 JE,nini kitafuatia?

Mzee Foya atamtambua binti Chuma?

Je,safari ya dar es salaam ipo?

 Hayo na mengine mengi utayajua katika sehemu ya EP. 5 ya URITHI WA BIBI


USISAHAU KU LIKE , COMMEnt


URITHI wa Bibi 3

 Story :.................... URITHI WA BIBI . EP.3


Author................... Steven Morgan


📞 : .......................+255 659 115 223


Email : ................. stevennemes2k@gmail.com


Karibu tena ndugu msomaji katika mwendelezo wa story yetu.Kabla ya kusonga mbele, ngoja tukumbushane kidogo..

TULIPOISHIA:

Ndugu msomaji, sehemu iliyopita tumeona kua chuma mashaka na bibi yake mbokeleni,wakiwa kwenye harakati za kishirikina za kuruka kwa usafiri wa  air kibeku aina ya " ungo natural air plane" ambayo safari yao iliwapeleka mpaka Nairobi Kenya. Ambako huko ,mambo yaliwaendea hovyo,walipokatiza kwenye anga la kanisa moja la Kenya Assemblies of God . Ambapo wali anguka na ndege yao kwenye uwanja wa kanisa nyakati hizo za usiku,ila bibi alifanikiwa kukimbia na kumwacha mjukuu wake Chuma akiwa amekwama.Ambapo baadae alikuja kuokolewa na mmama mmoja mchawi wa hukohuko Kenya na kutoweka nae.Chuma akiwa kwenye mikono ya yule mama mwenyeji wa kenya mambo ya kichawi yaliendelea Kama kawaida.Kwani tumeona kua chuma kwakua alikua na njaa aliweza kula supu ya kichawi yani supu ya nyama ya mtu ikiwa na mchuzi mwingi wa damu.Majanga kwa chuma yaliendelea ambapo walipata misukosuko pia walipokwenda kuwachawia watu mtaani. Mwishoni tuliona Chuma akinusurika kubakwa akiwa amekwama kwenye nyumba ya kijana mmoja huku yule mama akiwa amekimbia na kumwacha na alipojipanga tena ,alirudi kumwokoa tena Chuma .Ambapo baaadae kwa kutumia usafiri wa ndege ya kichawi aina ya "fagio natural Air Plane" , Chuma akiwa na yule mama bila kupoteza muda walisafiri kwa haraka na kuwasiri nchini Tanzania nyumbani kwa kina chuma.Ambapo walimkuta bibi yake na chuma akiwasubiri ,kisha baada ya chuma kupokelewa na bibi yake,yule mmama mchawi wa Kenya akaondoka zake bila kusubiri. 


ENDELEA..

 Bibi alinipokea usiku ule ,kwakua nilichoka Sana sikuweza kuongea mengi bali nili muomba bibi niende nikalale afu mambo mengine tutazungumza asubuhi. Bibi aliniruhusu Kisha nikaenda chumbani kwangu kulala . Nilipokuja kushtuka ilikua tayari kumesha kucha,kwani nilisikia ndege wakilia huku nje bibi aliendelea kufagia uwanja. Niliamka na kuchukua ndoo yenye maji ya kuoga ya baridi ,nikaenda kuyaoga ili niondoe uchovu. Kiukweli nilichoka Sana tena Sana!!  Nilipomaliza kuoga , tayari bibi alisha ivisha chai na futari yenye mchanganyiko wa magimbi,miogo ,ndizi na vigonzo. Futari iliungwa kwa nazi . Bibi alitandika jamvi dogo na aliandaa chai Kisha wote tukaketi jamvini na kunywa chai kwa pamoja. "Pole Sana mjukuu wangu ndio ukubwa huo".  " Asante bibi ila namshukuru Sana mungu ameniepusha na mengi".    " Mh! Mungu tena katokea wapi? Wewe umshukuru tu yule mama mchawi wa Kenya ,ndie alie kusaidia sana."   "Nikweli bibi napaswa pia kumshukuru yule mama mungu ambariki Sana."  

"Mungu ambariki kwa kazi gani nzuri aliyoifanya? Hebu wacha kumtaja taja huyo mungu wako kwenye haya mambo!"


"Sawa bibi ila hii kazi Mimi siitaki tena !"


"Wee! Tena funga huo mdomo wako,hivyo unavyosema wiki hii tu! Natakiwa nikukabidhi mikoba rasmi ,na wala huwezi kupinga wamesha kuchagua wakubwa, hahaha haahaa haahaa!" 


Kiukweli mtoto wa nyoka ni nyoka , sikuweza kulipinga hilo . Sijui bibi aliniroga!! Maana siku zilikwenda hatimaye wiki ikafikia ,alilolisema bibi ndilo lililokua . Na kiukweli sikuweza kupinga . Nakumbuka ilikua siku ya juma nne nyakati za usiku sana,waswahili wanaita mida ya wanga! Tukiwa nyumbani ,bibi alinipaka dawa na kunichanja chale nyingi za kichawi mwilini na kunielekeza baadhi ya mambo makubwa. Kisha baada ya hapo ,tukaenda kwenye sherehe ya kukaribishwa mwanachama mpya wa kichawi. Tukaenda kwa kuruka kwa kupiga guu la kushoto chini na kupotea kwa ghafla Kisha tukaenda kutokea kwenye uwanja wa mpira wa miguu,ukiwa umefurika watu kibao ,wakubwa kwa watoto ,vijana kwa wazee!! Uwanja huo pembeni kuna makaburi mengi sana . Kiukweli niliogopa Sana ! Japo Mimi mwenyewe nilikua natisha ukinitazama lakini,na Mimi pia niliwaogopa wenzangu nilipo watazama ! Walikua wanatisha Sana.!

Uwanja huo siku ufahamu kwa haraka kwani sikua mtu wa kutembea tembea sana maeneo.

Basi kwakua watu walijaa Sana uwanjani,na sisi pia tukatafuta siti na kuketi. Tukawa tuna sikiliza kinacho zungumzwa na mkuu pale katikati ya uwanja.    " Karibuni Sana wanachama wenzangu,katika utangulizi wa  sherehe yetu ya kuwakaribisha wanachama wapya katika utawala wetu" 

Watu walishangilia Sana kwa sauti zenye milio tofauti za wanyama ,yani wengine walilia Kama paka , wengine Kama farasi ,Simba ,bundi yani kila mtu alikua na mlio wake ! Niliogopa Sana kwani hata bibi nilie kaa karibu nae ,pia nae alishangilia kwa kulia Kama paka shume " nng'aaaaaaaaaauuuuuuuuuuu!" 

Haisee! Muda mwingine nilitamani hata kumkimbia bibi lakini sikua na jeuri hiyo.


