Ijumaa, 8 Novemba 2024

URITHI wa Bibi 13

 Story........ URITHI WA BIBI EP. 13


Mtunzi........ Steven Morgan


📲.............. +255 659 115 223


Karibu ndugu msomaji katika mwendelezo wetu wa story yetu tamu,ikiwa tunaelekea elekea mwisho kabisa.

Basi,Kama kawaida pale tulipoishia ndipo tunapo anzia.


ILIPOISHIA episode 12..


Mume wangu Sadiki alikurupuka bila kudai chochote kisha akachukua begi lake akalibeba mgongoni bila kunawa uso akaondoka. 

Alipokua barabarani nami nilimfuatilia nyumanyuma nikiwa kwenye hari ya kichawi ya kuto onekana na mtu wa kawaida. Niliona gari ndogo likija kwa Kasi upande ule ambao Sadi alikuwepo ,nilimzubaishasadi kichawi na kumpa kizunguzungu Cha ghafla,akajiingiza mwenyewe barabarani kwenye kumi na nane ,dereva alishindwa kumkwepa Wala hakupiga bleki ,alimgonga Sadi kwa Kasi ileile aliyo kua anakuja nayo!! 

Sadi alipezwa juu Kama karatasi akatua chini kwa kujipigiza kwenye Rami,alipasuka vibaya Sana !!!!   Kisha Mimi nikaenda kwenye mwili wa Sadi nikafanya yangu Kisha nikaondoka bila kuonekana na mtu.

Nilirudia nyumbani na kuendelea na shughuri zangu. Baada ya masaaa kadhaa ,taarifa zilinifikia na kila mtu alikua kua Sadi amepata hajari amefariki.mwili wa Sadi uliifadhiwa mochwari na ulichukuliwa na ndugu yake mmoja kesho yake Kisha ukasafirishwa kwenda kwao,Mimi sikutaka kwenda sababu sikutambulika na ndugu yake yoyote hivyo waliniona Kama  awala tu!


.............. Endelea.......🔋👇👇ep.13


Basi ndugu msomaji kiukweli Sadi  mpenzi wangu ,ndio tayari nimesha muweka ndondocha au Msukule kwa muda kabla ya kifo chake Cha ukweli.


Ndugu msomaji labda ulikua hujui tu,ila kiukweli mtu kabla ya kuchukuliwa Msukule huwa wachawi Kwanza wana andaa kisa ambacho baadae hugeuka mkasa kamili wenye ushahidi kamili machoni pa watu. 

Mfano Kama mpenzi wangu Sadi alivyo patwa na mkasa wa kugongwa na gari ,na watu walimuona  alivyo gongwa,hivyo kisa Cha Sadi kufa ni gari . Labda Kama utataka kujua ukweli harisi wa kifo Cha utata Kuna baadhi ya ishara mbalimbali unaweza kuziona eneo la tukio au kwenye mwili wa marehemu. Au una weza kwenda kwa mganga kuchunguza 

zaidi.

Sadiki nilimficha mvunguni mwa kitanda changu mpaka ule mwili wake wa uongo utakapo zikwa ndipo na sisi tunaanza kuutumia ule mwili wa ukweli ukiwa na nafsi yake iliyo hai.

Ndugu wasomaji ninaposema Sadiki nimemficha chumbani kwangu mvunguni, haina maana kwamba ,ukija kuingia chumbani kwangu na kupekua mvunguni ndio utaona chochote Cha kushangaza, kiukweli ukija na macho yako mawili ya wazi huwezi kuona chochote zaidi ya kuona kweupe tu!!! Labda uwe umechanjia dawa au uwe umepata upako  wa maono kutoka kwa Mungu mwenyewe zaidi ya hapo huwezi kuona chochote. Na unaweza kukaa na mtu mchawi chumba kimoja kwa muda mrefu na usione chochote kile ndani zaidi ya kuhisi .


Basi,siku moja hasubui nilitulia zangu nyumbani,Mara ghafla akatokea yule Mama yangu mkenya, alikuja kuniambia kua Usiku  wa siku hiyo natakiwa kumpeleka Sadi kilingeni maana siku zilishaenda Sana na miezi kadhaa ilipita .Hivyo , wanachama wenzangu walikua wanahitaji kula  nyama ya zamu yangu..