" Bila kupoteza muda,tunawaomba watu wafuatao waje hapa kati, aje binti nuru,aje kijana Lazaki,aje binti Chuma,pia aje na mwana dada Maria ."

  Nilishtuka sana nilipo lisikia jina langu lakini Cha kushangaza nilijikuta nakwenda pale kati bila mwenyewe kujielewa . Wote tulio tajwa tulienda pale katikati ya uwanja kwa mkuu ambae alionekana kutisha zaidi ya wengine. Mkuu akanyosha msinga wenye manyoya ya mnyama was hajabu Kisha akatupiga piga nao usoni Kisha akanyosha mkono wa kushoto likaja kapo kubwa lililojaa vibuyu tofauti tofauti. Akatoa dawa ya mgando katika kila kibuyu akazichanganya Kisha akatuchanja chale za kutosha na kutupaka ile dawa .Alipo maliza akasema karibuni Sana ,nasi nasi kwa pamoja tukajibu  Asante sana mkuu.


" Ndugu zangu Sasa mmekua mafundi,hakuna mtu wa kuwasumbua duniani hapa ,labda mbinguni! Zoezi la kuwapa mikoba limekwisha,kilichobakia ni kuwaapisha ambapo zoezi hilo litafanyika kesho juma tano kuanzia saa kumi jioni.Leo tutashangilia kwa pamoja kwa kuimba na kucheza pia tutakula na kunywa.hivyo kila kamati ijiandae kwa majukumu yake . Kamati ya mapishi naomba mchangamshe mikono Wakati tunaendelea kuburudika kwa ngoma na kucheza baada ya hapo tunataka kula "

 

Mkuu aliongea hivyo Kisha ngoma zikaanza kupigwa lakini nilishangaa Sana baada ya kuona ngoma zinazopigwa haziku ngoma Kama unavyo fikiria,bali walikua watu wakipigwa vichwa na wengine walipigwa makalio na kutoa mlio Kama ngoma iliyo wambwa kwa ngozi!!

Tulicheza Sana kwa kuimba kwa sauti kubwa yani endapo watu wangetusikia majumbani basi ni lazima wangetoka kututazama.

Mkuu alinyoosha msinga wake juu ,ngoma ikazima na wale watu waliofanywa kua ngoma walionekana kuchoka Sana. Mkuu aliwanyoshea msinga wake ,wale watu wakatoweka!!

Sijui walipokwenda ila nafikiri walirudishwa makwao.

    

"Ndugu washirika wenzangu,baada ya kucheza vya kutosha ,na kuimba vya kutosha ,Sasa ni muda muhimu wa kula chakula chetu pendwa . Chakula kipo tayari ,bakia hapo hapo ulipo utaletewa chakula chako" 

Mkuu baada ya kumaliza maneno hayo,mara watu wa hajabu wakaanza kugawa chakula kwenye mabakuli makubwa Sana yakiwa yamejaa mapande makubwa ya nyama huku yakiwa na mchuzi mwekundu wa kutosha. Chakula kiligawiwa kwa haraka ,muda huo sisi pia tukiwa katikati ya uwanja Kama wanawali,pia tuliletewa msosi wetu kwenye mabakuli makubwa . Tukala na kunywa bila kuhofia msosi ulikua mtamu Sana kwani ulikua unafanana kabisa na utamu wa supu niliyo kunywa kule Kenya. Nilikunywa na kula bila hofu kwani niliufurahia msosi ule, kiukweli ilikua ni damu mbichi ya mtu pamoja na minyama nyama ya mwili wa mwana damu.


Tulipomaliza kula na kunywa mkuu akasimama na kutupongeza wote tuliojiunga na uchawi siku hiyo na kusema kua kesho juma tano tusisahau ,saa kumi kamili jioni tukutane kwenye pori la kusimikwa .


"Ndugu zangu sherehe yetu imeisha ,ila kesho juma tano chonde Sana,walengwa wote tukutane kwenye pori la kusimikwa kwa haraka kwa muda uliotajwa, kwa Sasa hakuna Cha zaidi ,kusanya kilichochako kila mtu arudi nyumbani ila msikose kuwanga japo nyumba moja kabla hamjaenda kulala makwenu"


"Sawa mkuu" watu wote tuliitikia kwa pamoja Kisha tukapiga miguu chini na kutoweka kwa ghafla .Mimi na bibi tukakutana kwenye njia panda moja karibu na makazi ya watu ,ikiwa kunakaribia kupambazuka kabisa,bila hofu tuliingia kwenye nyumba moja ya mchungaji Boniface ,tuliwanga kwa kusota sota kwa makalio kuanzia sebuleni mpaka vyumbani walimo lala. Kiukweli mchungaji Boniface alikua mwepesi Sana ,alikua anamwongopea mungu hakua mchungaji kweli alikua tapeli yani ni nabii wa uwongo. Tulimchezea Sana mwisho tulimbeba na kumlaza nje ya nyumba yake Kisha sisi tukaondoka zetu nyumbani. Tukalala kidogo asubuhi na mapema ikawadia . Bibi aliniambia kua nijiandae mapema kwani saa kumi kamili inatakiwa niondoke ili nikasimikwe.


Siku hiyo nilichoka kiasi nikaenda kuoga Kisha nika andaa chai Kama kawaida Mimi na Bibi yangu tukanywa huku story nyingine zikiendelea. Muda ulisonga mbele hatimaye saa kumi kasoro dakika tano,nilishtuka bibi akiniamsha kumbe nilipitiwa na usingizi,Bibi alishapika Cha mchana Lakini sijala tukaingia ndani na kuvaa mavazi yetu ya kazi. Tukapiga miguu chini na kuibukia kwenye msitu mkubwa ambapo tuliwakuta wenzetu walishafika nilikua nasubiriwa Mimi tu!

 

"Afadhari bibi mbokeleni na chuma kwa kufika maaana mlikua mnatuchelewesha"

Aliongea mkuu mwenye sura ya kutisha.

"Bila ya kupoteza muda walengwa wote njoeni mkae chini ya mti huu" ulikua ni mti mkubwa sana ,tulikaa pale chini tukiwa uchi ,mkuu alitambika kwa lugha yake tusio ielewa ,mara ghafla ikanyesha mvu kubwa japo kulikua na jua kari la saa kumi.Yani kulikua na mvua na jua kwa pamoja. Waswahili wanasemaga eti,simba anazaa!!!!  Dhana hii imeenea Sana mtaani kwamba jua likiwaka na mvua ikinyesha kwa pamoja eti,Simba ana zaa, ukweli ni kwamba ukiona jua linawaka na mvua inanyesha kwa pamoja, ujue kuna wachawi wapya wana hapishwa na wamekubariwa kupokea nguvu kutoka kwa shetani wa kichawi.


Basi,mvua ikaendelea kunyesha na jua likaendelea kuwaka ,mara ghafla mvua ikakata na likabakia jua Kama kawaida. Mkuu wetu alicheka Sana , akasema kwamba " vijana wangu mmepokea nguvu kubwa Sana za kuusumbua ulimwengu, natumaini mtakua mawakala wazuri Sana wa shetani katika kuleta ubovu ulio kidhiri katika Dunia . Mbarikiwe Sana na lusifa ,na mkafanikiwe katika kutenda dhambi zenu zilizobarikiwa na shetani". 

 Mkuu alipomaliza kusema hayo Mimi nikajihisi mwenye nguvu Sana na nikajikuta naweza kufikiria na kufanya mambo makubwa bila ya kufundishwa. Macho yaliniwiva kama nyanya ya utunguja. Mkuu alinitazama Kisha akasema " Chuma ,wewe unaonekana kua na nguvu nyingi sana ,kafanye kazi ,jamii ikutambue na kukuogopa ,hakuna kiumbe atakae weza kukudondosha , ulimwengu ni wako chuma , chochote unaweza kufanya kuanzia Sasa,umesha pewa nguvu ya mamlaka!"  Hayo yalikua maneno ya mkuu akinisifu,baada ya hapo tukanyanyuka na kurudi nyumbani baada ya kuruhusiwa na mkuu.

********************************************

                      ITAENDELEA.


JE,nini kitafuatia? Sasa chuma amesha kua kamili ,unafikiri nini kitaendelea? Usikose kufuatilia sehemu ya 4,ya URITHI WA BIBI. UHONDO NDIO KWANZA UNAANZA. Fanya ku LIKE PAGE, NA KU SHARE,Ili wengine waone na kuburudika.

URITHI wa Bibi 2

 story : URITHI WA BIBI. EP.2

 ( Grandmother's inheritance.Ep.2)

Author :  Steven Morgan

Email : stevennemes2k@gmail.com


Kabla hatujaendelea ngoja tukumbushane kidogo pale tulipoishia.

Ndugu msomaji tumeona jinsi binti chuma mashaka anavyo fundishwa jinsi ya kuendesha aina za ndege za kichawi .Tumeona kati ya mifagio miwili, mkubwa wa nje wa chelewa na mdogo wa ndani wa ukindu pamoja na ungo, vyote vikiwa ni aina za usafiri wa kichawi.Tumeona bibi yake na chuma amechukua ungo na kuweka manjonjo yake kisha kwa pamoja na mjukuu wake chuma walianza kuyakata mawingu kwa raha zao! Lakini baadae bibi aliamua kumpeleka mjukuu wake kenya ,kwa  usafiri wa ungo ,lakini mambo yalikua mabaya kwani baada ya kufika kwenye anga la kanisa moja la kiroho mjini Nairobi, ndege yao iliyumba na wote walishuka chini kwa kasi pamoja na ungo wao.!! Lakini bibi ghafla alipaa juu na kutoweka kabisa maeneo yale ,alibakia mjukuu wake Chuma ambae ndio siku  yake ya kwanza katika shughuri za uchawi.Masikini chuma amebakia yeye mwenyewe akiwa uchi wa mnyama pamoja na ungo wake asijue cha kufanya ndani ya uwanja wa kanisa la kiroho.Ikiwa ni bado usiku sana chuma akatulia akisubiri asubuhi ifike ili azijue mbivu na mbichi.

Nini kiliendelea? Chuma anaendelea kusimulia  Endelea nayo.


Nikiwa bado nipo nje ya kanisa la kiroho nikihangaika,lakini hakuna nilicho kifanya zaidi ya kubakia palepale ,nililitazama lile kanisa, kwa juu lilikua limeandikwa (Kenya assemblies of God - Buruburu). Usiku ule wote ukaniishia mimi yani kama waswahili wanavyosemaga kua ,usiku wa deni haukawii kucha (the night of debt does not last long), ndivyo ilivyokua ,asubuhi ikafika ,maana nilianza kusikia sauti za ndege wakilia na majogoo yakiwika.Lakini kuna sauti nilikua nikiisikia ikipenya masikioni mwangu kama sauti ya bibi! Ikiniambia "chuma ili upate msaada ,inakupasa ulale kifudifudi muda wote yani ulalie tumbo,kinyume na hapo utaumbuka,zingatia hilo sasa" sauti hii ilikua ikijirudia rudia mpaka masikio yalikua yanauma . Kulizidi kupambazuka na kua kweupe,!! Ghafla nikasikia mayowe mtu akiita "jamani mje mjionee maajabu,mchawi amenasa hapa kanisani!!" Nilishtuka sana,kumbe alikua ni mlinzi wa kanisa tayari ameshaniona!! Haraka nikalala kifudifudi huku furushi langu la makalio yakiwa juu na ungo ukiwa pembeni.Watu walijaa sana,kila mtu alisema lake huku mwingine nilimsikia akisema "jamani afu mchawi mwenyewe ni binti mdogo sana,bado mwali alafu ana umbo zuri!!"

Sikuyajari maneno yao ,mimi niliendelea kulala kifudifudi huku watu wakiendelea kuyashangaa makalio yangu yalio chafuka kwa vumbi na maungaunga ya kichawi. Nilijisikia vibaya sana ila sikua na namna. Mara nikamsikia mtu akiongea na simu.."haloo mchungaji,wahi kanisani,kuna mchawi mtoto ameanguka"  Nilishtuka tena kwa presha baada ya kusikia kua mchungaji anakuja!! Niliona sasa huo ndio mwisho wangu! Watu walizidi kujaa na mimi nilizidi kuduwaa huku nikiwa nimelala chali.

Huwezi amini ghafla nikamwona mmama mmoja akipenya kwenye ule umati wa watu na kunijia mimi huku akiwa uchi !! Bila shaka alikua haonekani na watu wengine zaidi yangu.sura yake ilikua ni ngeni kwangu ! Lakini akaja akaniezeka kibao kimoja cha makalio kisha akaniambia kua ninyanyuke tuondoke kwani hakuna mtu anaeniona kwa sasa!! Nikweli sikuonekana maana ghafla! Niliwasikia watu wakisema huku wakikimbia kua "ameyeyuka" "jamani ameyeyuka yeye na ungo wake!!"  Kiukweli sikuyeyuka bali,nilipotea kwenye macho yao kimiujiza baada ya yule mama kuja kunigusa na kuninyanyua.kiukweli yule mama alie nisaidia ,alikua ni mchawi wa kulekule kenya ! Ila amenisaidia kwa kunipa nguvu tena za kichawi .Ngoja nitoboe siri moja hapa,kwamba mchawi yeyote anapokwama sehemu,asipolala kifudifudi ,hawezi kupata msaada kutoka kwa washirika wenzake labda ajiokoe mwenyewe.