"Chuma leo ndio siku ambayo mkuu amenituma nije kwako kukupa habari kua umpeleke Sadiki leo akawe chakula chetu,maana kila mtu katika jamii anajua kua Sadi alisha kufaga muda"

Aliongea yule Mama mkenya.


"Sawa mamangu basi naomba leo tushinde wote hapa kwangu Kisha Usiku tuondoke wote."

"Usijari Chuma tupo pamoja ,ndomana nilichaguliwa kukusaidia."


Basi tulishinda wote nyumbani kwangu ,tulipika tukala , story nyingine ziliendelea.

Atimae Usiku uliingia tulikula kisha tukaanza kujiandaa mida ya saa mbili Usiku, 

Ndugu msomaji Mara nyingi mchawi huwa hujiandaa na Safari yake kuanzia saa mbili kamili usiku, na mchawi hana muda maarumu wa kuwanga  au kumchezea mtu,hata asubuhi au mchana mchawi anaweza kukuwangia au kukuchezea.

Basi tulijiandaa vya kutosha na yule Mama mkenya Kisha mida ilipofika ya Usiku wa wachawi tukaondoka kuelekea kilingeni,tuliwakuta wachawi wengi Sana walioanza kufika wakiendelea na utaratibu.

"Chuma bila kupoteza muda naomba tuletee mnyama wetu hapa , tuendelee na utaratibu wetu hapa."


Aliongea mkuu kwa kumaanisha kua nimlete Sadiki pale kwa kutolewa sadaka.Nami kwa kutumia maneno ya kichawi ya mamraka,nikamwita Sadiki kutoka kule chumbani kwangu mvunguni. Huwezi amini ndugu msomaji,ila kilichotokea ni Sadiki alitokea palepale kilingeni akiwa Kama zuzu.


Mkuu akanyoosha kidole chini 👇 Mara ghafla! Akatokea mbuzi mkubwa wa kiume ( beberu) Kisha akaja mchinjaji akiwa ameshika bisu kubwa lenye makari Kama nyembe . Yule mchinjaji akamlaza mbuzi chali na kumshika miguu ya mbele,Mar ghafla! Sadiki pale aliposimama nae alianguka ,Kisha mchinjaji akaanza kumchinja yule mbuzi, mbuzi alilia Sana! Lakini pia nae Sadiki,alilia Sana huku mikono yake miwili ikishikilia shingo yake ili isidondoke au isidhurike kwa maumivu aliyo kua akiyapata.


Ndugu msomaji hakuna urogi mbaya Kama urogi wa mbuzi,Yani unapoona mbuzi anatolewa sadaka ujue,kuna Jambo zito linaenda kutokea .


Basi, mbuzi alichinjwa mpaka akafa,huku ulimi ukiwa nje,pia Sadiki nae ,alikufa huku ulimi upo nje na macho yalimtoka Kama fundi saa. 

 

Kamati ya chakula iliandaa msosi Yani nyama ya Sadi ,tukala na tulikunywa pia damu yake iliyo kingwa.


Ndugu msomaji najua unaweza kujiuliza swali moja ,kwamba ,kwa nini wachawi wanakunywa damu za kila mtu hata kama mtu akiwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi ila mchawi anakunywa damu ya mgonjwa huyo na yeye hapati maambukizi yoyote,zaidi ya kuwa salama !!!!!!

Ndugu msomaji kiukweli, wachawi wanapokua katika maumbile yao ya kichawi huwa Kama wanyama na si watu,na ndomana huweza kula hata nyama mbichi kitu ambacho mwana Adamu wa kawaida hawezi. Kiukweli kile anachokula mchawi ,hari yeye bali mchawi hutumika Kama njia ya kuwashibisha mapepo au mashetani wanayo yaabudu.  Japo wanapokula radha ya chakula huisikia lakini wanao Shiba ni viumbe wengine. Hata chakula kingekua na sumu mchawi ana uwezo wa kula bila kudhurika .