Basi watu wakawa wanatimka huku na kule huku na sisi taratibu tukaondoka kwa miguu mbali kidogo na kanisa nikiwa na yule mama,wote tukiwa uchi na kuto kuonekana (invisible). Yule mama aliniambia kua nisiogope ,kwani atanisaidia kurudi nyumbani Tanzania.Nikiwa nimeshika ungo wangu yule mama ,akanikumbatia ,ghafla tukapotea  nikaja kushtuka ,nikajikuta nipo ndani ya nyumba ya yule mama . "Itakubidi leo ushinde hapa kwangu mpaka usiku Ili niandae usafiri wa haraka kwaajiri yako."yalikua ni maneno ya yule mama nami,sikua na lakusema zaidi ya kumshukuru.yule mama hakutaka kunijua sana zaidi ya kutambua kua Mimi ni mshirika mwenzake. Ikawa hivyo ,nilishinda kutwa nzima kwa yule mama!! Mpaka giza likaingia ,ilikua ni usiku wa saa mbili, Kama kawaida yule mama aliingia ndani na kutoka na fagio kubwa la njelewa likiwa na mpini mrefu ."Binti unajua kuendesha usafiri huu?" Aliniuliza. "Hapana mama ,Mimi bado mgeni Sana kweye hayo mambo " nilimjibu.  " Sawa ,Sasa ngoja kwanza nikuandalie chakula Cha kichawi ,maana huwezi kunitembelea ,alafu uondoke bila kula hata supu." Nilishtuka sana .. "chakula Cha kichawi?" Nilimuuliza. " Ndio ,kwani hujawahi kula? Mbona unaonekana kua ni mgeni sana?" Aliniuliza.. "ni kweli mama yangu ,ndio kwanza siku yangu ya kwanza leo,bibi yangu alinibeba,hivyo Sijui mengi sana!!" Nilimjibu yule mama. Yule mama akacheka sana ,Kisha akaingia tena chumbani kwake na kutoka na bakuri kubwa la aluminium,likiwa limejaa nyama nisio ijua na mchuzi mwingi ila ulikua mwekundu sana.


"Kunywa na kula hizi nyama ,kutakufanya wewe uwe na nguvu nyingi,hebu kula kwanza alafu ntajua Cha kufanya!" Alinifosi kunywa ile supu,niligoma lakini akanifosi mpaka akaninywesha! Sio Siri ule mchuzi ulikua mtamu sana,japo ukiutazama ilionekana kua ni damu kabisa.sikua na jinsi ,kwakua nilikua na njaa Kali,nikala na zile nyama zote,nazo pia zilikua tamu sana ,yani utamu wake sijui nifananishe na mnyama gani!!! 

"Vizuri Sana binti, unaonekana ni muelewa Sana ,Sasa usafiri uko tayari lakini kabla hatujaondoka inatakiwa twende tukawachawie watu kwanza (kuwanga) ili kupata nguvu zaidi!"  Aliongea yule mama huku Mimi nikitikisa kichwa ,kama ishara ya kumkubalia.

Yule mama akiwa uchi kama mimi lakini ukimtazama alionekana Kama amevaa kaniki ,alinichukua nakutoka nje ya nyumba yake,akanishika mkono Kisha akapiga mguu chini kwa nguvu!! Ghafla tukajikuta tupo kwenye mitaa flani huko ulaiyani kwenye makazi ya watu. Tukaenda kwenye nyumba moja ambapo tulitua juu ya paa,kwakua ilikua mapema Kama usiku wa saa tatu hivi, wenye nyumba walikua bado hawajalala ila watoto zao baadhi walionekana wamelala vyumbani. Kwakutumia maneneo makali ya kiimani tuliweza kuingia ndani bila ya kufungua milango,tulifikia sebuleni ambako tulimkuta mtu na mke wake wakitazama sinema runingani.Tukaanza kuwazunguuka kwa kuwasoteasotea na makalio.Kuna muda Kama walikua wakihisi Kama kuna Jambo linatendeka! Lakini hawakua na uhakika .Nilimsikia yule mzee akimwambia mkewe .. "mbona nyumba imekua nzito ghafla? itakua kuna wachawi wameingia mke wangu,hebu niletee ile biblia yangu." Tuliposikia habari ya biblia tukashtuka automatic na kujikuta tupo nje juu ya paa, kule ndani walianza kufanya maombi mazito wakilitaja mara nyingi jina la Yesu na Mungu baba. Sio Siri tulipata tabu Sana , nikajihisi Kuungua mwili mzima ,yule mama akanishika mkono ,tukakimbia huku atua zetu zikisikika kwenye mabati ,tuliruka na kupaa Kama ndege na kwenda kutua barabarani. Asikudanganye mtu,neno la mungu ni kiboko ya wachawi haswa unapomtaja mara nyingi bwana yesu na Mungu baba,mchawi hawezi kukukalia karibu. 

Basi baada ya hapo tukaenda kwenye nyumba nyingine ambapo ile tunatua tu kwenye paa,tulihisi Kama tumekanyaga misumari ya Moto !! Haraka tena tukakimbia kwa kuruka juu na kutua mtaa wa pili!!   Nikaamua nimuulize yule mama kua inakuaje lile paa linaumiza namna ile? Akaniambia kua yule mwenye nyumba aliweka chumvi ya mawe batini ndio maana ilitupa shida.Hapa naomba nikufafanulie kidogo ndugu msomaji kuhusiana na chumvi ya mawe. Chumvi ya mawe ni ulinzi mkubwa sana wa nyumba yako Kama hutaki wachawi wakujie.Unaweza kuchukua chumvi kidogo ukanuiza na maneno kidogo alafu ukairusha batini ,hapo mchawi hawezi kuingia ndani,au ukachukua chumvi kidogo alafu ukaiweka kwenye kila pembe  au cona ya nyumba yako ,hapo pia mchawi hawezi kuingia wala kutoka .Au ukachukua chumvi ya mawe na kuiweka kwenye mvungu was kitanda unacho lalia ,hapo mchawi hata Kama ameingia ndani,lakini hatoweza kukusogelea au kukugusa.Huwezi amini lakini ukweli ndio huo ,Kama unasumbuliwa Sana na wachawi, fanya hivyo ,utalala vizuri sana bila kuchezewa.Kama uhamini ngoja nikuhaminishe kitu, je,umeshawahi kujiuliza kua ,ni kwanini kanisani maji ya baraka wanaweka chumvi na sio sukari? Jiulize vizuri ndio utahisi kua chumvi  ya mawe ina Siri nzito kuliko haya niliyo kueleza.

Basi tukiwa bado tupo pale njiani Mimi na yule mama mkenya,tukawaza Cha kufanya nini, mwisho yule mama akasema kua twende kwenye nyumba ya mwisho kwa kijana mmoja hua anaringaga Sana wacha tukamkomeshe.Tulishikana mikono na kuruka juu sana na tulipotua , tulitua kwenye paa la nyumba la huyo kijana.Mama akanyoosha mkono juu ikaja dawa flani ya ungaunga akaiweka batini nyingine akaipeperusha kwa kuipuliza .Kisha akasema kua Mustafa hajalala  bado ,huyu kijana ni mbishi Sana,ila muda si mrefu atalala tu. Tukasubiri kidogo baadae tukaingia ndani tena chumbani kwa yule kijana! Tulimkuta akiwa amevalia bukta huku akiwa tumbo wazi na mikono yake ikiwa nyuma Kama ameficha kitu . Niliogopa Sana kwani yule kijana alikua akitutazama sana mpaka nikahisi kua huenda ikawa anatuona. "Mama mbona huyu kijana anatushangaa Sana! Au anatuona?" Nilimuuliza mama .. " mh! Sidhani Kama atakua na uwezo huo!"  Alijibu mama kwa hofu. Lakini tulipo angalia pembeni mwa kile chumba tukayaona marimao kadhaa na sindano zikiwa zinaning'inia juu yake! Mama alishtuka Sana Kisha akasema " tukimbie tunaonekana!!" Wakati huo yeye tayari ameshapiga guu lake chini na kutoweka peke yake.Na Mimi nilitaka kufanya hivyo, lakini kabla sijanyanyua mguu yule kijana alinikamata na sikuwa na ujanja tena!! .


Nilijiona mtu mwenye mikosi Sana kwani ,kila mara Mimi ndio wa kukamatwa tu! Kumbe yule kijana aliweka mtego wa kuona wachawi .Hata wewe ndugu msomaji endapo utachukua malimao au ndimu Saba,na sindano za kushonea nguo kwa mkono saba, Kisha ukachukua kila sindano moja ukaichomeka kwenye ndimu au rimao lake ,usiikandamize Sana,choma juu juu ili sindano ining'inie Kisha chukua hizo ndimu weka eneo ambalo upo Kisha tulia,hapo unaweza ukaona vitu vilivyo jificha visionekane kwa macho.(invisible) Lakini nikuonye usije ukafanya zoezi hili Kama una roho nyepesi ,maana wachawi huwa wanatisha Sana wanapokuja kwako.Kabla hujafanya hivyo jiulize kua baada ya kumwona mchawi utamfanya nini? Je, unaweza kumkamata akiwa na sura ya kutisha? Kama huwezi usijaribu ni hatari Sana.

Basi,nikiwa mikononi mwa yule kijana Mustafa ,sikua na ujanja kwani mchawi ukisha kamatwa huwezi fanya lolote zaidi ya kuokolewa baadae na mchawi mwenzio. " unaitwa nani wewe binti?"  Ilikua ni sauti ya ukari ya yule kijana aliniuliza. " Naitwa chuma" nilimjibu. " Chuma! Hahahaha haa! Chuma leo hunaga bahati " alishangaa yule kijana Kisha akasema .." chuma wewe unaonekana ni binti mzuri Sana ,una umbo zuri ,makalio makubwa Sasa kwanini,unakua mchawi ? Ona Sasa ulivyojiweka Kama kinyago Wakati wewe ni mrembo!!!" Yalikua ni maneno ya yule kijana Mustafa. Mimi sikujibu chochote zaidi ya kuinamisha kichwa chini kwa haibu!!  " Sasa nikufanye nini binti chuma?" Aliniuliza lakini nilinyamaza kimya . Sauti ya hajabu ikapita masikioni mwangu kua nilale kifudifudi ili nipate msaada ,nami nikafanya hivyo muda uleule ,yule kijana Mustafa alishangaa Sana kua nina maana gani ya Mimi kulala pale sakafuni kifudifudi huku makalio yangu yaliyojaa minofu yakiwa juu yakitikisika. " We binti ndio nini Sasa?, Au una nitega? Nitakubaka kweli Mimi mwenyewe nimedata vilevile!" Nilishtuka nilivyosikia yule kijana Mustafa anataka kunibaka ,nilimtazama nikaona taratibu bukta aliyovaa inanyanyuka juu yani tayari alishakua na hisia Kali na Mimi japokua nilikua Kama kinyago lakini Mustafa alivutiwa na Mimi,ama kweli huyu kijana ni jasiri Sana kwa mtu mwingine huwezi kunitazama mara mbili,nilitisha sana.

Taratibu Mustafa akaanza kunisogelea pale nilipolala na akaanza kuyachezea makalio yangu ,nikajua Sasa muda si mrefu huyu kijana atanibaka !!

Nikatulia Kama maji ya kisimani,ghafla mbele yangu namwona yule mama mkenya ananipa mkono ,nami nikamshika  mkono tukapotea na kuibukia nyumbani kwa yule mama mkenya. " Pole Sana binti,hizi ni ajari ndogondogo huwa zinatokeaga maana siku hizi watu wengi wanajua jinsi ya kujikinga na wachawi." "Asante mama "  nilijibu.." ehee! Nambie ,vipi yule kijana Mustafa mbona alikua anakuchezea makalio alikua anataka kukufanya nini? ".   "Alikua anataka kunibaka !!" Nilimjibu . " Kukubaka? Huyu kijana ana hatari kweli na angesubutu kufanya hivyo, basi jua la asubuhi ,asingeliona tena,angekufa.!  Alishtuka yule mama alivyosikia kua nilitaka kubakwa ningari kwenye hari ya vazi la kichawi. Baada ya hapo yule mama akauchukua ungo wangu na kuupigia maombi maarumu Kisha ule ungo ukapotea  kimiujiza. Kisha akachukua lile fagio lenye mti au mpini mrefu akanishika mkono ,akapiga guu lake chini tukatokea njia ya panda .Akaniambia Sasa muda wa kurudi nyumbani Tanzania umefika.Ilikua bado ni usiku Sana Kama Sasa nane hivi! Baada ya hapo akaulaza ule mfagio chini Kisha akanipaka dawa flani nayeye pia akajipaka Kisha tukaukalia ule mfagio.sijui nini kilitokea lakini tukajikuta tupo juu ya anga kwenye spidi Kali zaidi ya ndege za kivita!! Haikuchukua dakika nyingi tukajikuta tupo nje nyumbani kwa bibi. Bibi alitoka nje akiwa kwenye hari yake ya kichawi,akatupokea na akamshukuru Sana mshirika mwenzake raia wa Nairobi Kenya. Yule mama hakutaka kukaa Sana alituaga na akaondoka na usafiri wake kwa haraka. 