Basi ,tulikula nyama na kunywa damu Kisha tukacheza ngoma za kikwetu kwetu. Baadae mkuu alionge.


" Ndugu zangu shughuri yetu imeisha kilichobaki Sasa,kila mtu apotee hapa arudi kwake akalale au Kama utataka kwenda kuwanga kidogo ruksa, ila naomba Chuma na mama mkenya mbaki hapa Kuna kazi nataka kuwapa."


Mkuu alipomaliza kutoa maagizo kila mtu,alitoweka isipokua Mimi ,mama mkenya na mkuu tulibakia kwa mazungumzo kidogo.


" Chuma ukisaidiwa na mama hapo, kesho mida ya saa Saba mchana,naomba muende kwa bosi wako mzee foya mkamroge ili afe ,ili ulipe kisasi Cha Bibi yako Mbokeleni ila mke na watoto wake msiwaguse hawana hatia. Baada ya kazi hiyo,kuna kazi ya mwisho kabisa ya kwenda kukabiriana na yele Mganga wa morogoro mgeta anae itwa Alumbile Kalumba."

"Sawa mkuu tumekuelewa"


Tulimuaga mkuu Kisha tukatoweka,ninaposema tulitoweka nadhani unaelewa ndugu msomaji Yani tulifutika Kama mwanga wa radi na kuibukia kwenye chumba changu,ilikua ni Usiku Sana bado. Tililala kuitafuta asubuhi.


Asubuhi ilifika ,tulioga Kisha tuka andaa chai tukanywa Kisha tukaanza kujiandaa na Safari iliyopo mbele yetu.

Mida ilizidi kwenda,tulishajiandaa kikazi, hatimaye saa Saba ikaingia! 


Bila kupoteza muda tukapotea na kwenda kuibukia kwa mzee foya nje ya nyumba yake,tukaangalia usalama ,tukagundua kua mke na watoto wa mzee foya pamoja na mfanya kazi wao hawakuwepo pale nyumbani ,walienda kula likizo nyumbani kwa mke wa mzee foya ila tulihisi kwa muda ule Kuna watu Kama wawili ndani chumbani kwa mzee foya.


Ndugu msomaji, tulitoweka tena na kuibukia sebuleni kwa mzee Foya,tulitulia kimya Mara tu ! Tukaanza kusikia miguno na sauti za mahaba kutoka chumbani kwa mzee foya ,nikatazama kiganja changu ,nikamwona mzee foya akiwa ana mla uroda binti mdogo Sana Kama wa kidato Cha nne hivi!!!


"Kumbe huyu mzee mshenzi namna hii?"

Aliongea yule Mama mkenya.


Baada ya hapo tukatoweka andaa mtego wa jini makata chooni kwa mzee foya  ambacho kilikuwepo kulekule ndani kwa mzee Foya Yani chumba chake kilikua ni masta. Tulilituma lile jini chooni kwake . Kisha tulitulia pale sebuleni kusikilizia mtego, mzee foya aliendelea kumgeuza mtoto wa watu Kama chapati huku binti akaendelea kutoa kilio Cha furaha kilicho changanyika na sukari ya zuchu.


Tuliendelea kusubiri Kisha tukaroga ili mzee foya ajisikie kwenda chooni,mida ileile tulisikia sauti ya binti akilia kilio Cha ukweli na sio Cha mahaba ,yule binti akatoka mbio akatupita pale sebuleni bila kutuona akatoka nje huku akiwa amejifunga kanga moja ,akaondoka zake ,nasi tulienda hadi chooni kwa mzee foya na kumkuta ametoa macho huku damu zikimtoka puani. Tukajua kua tumesha maliza mchezo ,tulicheka Sana Kisha tukatoweka kurudi nyumbani.


..............Itaendelea...................


Je,mzee foya atakua amekufa kweli?

Je,mganga Alumbile Kalumba wa Moro mgeta atawezekana? Usikose kufuatilia sehemu ya 14 ya URITHI WA BIBI.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

URITHI wa Bibi 15

 Story... URITHI WA BIBI EP.15. Mwisho. Mtunzi....Steven Morgan 📲......... 0659115223 Naam kwa Mara nyingine tena ndugu msomaji tumekutana ...