*********** ITAENDELEA ***************


Je,nini kitafuatia? Usikose kufuatilia sehemu ya tatu ya URITHI WA BIBI.Uhondo ndio kwanza unaanza. Hujachelewa, fanya ku LIKE PAGE, COMMENT , au SHARE ili wengine wapate kuburudika na kuelimika pia.Asante.

URITHI wa Bibi 1


STORY : URITHI WA BIBI  . Ep.1

AUTHOR : STEVEN MORGAN

EMAIL : stevennemes2k@gmail.com

PHONE : +255659115223


Habari zenu! Bila Shaka mu wazima wa afya! Ndugu msomaji , karibu sana kwenye story hii nzuri yenye kufundisha na kusisimua . Utayajua mambo mengi usiyoyajua au unayo yasikiaga kupitia story hii.

 Kwa jina naitwa chuma mashaka, naishi na bibi yangu kwa Sasa. Katika Kijiji Cha ndolelo kinacho patikana katika safu ya milima ya ulugulu. 

Wazazi wangu baba na mama sikuwahi kuwaona kwani inasemekana ,walifariki Mimi ningari mdogo sana.

Mimi ni binti wa miaka kumi na tano kwa Sasa,naitwa chuma kwa sababu hilo ni jina lenye asili ya kabila ya kilugulu. Yani Kama nitamzaa mtoto wa kike basi angeitwa mwenda au Kama nitamzaa wa kiume basi angeitwa mkude. Yani huo ni mtiririko tu wa majina ya kilugulu.

Kijiji Cha ndolelo ndiko ninapoishi na bibi kwa sasa. Ndolelo ni jina lililotokana  na tabia za kinamama wa zamani walipokua wanakwenda kuuza biashara zao sokoni,na wanaporudi kutoka sokoni,watoto zao  wakiwa nyumbani wanatazama chini bondeni kabisa wanatazamia Kama mama zao wanarudi kutoka sokoni ,Sasa ile sehemu ambayo mama zao au Bibi zao walikua wakikatiza na kuonekana ndio mpaka leo inaitwa ndolelo yani  kwa tafsiri ya haraka ni sehemu ya kuonea/tazamia/angalizia. 


Bibi yangu anajulikana kwa jina maarufu la Bibi mbokeleni, huku neno mbokeleni likiwa na maana ya mpokeeni/nipokeeni. Aliitwa hivyo kwa sababu kila anapobeba mzigo wake huwezi kumpita ,ni lazima umpokee mzigo wake na kuupelaka mpaka kwake ,hata Kama ulikua huna nia hiyo! Sijui kwa nini lakini kiukweli Bibi yangu aliheshimika na kuogopeka sana na watu.


Siku moja Bibi yangu aliniita tukiwa nyumbani "we chuma"  bee bibi,nilimjibu Bibi Kisha nilitoka nje kumsikiliza . " Njoo kaa hapa kwenye mkeka nina mazungumzo muhimu sana na wewe"   "mh!" Nilishtuka kidogo baada ya kusikia kua bibi ana mazungumzo muhimu na Mimi! Sikuhisi kua huenda yakawa mazungumzo yapi! Hivyo,niliamua kuketi kwenye mkeka ili nimsikilize bibi yangu.


"Chuma mjukuu wangu sasa umekua na unajitambua sana.wewe ni mjukuu wangu wa pekee Sina mwingine.kwa Sasa Mimi tayari ni mzee sana ,Sina nguvu tena Kama zamani hivyo, natumaini wewe ndio mtu pekee wa kunipokea mizigo yangu!"

Mizigo gani bibi? Nilimuuliza bibi nikiwa nataka kujua kua ni mizigo ipi anayotaka kupokewa.  " Usiwe na haraka chuma! Hivi si unakumbuka jinsi watu walivyokua wakiniheshimu!,na mashamba yangu watu wakiyaogopa ? Mpaka ndizi zinaivia juu lakini haziibwi?"   Ndio Bibi nakumbuka sana na mpaka Sasa bado nalijua hilo kua watu wanakuheshimu mpaka wanakuogopa!  Nilimjibu Bibi Kisha bibi akaniwahi kwa kuniuliza " unajua ni kwa nini ,watu wananiheshimu na kuniogopa Mimi na mari zangu?" "Hapana Bibi sijui!" Nilimjibu kwa haraka. "Je,na wewe unapenda uje kuheshimika na kuogopwa wewe na mari zako?"  Ndio Bibi napenda kuheshimika lakini sipendi kuogopwa maana nitakosa marafiki! Nilimjibu Bibi huku nikiwa sijui dhumuni la Bibi kwangu!  "Hahahaha, hahahaha!" Alicheka sana Bibi baada ya kumjibu hivyo! " Chuma wewe ndio chuma changu ninacho kitegemea kwa Sasa na baadae, hivyo sitaki uniangushe , kuna kazi nataka nikuachie,ni ngumu lakini ni nyepesi nikikufundisha.Wakubwa wamekuchagua wewe ,kuna mizigo nataka unipokee,ni mizito lakini ni myepesi ukisha ibeba.Utaheshimika sana ,utafanya lolote unalolitaka duniani."   " Sawa Bibi nimekuelewa lakini hao wakubwa walio nichagua ndio akina nani?" Nilikubali Kisha nikamuuliza Bibi.   " Wakubwa ni viongozi wetu, huwezi kuwaona mpaka na wewe uwe mwanachama." " Mwanachama?"   "Ndio ,bila kua mshirka huwezi kuwaona wakubwa,usiwe na haraka muda si mrefu utawajua tu,hebu nenda kapike kwanza maana Mimi njaa imeshaanza kuniuma ." Alinijibu hivyo Bibi Kisha Mimi nikanyanyuka kwenye mkeka na kwenda jikoni kupika.

Nikiwa jikoni kwenye kibanda kidogo Cha miti kilichoezekwa kwa vipande vya mabati ya madebe,bibi akaja nae akaketi pembeni kwenye kigoda au kiti Cha miguu mitatu. Niliendelea kupika huku bibi akiendelea kuzungumza . Alizungumza mambo mengi sana mpaka mwishoni nikahisi kabisa kua huenda Bibi akawa ni mchawi japo sikuwahi kumshuhudia lakini nasikiaga tetesi mtaani kua bibi ni mchawi. Na ndio maana na Mimi pia mtaani watu wazima na watoto wenzangu pia hua wananiogopa kwani hata nikiwakosea hua hawaniadhibu Kama watoto wengine wanavyo adhibiwa!! 

Chakula kiliwiva nikatenga kila kitu na tukala palepale jikoni . " Inamaana we chuma unataka kuniambia kua hujawahi kusikia tetesi zozote kuhusu Mimi huko mtaani?"  "Nasikiaga bibi "  , " mbona huniambiagi Sasa ! Unachokisikiaga huko?"  " Hapana bibi sikuambiagi kwa sababu ninacho kisikiaga ni kibaya sana lakini pia hua siamini kile ninachokisikiaga kwa watu!!"  Bibi aliendelea kuniuliza , "Sasa niambie unasikiaga nini kwa watu wakisema kuhusu Mimi?"  " Watu huwa wanasema kua wewe ni mchawi,lakini Mimi siamini !!" Nilimjibu Bibi bila woga Kisha bibi akasema " unajua watu wanachukulia Kama uchawi ni kitu hatari sana kuliko kitu kingine,lakini kiukweli uchawi ni kinga na ulinzi Kama ulinzi mwingine.Anaye shika panga au bunduki au bomu ujue anataka kujilinda.Na anayeshika uchawi pia huyu nae hana tofauti na aliye shika bunduki au panga .labda uchawi huenda ukawa na nguvu nyingi kuliko panga au bunduki ndomana unaogopeka na watu"  "mjukuu wangu usiku wa leo nataka nikuoneshe jinsi uchawi ulivyo ili usije ukauogopa sawa chuma?"  "Ndio Bibi !!" Niliitikia kwa woga kwani kwa maongezi ya Bibi tu,tayari nimeshaanza kumwogopa.


Kiza kilishamili, ilikua ni usiku wa saa mbili.Bibi aliniambia tuingie ndani ili anioneshe huo uchawi unao zungumzwa.

 

Nilikua na hamu kubwa sana ya kuuona huo uchawi ukoje! Tukaingia ndani ndani kabisa kwenye chumba Cha Bibi .Bibi alitoa kapo kubwa mvunguni mwake likiwa limejaa tunguli /vibuyu mbalimbali na madawa mengi ya miti shamba.Niliogopa sana lakini ilinibidi nivumilie kile ninacho kiona.

"Chuma ,Mimi ndio Bibi mbokeleni,Sasa si unaliona hili kapo? " Ndio Bibi,naliona. Nilimjibu Bibi kwa woga. " Hivi vitu unavyoviona kwenye hii kapo ndio vifaa vya uchawi ila uchawi ni maneno yako mwenyewe!, Huu muda ni saa mbili usiku,bado mapema sana ila ndio muda pekee ya wachawi kujiandaa kwa shughuri zao za kiwanga na kichawi.maandalizi yanafanyika muda huu  Kisha kuanzia saa sita za usiku ndio cheketu zinapoanza japo unaweza kucheketua muda wowote lakini mida hiyo niliyokwambia ndio mizuri!"  Duh! Bibi aliongea maneno ya kutisha sana ambayo sikuwahi kuyasikia.   " Chuma hebu shika hiki kibuyu" nikakishika kibuyu Kisha Bibi akachukua kibuyu kingine kwenye lile kapo Kisha akasema maneno kwa sauti kubwa mpaka niliogopa!!  " Wakubwa!, wakubwa,chuma amekua Sasa na leo ndio ile siku ambayo tuliyokua tunaisubiri kwa hamu ,tumkabidhi mizigo yake mapema!!"  Bibi aliongea kwa sauti kubwa mpaka nikamwambia " Bibi punguza sauti watu watatusikia huko nje " " chuma kuanzia Leo ujue kua mchawi hua anong'oni,ukisha vaa vazi lako la kichawi hutakiwi kuongea taratibu kwani kila mtu atakusikia,unatakiwa kuongea kwa sauti kubwa na hata ukicheka ,cheka kwa sauti kubwa ukiwa ndani ya vazi la kichawi tu!!"

 Bibi alinipa Siri hiyo Kisha akaendelea kuchanganya madawa na akanipaka usoni nikawa Kama kinyago Cha mpapule! Akachukua kile kibuyu alichokishika Kisha akaniamuru niasame mdomo ,nilitaka kukataa lakini nikajikuta nafanya hivyo bila ubishi. Akanimiminia kitu Kama majimaji ya asali mdomoni kutoka kwenye kile kibuyu .Nasema asali sababu ilikua tamu sana . Akanichanja chale na nyembe mwilini kisha akachukua dawa ya unga kwenye lile kapo,aknipaka mwilini,muda huo nipo uchi kabisa wa mnyama. Ila nilipomtazama Bibi ,nilimuona amevaa kipande Cha kaniki kiunoni ,huku mwili wake ukiwa umegubikwa na madawa ya ungaunga yani nae alionekana Kama kinyago Cha mpapule ila kinachotisha sana.

Baada ya hapo ,bibi alisema kua maandalizi yamekamilika na hapo tayari tumeshavaa mavazi ya kichawi. " Bibi mbona wewe umevaa, warau hiyo kaniki mbona Mimi nipo uchi kabisa ?" Nilimuuliza bibi.." hata Mimi pia nakuona wewe umevaa kaniki na mimi pia najiona niko uchi!! Kiukweli hapa tuko uchi kabisa ila mtu yeyote akibahatika kutuona ,basi atatuona Kama tumevaa kaniki kumbe tuko uchi kabisa."   Bibi akatoa mifagio miwili ,mmoja ule wa ndani uliotengenezwa kwa kindu,na mwingine wa nje ulitengenezwa kwa mti mrefu na njerewa za mikuti ya mnazi. Kisha akaleta na ungo unaotumikaga sana kupepetea nafaka. Vitu hivyo vyote alivitoa mvunguni kwake japo kwa miaka mingi sikuwahi kuviona na wala sionagi chochote .

Baada ya hapo akaniambia.." unaviona hivi vitu? Mifagio na ungo! Hivi vitu ni aina za usafiri tunao utumia katika shughuri zetu,huu mfagio mdogo wa ndani  hutumika kwa safari fupifupi za ndani ya mkoa.Na huu ungo hutumika kwa safari ndefundefu za ndani ya nchi,yani mkoa mpaka mkoa .Na huu mfagio mkubwa wa mti ,huu hutumika kwa safari za masafa marefu ya nje ya nchi,iwe ulaya au popote pale japo hata ungo pia hutumika kwa masafa marefu ya ndani na nje ya nchi."

Duh! Usiku huo Bibi alinifundisha mambo mengi sana .

" Sasa mjukuu wangu chuma umeshakua chuma,Sasa kilichobakia ni vitendo tu!" " Kama nilivyo kwambia kua sehemu kubwa ya uchawi ni maneno yako mwenyewe,Sasa ukisha vaa vazi la uchawi unaweza kuongea chochote na kikawa Kama unavyotaka" alizidi kuongea Bibi. " Sawa Bibi lakini mambo hayo yanawezekana vipi?" Nilimuuliza bibi.." unataka kujua ngoja nikuoneshe!, Hebu tazama kwenye kiganja changu ,Sasa hivi namuamuru zefania atokee hapa kwenye kiganja changu ,na iwe hivyo!!" Duh! Huwezi amini kweli aliyoyasema Bibi ndivyo ilivyokua ,nilimuona mmama mmoja aliye muita kwa jina la zefania akiwa amesimama juu ya kiganja Cha Bibi!!. 

" Usijari chuma muda si mrefu utayajua yote haya" na usiku wa leo nitakufundisha kuendesha hizi aina zote za ndege za kichawi na kuwasumbua watu majumbani mwao." " Sawa Bibi lakini ni kwanini tuwasumbue watu bila kosa?"  " HataMimi sipendi watu wasumbuliwe lakini kazi zetu ndizo zinaitaji ufanye hivyo kwani kwa kufanya hivyo ,unakua na nguvu nyingi sana ,kinyume na hapo,utakua dhaifu sana."   Basi kwakua muda ulisha kwenda sana ,bibi mbokeleni akachukua ungo Kisha tukatoka nje na kuelekea njia ya panda, tulitembea bila kuonekana na yeyote ila mbwa walitubwekea sana tulipokatiza kwenye nyumba zenye mbwa,niliogopa sana lakini Bibi aliniondoa hofu . Tukafika kwenye njia panda nne ( 4ways cross road) tukasimama katikati ya njia nne ,Bibi aliweka ule ungo pale chini Kisha akachota vumbi la ile njia ya panda akaweka kwenye ule ungo Kisha ghafla kikatokea kichwa Cha mtu ambaye macho yake yakiwa yanatazama ,akakiweka kwenye ungo Kisha akanyosha mkono wake juu na akaita aina flani ya dawa ikaja palepale mkononi,niliogopa sana ilinibidi nimuulize.." Bibi vitu hivyo vinatoka wapi?" "Hahahaha!, Chuma umeshakua subiri uyaone, mjukuu wangu chuma uchawi una mambo mengi sana,yani Kama ungekua unafundishwa daraeani elimu hii,usingeweza kushika kila kitu kichwani!, Hivi vitu nilivieka mbali sana na vipo vingi sana siwezi kuvibeba na kutembea navyo,hivyo popote ninapokua ,ninachokihitaji ,nakiita kwa kukiamuru kwa imani kali ,kinakuja mpaka nilipo haina haja ya kubeba furushi kubwa la mzigo utachoka chuma,haa haa haha haaa haaahaaaa!" Alimalizia kwa kusema hivyo bibi, Kisha akacheka sana mpaka nikaingiwa woga. Basi baada ya hapo kile kichwa baada ya kuwekwa juu ya ule ungo na kumimina baaadhi ya dawa za ungaunga na damu ,Bibi aliongea maneno akiamuru ule ungo utanuke uwe mkubwa was kuenea watu wawili,ikawa hivyo !nikapanda juu ya ule ungo baada ya kuambiwa na Bibi ,Kisha Bibi nae alipanda na kunifundisha maneno fulani ya kiufundi,baada ya kumuelewa ghafla ungo ukaanza kunyanyuka na kwenda juu ya anga.  "  Bibi mbona Sasa usafiri huu hauna usukano?" (Staring wheel) nilimuuliza bibi baada ya kuona kua kile chombo kinakwenda hukuu sisi tukiwa tumetulia . " Hiki chombo mjukuu wangu msukano wake ni akili yako yani vile unavyo waza wewe ndivo chenyewe kinavyotenda kwa mfano hapa Mimi na waza kuzunguka zunguka kwenye mawingu tu ,Kama unavyoona nacho kina fanya hivyo na nikiwaza kutua au kurudi nyumbani ,mara moja kwa haraka kinanirudisha, hata na wewe mwenyewe siku ukiwa peke yako fuatisha Kama ninavyo fanya sawa?"   " Sawa bibi, " nilimjibu Kisha nikakaa kimya , tuliendelea kuyakata mawingu,Kisha Bibi akakiamuru kile kifaa watu hukiitaga kibeku kitupeleke kwa haraka nchi jirani ya Kenya mjini Nairobi.

Sijui nini kilitokea lakini nilihisi upepo mkari ukinipuliza kwa kasi mpaka nikahisi   kufakufa!! Ghafla tukajikuta tunatua mjini Nairobi ,tulitua kwenye njia panda moja ambayo Bibi si mara yake ya kwanza kufika hapo,maana alionekana kuijua mitaa vizuri Sana. " Usijari  chuma nataka nikutembeze mitaa yote ya Nairobi kwa muda  mchache Kisha turudi nyumbani si utafurahi?". " Ndio bibi nitafurahi sana" nilimjibu Bibi huku nikiwa na furaha moyoni. Tulipumzika kidogo Kisha bibi na Mimi tukapanda chombo chetu ,na kuanza kukatiza mitaa,huwezi amini sijui ilikuaje lakini tukajikuta tunatikisika Kama vile tunatingishwa mara ghafla chombo kimeenda mlama tukajikuta tupo chini kwenye uwanja mkubwa wa jengo la kanisa la kiroho. " Mama wewee! mjukuu wangu umekwisha ,Sina jinsi lakini unisamee"  Bibi aliongea hivyo,sikumuelewa lakini nilikuja kumuelewa baadae, nikataka kumuuliza kitu Bibi kua mbona tumekwama pale inakuwaje?    Lakini Bibi kabla hajajibu ,akapaa angani juu sana na kupotea Kisha nikasikia sauti masikioni mwangu ikiniambia kua kesho asubuhi ikifika   nilale kifudifudi ili nipate msaada ,zaidi ya hapo nitaumbuka.Nikawa Sina Cha kufanya ikabibi nibakie pale Mimi nikiwa uchi na ungo wangu .Sijui Cha kufanya nikangoja asubuhi ifike ili zijulikane mbivu na mbichi. ........... .......      ......................


*********** ITAENDELEA ************


Je,nini kitamkuta binti chuma baada ya kuachwa na Bibi kwa mzee kenyata kwenye uwanja  wa kanisa la upako wa kiroho? Je, bibi amekwenda wapi? Usikose sehemu ya pili ya URITHI WA BIBI,.  Uhondo ndio kwanza unakorea. Fanya ku like page , share na wengine wapate kuburudika na kuelimika.

URITHI wa Bibi 15

 Story... URITHI WA BIBI EP.15. Mwisho. Mtunzi....Steven Morgan 📲......... 0659115223 Naam kwa Mara nyingine tena ndugu msomaji tumekutana ...